Na Mwandishi
Wetu
KATIBU Mkuu
wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Zena Mohamed Said amepongeza kazi kubwa na
nzuri inayofanywa na Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL)
katika sekta ya elimu nchini kwa kuwaunganisha wanafunzi wa Tanzania na vyuo
vikuu nje ya nchi.
Ametoa
pongezi hizo alipotembelea mabanda ya GEL yaliyopo katika Maonesho ya 16 ya
Vyuo Vikuu Tanzania yanayoendelea Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
ambapo vyuo vikuu mbalimbali vimeshiriki.
Aidha katika
maonyesho hayo GEL imefanikiwa kuleta vyuo vikuu 10 ambavyo ni washirika wake
nje ya nchi kwa ajili ya kuja kuelezea fani wanazotoa.Vyuo hivyo ni Chandigarh,
Lovely Professional University (LPU), CT, Maharish Makandeshwar, Pandeet Deendayal
Energy, Sharda, Rayat Bahra vya India na VN Karazan na Sum State vya Ukraine.
Katibu Mkuu
Kiongozi amesema "Ni kweli kutokana na uhaba wa fani mbalimbali wanafunzi
wa hapa nchini wanalazimika kwenda nje ya nchi kusoma elimu ya juu, hivyo kuwa
na kiunganishi kama GEL ni jambo la msingi katika kurahisisha upatikanaji wa
vyuo hivyo.
"Ni
kweli vyuo vyetu haviwezi kuchukua wanafunzi wote sasa nawapongeza nyinyi kwa
kazi hii ya kuwaunganisha wanafunzi wetu na vyuo vya nje na pia kwa wale ambao
wako tayari kushirikina na sisi,Serikali inawashukuru kwa mchango
wenu,"amesema.
Awali
Mkurugenzi wa GEL Abdulmalick Mollel amemueleza kuwa kampuni hiyo imekuwa
ikishirikiana na vyuo hivyo kuwapeleka wanafunzi wa Tanzania kwa kozi
mbalimbali ikiwemo mpango wa kubadilishana wanafunzi.
Ameongeza
wakati Mollel nchi mbalimbali duniani zina kozi nyingi sana za afya kwa
Tanzania bado hazijawa za kutosha, hivyo wanafunzi wanaotaka kozi hizo wamekuwa
wakiwaunganisha kwenda kusoma kwenye nchi hizo.
Amesema
wamezungumza na vyuo vingi vya nje ya nchi kuwa Tanzania kuna wanafunzi wengi na wamekubali kuwachukua kwa
gharama za hapa hapa ndani ."Wakati sisi tunajipanga kuongeza kozi za afya
hapa nchini."
Mollel
amesema baadhi ya vyuo vimeahidi kufungua matawi hapa nchini baada ya kuona
mahitaji makubwa ya kozi wanazofundisha ambazo wanafunzi wa Tanzania wamekuwa
wakizifuata kwenye mataifa yao.
Amesisitiza
baadhi ya vyuo hivyo vya nje vitaingia makubaliano na vyuo vya hapa nchini
kuhusu namna ya kufanyakazi pamoja katika utoaji wa elimu ya juu."Ujio wa
vyuo hivyo ni fursa kwa vyuo vya Tanzania kuangalia namna ya kushirikiana
kwenye kozi mbalimbali pamoja na kubadilishana wanafunzi wanaoendelea na masomo
ili kupeana uzoefu.
Amefafanua kuwa mwanafunzi anaweza kusoma miaka miwili India na kisha akaja kumalizia hapa nchini Tanzania"Na wa hapa anaweza kusoma mwaka mmoja na kisha akaenda kumalizia kwenye chuo cha nje, haya ni mambo ambayo vyuo vinapaswa kuangalia namna ya kushirikiana."
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...