Na Mwandishi wetu, Babati
TAASISI
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoani Manyara, inamshikilia
karani wa Mahakama ya mwanzo Magugu Wilayani Babati, Alfred Jackson
Ntatirwa kwa kudaiwa kuomba na kupokea rushwa ya shilingi elfu 30 ili
ampatie mwananchi nakala ya hukumu.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Babati, Mkuu wa TAKUKURU
Mkoani Manyara, Holle Joseph Makungu amesema tukio hilo limetokea Aprili
6 mwaka huu mji mdogo wa Magugu.
Makungu
ameeleza kuwa Ntatirwa anadaiwa kufanya makosa hayo kinyume na kufungua
cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11/2007.
Amesema
karani huyo Ntatirwa anatuhumiwa kuomba rushwa ya shilingi elfu 30 na
kukamatwa na maofisa wa TAKUKURU akiwa amepokea kiasi hicho cha fedha
ili atoe nakala ya hukumu ya kesi.
Amesema
Ntatirwa aliomba fedha hiyo ili amsaidie mtu mmoja aliyeomba nakala ya
hukumu ya kesi iliyokuwepo mahakama ya mwanzo Magugu ambaye hakuridhika
na hukumu hiyo na alitaka kukata rufaa mahakama ya Wilaya.
Ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote ili akajibu mashtaka hayo yanayomkabili.
"Wananchi
wote wanapaswa kufahamu kuwa hawalazimiki kulipia tozo yoyote
inayohusiana na nakala za hukumu na maamuzi ya mahakama Kuu, mahakama ya
Hakimu mkazi na mahakama ya mwanzo," amesema Makungu.
Amesema
Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Hamis Juma alikwashatoa
maelekezo kwa mahakama zote nchini kuwa hawatalazimika kulipa tozo
yoyote kuhusiana na nakala za hukumu na maamuzi mbalimbali kwa maana ya
Judgement, Rulings, Order, Decrees and Drawn orders.
"Kwa
hiyo mwananchi yeyote akidaiwa fedha katika orodha hiyo fahamu kuwa ni
rushwa na unapaswa kutoa taarifa TAKUKURU kwa kutumia namba za dharura
111 ili hatua stahiki zichukuliwe," amesema Makungu.
Mkuu
wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU Mkoani Manyara,
Holle Joseph Makungu akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
mjini Babati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...