Kufuatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akizungumza na Wazee wa jiji la Dar es salaam, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi hilo huku akiwaagiza Wenyeviti wa serikali za Mitaa kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi vitakavyosaidia kukomesha vitendo ya kihalifu.

 IGP Sirro amesema hayo leo wakati akiongea na maofisa wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam huku akiwapa mwezi mmoja makamanda hao kuhakikisha wanakomesha vitendo vya uhalifu katika jiji hilo.

Aidha, IGP Sirro ameendelea kusisitiza hasa kwa watu wanaopata msamaha wa vifungo kutoka gerezani kuacha kujihusisha na vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani ambapo amesema Jeshi la Polisi litaendelea kutumia sheria zilizopo ili kuwashughulikia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...