*Wachekeshaji watakiwa kuipa kipaumbele Sanaa ya uchekeshaji

Na Khadija Seif Michuzi Tv

WASANII wa Vichekesho watakiwa kuijengea heshima tasnia hiyo.

Akizungumza na Michuzi Tv Conrad Kennedy maarufu Kama "Coy Mzungu" amesema kuwa tasnia hiyo ya uchekeshaji imekua ikidharaurika kutokana na wasanii wenyewe kutoipa kipaumbele na kuijengea heshima Kama tasnia zingine.

"Tunajiweka Sana nyuma matokeo yake unakuta tunadharaurika mno wakati Miongoni Mwa tasnia ngumu katika Sanaa ni uchekeshaji ni unatumia akili na maarifa Kumtoa mtu mawazo na kumfanya acheke na kusahau kwa wakati huo."

Mzungu amesema kuwa kupitia Kampuni yake ya "Cheka tu" imeamua Kuandaa Mashindano ya Kusaka vipaji vya Ucheshi yanayotarajia kuanza kufanyika mapema April mwaka huu.


"Mashindano hayo yanalenga Kuzalisha vipaji vya fani ya ucheshi si Kwa ajili ya Kusaka washindi pekee balu Kuinua vijana wenye uwezo."


Pia amesema Mashindano hayo yatafanyika katika Mikoa mitano ikiwemo Mwanza,Arusha,Mbeya,Dodoma na Dar es salaam ikijumuisha pande 3 wakiwemo washiriki,majaji na watazamaji na Majaji Kutoka wasafi Media Zembwela pamoja na Baba levo.

Mshindi wa Kwanza atazawadiwa Milioni 10 ,Mshindi wa pili Milioni 5 pamoja na Milioni 2 pamoja na kuwezeshwa kukuza vipaji vyao kwa kusainiwa kufanya kazi na "Cheka tu" huku dalali mwanamke akiwazawadia washindi watatu viwanja.











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...