Na Mwandishi wetu, Mirerani
WADAU
wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro
Mkoani Manyara, wamewapongeza wabunge kwa kukemea kitendo cha upekuzi wa
kuvuliwa nguo unavyofanyika kwenye lango la ukuta unaozunguka migodi ya
madini hayo.
Mkazi wa
Mirerani Obeid Sarakikya amesema wabunge wamewatetea wananchi ipasavyo
kwani siyo vizuri na pia ni uvunjifu wa haki za binadamu kuwavua nguo
watu wakati wa kuwapekua.
Sarakikya
amesema alimsikia mbunge wa jimbo la Simanjiro Christopher Ole Sendeka
akipiga kelele dhidi ya upekuzi huo kwani ni udhalilishaji mkubwa usio
na chembe ya utu wa kibinadamu.
"Mbunge
wa vijana Taifa Asia Halamga na Joseph Musukuma nao wamelia na wadau wa
madini juu ya upekuzi wa kuvuliwa nguo kwa wadau wa madini ya
Tanzanite, tunawashukuru sana," amesema.
Katibu
wa chama cha wachimbaji madini mkoani Manyara (Marema) Tawi la Mirerani
Rachel Njau amesema anamuomba Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atimize ahadi
aliyoitoa Bungeni kuwa watanunua mashine ya upekuzi kuliko kuwavua nguo
na kuwadhalilisha watu.
Njau
amesema kauli ya Waziri wa ulinzi Elias Kwandikwa inapaswa kukanushwa
kwani watu wanavuliwa nguo siku zote na siyo wakihisiwa wakiwa na madini
kama alivyosema Bungeni.
"Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Arusha Catherine Magige alielezea vizuri juu
ya udhalilishaji unaofanyika Mirerani unasababisha wananchi wengine
kutopanda mlimani kwa hofu ya kuvuliwa nguo, tunawapongeza wabunge wetu
kwa kutetea," amesema Njau.
Mdau
mwingine Mashaka Jororo amesema wananchi wanaichukia Serikali yao kwa
vitendo vya udhalilishaji unaofanyika Mirerani hivyo wanunue vifaa vya
upekuzi na siyo kuwavua nguo.
Jororo amesema kitendo cha kuwavua nguo wananchi kinapaswa kupigwa vita hivyo anawapongeza wabunge kwa kuwatetea Bungeni.
Mdau
mwingine Sokota Mbuya amesema wabunge wameonyesha kuwa wanajali maslahi
ya wananchi wao kwa kukemea kitendo cha askari kuwavua nguo wakati wa
upekuzi.
"Tunawapongeza
wabunge wote akiwemo Ole Sendeka, Musukuma, Asia na Magige ambao kwa
namna moja au nyingine wamekemea vikali kitendo hicho," amesema.
Waziri wa Madini Dotto Biteko akizungumza na wachimbaji
madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani, Wilayani Simanjiro Mkoani
Manyara, alipotembelea eneo hilo hivi karibuni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...