Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bwana Nyakimura Muhoji
===== ======= ========== =======
Tume ya Utumishi wa Umma inatarajia kutoa mafunzo kwa Watumishi wa Kampuni ya Uendelezaji wa Kiwanja cha Ndege Kilimanjaro (KADCO) Mkoani Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jijini Dar es Salaam na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bwana Nyakimura Muhoji amesema kuwa mafunzo haya yameandaliwa na KADCO kwa lengo la kuwajengea uwezo Watumishi wa KADCO kuhusu Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma Sura 298 na Usimamizi wa Utendaji Kazi kupitia Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji kazi (OPRAS), kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo inayosimamia masuala ya Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma.
Mafunzo haya ya wiki mbili yatafanyika kuanzia siku ya Jumatatu tarehe 10 Mei, 2021 na yatafunguliwa Rasmi na Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Mheshimiwa George D. Yambesi kwa niaba ya Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Dkt. Steven J. Bwana na yatahitimishwa tarehe 24 Mei, 2021.
Bwana Muhoji amesema, Tume inatekeleza jukumu hili kwa mujibu wa Kifungu cha 10 (1) ( C) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298.
Imetolewa na:-
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
TUME YA UTUMISHI WA UMMA
DAR ES SALAAM
07 Mei, 2021
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...