Na Woinde Shizza ,Michuzi Tv

Mchimbaji mdogo  wa Madini ya Ruby yaliyopo katika kata ya Mundarara wilayani Longido Mkoani Arusha Sendeu Laizer amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kubaini mwenendo usioridhisha wa ukusanyaji kodi pamoja na kuruhusu wachimbaji Madini kuendelea kuchimba Madini

Aliyasema hayo leo wakati akizungumza na Vyombo vya Habari, ambapo  alisema kuwa baada ya kuwaapisha Mawaziri Ikulu Chamwino jijini Dodoma, Rais Samia alimtaka Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba kutanua wigo wa ukusanyaji kodi akionya kile alichokiita kuwaua walipa kodi kwa kufunga biashara zao, kuchukua fedha na vifaa vyao vya kazi pamoja na kufunga akaunti zao.

Alisema kuwa kauli hiyo imerejesha amani kwa wafanyabiashara na itaongeza uwekezaji chini Katika sekta mbalimbali ikiwemo ya madini

“Tunampongeza sana Rais na tunamuunga mkono ambacho kilikuwa kinafanyika ni kibaya sana, watu kuvamia katika biashara, kufunga akaunti na kuchukua fedha,  kwa nchi nyingine ni kesi kubwa tunamuombea mungu aendelee kumlinda," alisema.

Alisema kauli hii itasaidia sasa wafanyabiashara kuendeleza biashara zao na kulipa kodi ya Serikali lakini bila kuua biashara zao

 Sendeu Laizer ambaye kampuni yake hivi karibuni  ilipewa  tuzo na serikali ya upambanaji kwa jitiada kubwa alizofanya bila kukata tamaa ,ambapo alizingatia sheria zote za nchi pamoja na sheria zote za uchimbaji wa  madini  ,uhuzaji wa madini na uhusiano

Alisema tuzo hiyo  alikabidhiwa na Rais wa sasa wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia 
Tanzania na amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Samia Suluhu  kwa niaba ya hayati Rais magufuli kipindi alipokuwa makamu wa rais. 

 cha kutambua mchango wake sekta ya biashara ya madini ya vito, amesema  Rais ameonyesha huruma kwa wafanyabiashara na watahakikisha wanahamasishana kulipa kodi. 

Aidha alimpongeza Rais kwa kuweza kuhamasisha  uchimbaji wa madini , kwani utawezesha wawekezaji wengi wa ndani na nje kujitokeza kuja kuchimba Madini hayo.

Aliwapongeza watanzania kwa ujumla kwa kuendelea kutunza amani na mshikamano wa nchi yetu ,ambapo aliwasisitiza watanzania kuendelea kumuenzi hayati Rais John Magufuli ambaye aliwaonyesha watanzania njia ya kuthubutu kwamba wanaweza wakafanya mambo yakaenda sawa.
 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi bilionea Sendeu Laizer tuzo wakati alipokuwa  Makamu wa Rais.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...