Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa Kitila Mkumbo(kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Mauzo ya Nje(EPZA) John Mnali wakiteta jambo wakati wadau walipokutana kujadili masuala mbalimbali yanayohusu uwekezaji nchini.
Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa Kitila Mkumbo akizungumza wakati akifungua majadiliano yaliyohusu uhusiano baina ya maeneo maalum ya uwekezaji na uchumi wa ndani ambapo wadau mbalimbali wanaojihusisha na masuala ya uwekezaji wameshiriki.
Wadau wa uwekezaji, wafanyakazi wa Taasisi ya Uongozi pamoja na wafanyakazi wa EPZA wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa Kitila Mkumbo(hayupo pichani.)
Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa Kitila Mkumbo(katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Uongozi pamoja na wa Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Mauzo ya Nje(EPZA.)
Mmoja ya wadau akiwa makini kusoma kijarida cha EPZA wakati wa majadiliano hayo yakiendelea.
Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji Mku wa TPSF Godfrey Sembeye akiandika jambo wakati wa majadiliano hayo ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa Kitila Mkumbo(hayupo pichani.)
Mkurugenzi wa Uhamasishaji na Uwezeshaji wa Uwekezaji wa EPZA akitoa mada iliyohusu fursa zinatolewa na maeneo maalum ya uwekezaji na namna ambavyo Serikali za mitaa na biashara ndogo na za kati zinavyoweza kunufaika.









Matukio mbalimbali katika picha wakati wa majadiliano yaliyohusu uhusiano baina ya maeneo maalum ya uwekezaji na uchumi wa ndani.(PICHA ZOTE NA SAID MWISHEHE- MICHUZI TV.)

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

SERIKALI imesema imejipanga  kisera na kutoa huduma muhimu na sheria rafiki zinazokidhi na kuvutia wawekezaji wa nje na ndani ya nje ya nchi ili kuwezesha ukuaji wa biashara ndani ya bara la Afrika na nje ya nchi.

Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo wakati akizindua kongamano la uhusiano baina ya maeneo maalumu ya uwekezaji na uchumi wa ndani lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi Tanzania (Uongozi Institute,) pamoja na Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA,) na kuwakutanisha wawekezaji wa ndani na nje na kujadili namna ya kuunganisha maeneo muhimu ya uwekezaji na uchumi wa ndani pamoja na kuangalia namna ya kushirikisha wawekezaji wa ndani hasa wajasiriamali.

prof. Mkumbo amesema, katika kuhakikisha uchumi wa nchi unashindana kimataifa Serikali na taifa kwa ujumla linaendelea kujiunga na jumuiya mbalimbali za kikanda na kimataifa ili kushindana kimataifa kama ilivyoelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan juu ya msingi wa kuimarisha biashara ndani ya Afrika na nje ya mipaka kwa kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kukuza uchumi wa taifa.

''Serikali imejipanga kisera, huduma muhimu katika maeneo ya uwekezaji, skills muhimu katika elimu ili kwenda na matakwa ya soko kwa ujumla pamoja na sheria za kodi katika kuhakikisha uwepo wa uzalishaji wenye tija katika maeneo ya viwanda.'' Amesema.

Aidha amesema, Serikali imejipanga Katika ujenzi wa mitaa ya viwanda "Industrial parts" pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji katika maeneo ya uwekezaj ya Kurasini, Bagamoyo na Benjamin Mkapa mkoani Dar es Salaam.

Kwa upande wake kaimu mtendaji mkuu wa Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA,) John Mnali amesema mamlaka hiyo imekuwa ikitekeleza majukumu katika maeneo ya uwekezaji kwa niaba ya Serikali kwa kuhakikisha maeneo yote ya uwekezaji yanapata huduma muhimu hasa  miundombinu ya maji, umeme na barabara pamoja na kutoa leseni za uwekezaji kwa wawekezaji hao.

Amesema, wamekuwa wakishirikiana na Wizara ya viwanda na biashara pamoja na wadau wengine wa uwekezaji kwa kuhakikisha wanayafikia mafanikio kwa kiwango kikubwa na hadi sasa wamesajili kampuni zipatazo 176 zenye uwekezaji wa dola za kimarekani bilioni 2.5 na watanzania 58198 wamenufaika kwa kupata ajira za moja kwa moja hadi kufikia Machi, 2021.

Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi (Uongoz Institute,) kwa kushirikiana na EPZA liliwakutanisha wawakilishi wa Serikali za mitaa, wawakilishi wa biashara ndogondogo na kati, kampuni za uwekezaji, Taasisi za Fedha, Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...