Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akikata utepe ili kuzindua Kitabu cha Historia ya Maisha ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Convention Centre Jijini Dar es Salaam leo tarehe 08 Mei, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akinyanyua juu Kitabu cha Historia ya Maisha ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi mara baada ya kukizindua katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Convention Centre Jijini Dar es Salaam leo tarehe 08 Mei, 2021.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi akinyanyua juu Kitabu cha Historia ya Maisha yake mara baada ya kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Gari Jipya Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Mkewe Mama Sitti Mwinyi mara baada ya kuzindua Kitabu chake cha Historia ya Maisha yake ili liweze kumsaidia katika shughuli mbalimbali za usafiri.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi akizungumza na viongozi mbalimbali waliofika katika uzinduzi wa Kitabu chake cha Historia ya Maisha yake katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Convention Centre.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya Maisha ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Convention Centre.

PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...