Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
SHEIKH
Mkuu wa mkoa wa Pwani, Hamis Mtupa ,amekemea vitendo vya ubakaji
hususan kwa watoto ,vitendo vinavyodaiwa kushamiri katika baadhi ya
maeneo ,na kuiomba jamii kushirikiana kupiga vita vitendo hivyo.
Aidha ameitaka jamii kusimamia maadili na kudumisha tamaduni za kitanzania ,bila kuendekeza masuala ya utandawazi.
Alitoa rai hiyo katika sikukuu ya Eid pili na baraza la eid lililofanyika Misugusugu Kibaha Mjini .
Mtupa
alieleza, masuala ya ubakaji ni masuala ya kipolisi na ni mamlaka
inayopaswa kuzungumzia zaidi hali hiyo ,lakini wameagizwa na vitabu vya
dini kukemea maovu ikiwemo ubakaji na uhalifu mbalimbali.
Alibainisha
kwamba, hivi karibuni alihudhuria hafla ambayo Jeshi la polisi Pwani
lilithibitisha vitendo hivi kuongezeka ukilinganisha na matukio ya ajali
ambayo kwasasa yanapungua mkoani hapo.
"Nililibeba
hili ,kwakuwa limegusa jamii, na vitabu vya dini vinaruhusu kukemea
nimepanga kila ninaposimama kuongea basi nitakemea hili ,na nawaomba
viongozi wengine tusiliache hili linakua kwani watoto wanazidi kufanyiwa
ukatili huu" alisema Mtupa.
Mtupa
aliwataka ,viongozi wa serikali za mitaa kusimamia matukio hayo
yasitokee na endapo yakitokea wasibebane wala kufumbia macho .
"Suala
hili linashirikishwa na masuala ya ushirikina ,ila mimi nakataa
,msifuate waganga na kupotoshwa ,baba na mama kemeeni hili ,hakuna
utajiri unaokuja kwa kubaka kichanga,mtoto wako !!!hili linasababisha na
wale wenye maambukizi ya VVU kumpa mtoto Ukimwi asiye na hatia."
alisisitiza Mtupa.
Kwa
upande wake ,mgeni maalum mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini Silvestry
Koka alisema ,ameshiriki kuandaa baraza la eid ikiwa ni kawaida yake
kila mwaka .
Alisema ataendelea kushirikiana na dini zote kutatua shughuli mbalimbali bila kujali itikadi za kidini .
Koka
pia ,aliwaomba wananchi kuendelea kufuata taratibu za kiafya kwa kunawa
mikono, kuepuka mikusanyiko ili kujihadhari la gonjwa la corona.
Awali mjumbe wa baraza la masheikh Pwani,Athuman Mtasha alisema amani iendelee kudumishwa .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...