Na Woinde Shizza, ARUSHA
Kati ya Mikoa kumi ya Tanzania bara iliyofanyiwa Utafiti na chama Cha wafanyabiashara Nchini (TCCIA), Mkoa wa Songwe umebainika kuongoza kwa wafanyabiashara kufunga biashara zao kutokana na matatizo mbalimbali ikiwemo utitiri wa Kodi.Utafiti
huo umefanywa kwa miaka miwili kupitia Mradi wa kuboresha mazingira
rafiki ya kibiashara Tanzania(Building Bridges) unaotekelezwa kwa ubia
na shirika la Trias na TCCIA, chini ya ufadhili wa jumuiya ya Ulaya
(EU).
Akiongea na vyombo
vya habari mratibu wa Mradi huo ,Nebart Mwapwele alisema lengo la Mradi
ni kujenga daraja Kati ya sekta binafsi na Umma ili kuboresha mazingira
ya biashara na wamefanya utafiti huo kwa kuwahoji wafanyabiashara
wapatao 3000 nchini mzima.
Alisema
wafanyabiashara waliohojiwa kupitia Mradi huo walidai kuwepo kwa
changamoto kubwa ambayo ni pamoja na ukadiriaji wa Kodi kubwa ,utitiri
wa Kodi katika biashara moja na ukosefu wa masoko jambo lililosababisha
baadhi yao kushindwa kuendelea na biashara.
"Baadhi
ya Wafanyabiashara waliohojiwa wamelalamikia utitiri wa Kodi katika
biashara ya aina moja ,ukadiriaji mkubwa wa Kodi kabla hata hawajaanza
biashara"alisema
Naye
afisa mtendaji wa TCCIA Elijah Simbeye kutoka Mkoa wa Songwe alisema
kuwa utafiti uliofanyika kuanzia January mwaka Jana katika Mikoa kumi
,Mkoa wa Songwe ndio unaongoza kwa wafanyabiashara kufunga biashara zao
kutokana na Mamlaka mbalimbali za serikali ikiwemo TRA kutokuwa rafiki
na wafanyabiashara hao.
"Baada
ya tafiti kufanyika kwa kuongea na wafanyabiashara katika Mikoa
kumi,Mkoa wa Songwe ambao natoka Mimi ndio unaongoza kwa wafanyabiashara
kufunga biashara"alisema
Aidha
alisema utafiti umeonyesha kuwa wafanyabiashara wengi hawaelewi
utendaji kazi wa mamlaka za serikali zinazohudumia wafanyabiashara
zikiwemo Osha,Latra,serikali za mtaa,TMDA ,Fire na zingine Jambo
linalosabahisha kuwepo kwa malalamiko.
Kwa
upande wake mwakilishi wa shirika la Trias, Beatrice Minde ambao ni
watekelezaji wa Mradi huo alisema wamefanikiwa kupitia kumbukumbu za
tafiti zilizokusanywa kwa wafanyabiashara 3000 waliohojiwa na kwamba
shirika hilo litayafikisha mapendekezo hayo ngazi ya serikali .
Alisema
kuwa tafiti hizo zimefanyika katika Mikoa 10 ambayo ni Mwanza,Dar es
Salaam ,Arusha,Mtwara ,Shanyanga , Dodoma,Kigoma,Songwe ,Mbeya na Mara.
Naye
mkurugenzi was TCCIA Mkoa wa Dodoma na Makamu wa Rais Biashara wa
TCCIA,Dkt Ezekiel Meshack walisema Matokeo ya tafiti yatarejeshwa kwa
Kila mamlaka husika za serikali ili kuona namna ya kuyafanyia kazi
matatizo yaliyoibiliwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...