Ø * Awasha umeme rasmi kwenye kitongoji cha Mtakuja, kijiji cha Kibumba
Na. Dorina G. Makaya - Chato
WAZIRI wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani, amewahimiza wananchi wenye nyumba ndogo isiyozidi
vyumba vitatu ambao kwa sasa hawana fedha za kutandaza nyaya kwenye nyumba zao
(Wiring) kutumia kifaa cha UMETA (Umeme Tayari) ili kuhakikisha wanapata huduma
muhimu ya umeme.
Dkt.
Kalemani aliyasema hayo tarehe 13 Juni, 2021 alipofanya ziara kukagua na kuwasha
umeme rasmi kwenye kitongoji cha Mtakuja, kijiji cha kibumba wilayani Chato.
Waziri
Kalemani alisema, anatambua uwepo wa wananchi ambao katika kipindi ambacho
mradi unatekelezwa wanakuwa hawana fedha ya kutandaza nyaya kwenye nyumba zao (Wiring)
lakini wanahitaji huduma hiyo muhimu hivyo ni muhimu wakatumia kifaa hicho cha
UMETA.
Alisema,
wananchi hao wanayo fursa ya kuunganishiwa umeme kwenye mfumo wa umeme wa nyaya
za kawaida mara watakapopata fedha na kukamilisha kutandaza nyaya kwenye nyumba
zao.
Waziri
Kalemani alikumbushia kuwa, UMETA ni kifaa kilichosanifiwa kitaalamu ambacho
hupachikwa ukutani na kina matoleo ya kuwasha taa tatu (bulb), runinga, radio
na pasi ya umeme na hivyo kukidhi mahitaji muhimu kwa nyumba ndogo isiyozidi
vyumba vitatu.
Aidha,
Waziri Kalemani aligawa vifaa 20 vya UMETA kwa wananchi wa kitongoji hicho ili kuhamasisha
kaya ambazo hazina uwezo wa kutandaza nyaya kwenye nyumba zao wakati wa mradi,
kutokosa fursa ya kupata huduma ya umeme.
Waziri
Kalemani pia aliwataka wanakitongoji cha Mtakuja pamoja na wananchi wote
nchini, kutunza nguzo za umeme na kutandaza nyaya za umeme kwa wale ambao bado
hawajaunganishiwa umeme ili waweze kupatiwa huduma hiyo muhimu.
Kuwashwa
rasmi kwa umeme katika kitongoji cha Mtakuja kulishuhudiwa na viongozi
mbalimbali wa Chama na Serikali wa Wilaya ya Chato.
Katika
ziara hiyo, Waziri Kalemani aliambatana na mwakilishi wa Kamishna wa Umeme na
Nishati Jadidifu, Mhandisi Edson Ngabo na wataalam kutoka TANESCO na REA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...