Na Said Mwishehe, Michuzi TV
RAIS
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Samia Suluhu Hassan amezindua Kiwanda
cha Ushonaji cha Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam ambapo amsema
uzinduzi wa kiwanda hicho unakwenda sambamba na sera ya Tanzania ya
Viwanda huku akishuri majeshi mengine nayo kuanzisha miradi au viwanda
ambavyo vitakuwa na shughuli tofauti na ushonaji.
Akizungumza leo
Mei 18, 2021 , Rais Samia amesema hivi karibuni Bungeni wamepitisha
mpango wa maendeleo wa miaka mitatu kwa ajili ya kujenga uchumi shindani
na viwanda kwa ajili ya maendeleo ya watu, hivyo uzinduzi wa kiwanda
hicho unaendana kabisa na kauli mbiu hiyo inayounga mkono nguvu ile
sera ya Tanzania ya viwanda.
"Lakini pamoja na mradi huu
nimemsikia IGP kuna mlolongo wa viwanda kadhaa na miradi mingi ambayo
inapangwa kutekelezwa, nami naomba niwatie nguvu miradi hiyo itekelezwe
kwa nguvu zote. Nimejulishwa kwamba mradi huu umejengwa kwa kutumia
force account na kwa kiasi kikubwa kimeweza kupunguza gharama za ujenzi
wa kiwanda hiki.
"Gharama halisi ni kama kiwanda kama kingejengwa
na mkandarasi na Sh.bilioni 1.4 lakini gharama zilizotomika kwa kutumia
force account ni Sh.milioni 666.4 , ni hatua nzuri na hongereni sana
Jeshi la Polisi na ni imani yangu tutaendelea hata kwenye miradi
mingine kutumia njia hii ili kupata ufanisi kuweka miradi mingi bila
kupunguza sifa na ubora wa miradi na viwanda vinavyojengwa ,
"Mbali
na kutoa ajira , kiwanda hiki kitazalisha ajira kitakuwa kikitengeza
sare 125, 200 za askari na kitashona sare kampuni za majeshi mengine
pamoja na kampuni za ulinzi binfsi, na ili muweze kufanya kazi hiyo
lazima muoneshe mfano mzuri , wakati natembelea kiwanda nimeoneshwa sare
ambazo zimeanza kushonwa na kudaliziwa na kiwanda hiki.
"Ni sare
nzuri mnoo, hata mimi nimewekewa ya kwangu , sijui nitaivaa lini
lakini kuna siku nitaivaa, lakini nami niungane nawe. IGP, vikosi
vingine vya ulinzi vije kushona,"amesema Rais Samia na kuongeza kiwanda
hicho kikuzwe vizuri ili majeshi mengine yashone sare zao hapo na kwamba
kila.kikosi kiwe na shughuli yake.
Amefafanua vikosi vingine
navyo viwe na viwanda ambavyo shughuli zake hazifanywi na kiwanda
kingine, ili kila kikosi kiwe na shughuli yake inayofanyia kazi."Najua
Magereza kwa mfano wamejikita kwenye bidhaa za ngozi, hivyo ni vema
wakajikita katika bidhaa hizo za ngozi , pamoja na mambo mengine madogo
madogo ya kilimo wanayofanya.
"Hii sio tu itaokoa fedha za
serikali lakini itaongeza mapato kwa Jeshi la Polisi lakini la zaidi ni
kwamba kiwanda hiki kitasaidia kudhibiti au uingizwaji holela wa sare za
askari na hiyo kuimarisha usalama wa raia na mali zao.Sababu tunajua
kuna visare sare vinatembea huko na watu wanavaa kutishia watu na
kufanya mambo ambayo hayaeleweki.
"Nirudie tena kulipongeza
Jeshi la Polisi kwa kujenga kiwanda hiki, nafarijika kuona kwamba vyombo
vingne vya usalama kama nilivyosema JKT, JWTZ na vyombo vingine
wanaviwanda vyao lakini kama nilivyosema nguvu kubwa tuweke hapa na
wengine wa shughulike na mambo mengine , huu ndio muelekeo
tunaoutaka,"amesema Rais Samia.
Ameongeza vyombo vya ulinzi
vinayo nafasi kubwa ya kushiriki na kutoa mchango kwenye shughuli za
kiuchumi , ikiwemo ujenzi wa viwanda bila kudumaza kazi za msingi za
vyombo hivyo. " Nitumie fursa hii kuahidi kwamba Serikali itaendelea
kuweka mazingira bora kwa ajili ya ustawi wa sekta ya viwanda ikiwemo
kutoa vivutio mbalimbali vya kikodi na visivyo vya kikodi.
"Mbali
na kushiriki kwenye shughuli za uchumi , jeshi la polisi lina dhamana
kubwa ya kulinda usalama wa raia na mali zao, napenda kuchukua fursa hii
kuwapongeza askari wa jeshi la polisi kwa kazi kubwa na nzuri
wanayoifanya, sio siri kuwa hali ya usalama tuliyonayo sasa nchini
inasimamiwa kwa kiasi kikubwa na jeshi la polisi pamoja na majeshi
mengine"amesema.
Home
HABARI
IKULU
UJUMBE WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KWA VYOMBO VYA ULINZI WAKATI AKIZINDUA KIWANDA CHA USHONAJI CHA JESHI LA POLISI MKOANI DAR ES SALAAM
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...