WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewasilisha bungeni hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha 2021/22 jumla ya Shilingi Bilioni 680.3.

Akiwasilisha bejeti hiyo Waziri Aweso ameeleza mafanikio yaliyopatikana kutokana na utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta ya maji katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021 kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha upatikanaji wa huduma za maji nchini kutoka asilimia 70.1 vijijini na 84 mijini mwaka 2019/20 hadi asilimia 72.3 vijijini na 86 mijini.

Mafanikio mengine ni kuongezeka kwa idadi ya maabara za ubora wa maji zenye ithibati kutoka moja ya Mwanza hadi kufikia saba, kuzinduliwa kwa miradi mikubwa ya maji ya Tabora – Igunga - Nzega pamoja na Isaka Kagongwa baada ya  utekelezaji kukamilika. Aidha kukamilika kwa utekelezaji wa kihistoria wa miradi 422 ya maji ambapo kati ya hiyo ya vijijini ni miradi 355 na mijini miradi 67.

Waziri Aweso amesema hivi sasa   kasi na ubora wa utekelezaji wa miradi ya maji imeongezeka  na  gharama za ujenzi zimepungua kutokana na kutumia utaratibu wa force account. 

Mafanikio mengine ni pamoja na kuanza kutoa huduma ya maji kwa miradi 85 iliyokuwa na changamoto baada ya kufanya mabadiliko makubwa katika utaratibu wa usimamizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...