Na Mwamvua Mwinyi,Kibiti                                            

Naibu Waziri wa Maji , Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amesema ,wakazi wa kijiji cha Mahege na Ruaruke wilayani Kibiti mkoani Pwani ,watarajie kuondokana na kero ya ukosefu wa maji safi na salama ,ambapo amewahakikishia kuwa kero hiyo inakwenda kubaki historia.
                                               
Aidha amewatoa hofu wakazi wa Mahege na kusema serikali inatarajia kupeleka milioni 100 mwezi ujao ,ili kuanza mradi wa ujenzi wa maji kijiji Cha Mahege,ambao utagharimu milioni 735.761.3 hadi kukamilika kwake.                                          
Aliyasema hayo ,wakati wa ziara yake  ya kikazi , wilayani Kibiti ambapo ametembelea kijiji Cha Mahege kuzungumza na wananchi na miradi ya maji Nyamisati, Ruaruke na mradi wa maji wa Miwaga.                     

Pia Mahundi ,alimwelekeza mkuu wa wilaya ya Kibiti Ahmed ,kusimamia kuondosha changamoto ya kuzungusha maji kwa dizeli mradi wa maji Miwaga ,na kumtaka ashughulikie tatizo hilo TANESCO ili uendeshaji ubadilike .

Mahundi alimtaka meneja wa wakala wa maji na usafi wa mazingira Vijijini (RUWASA )Kibiti,Pascal Kibanjulo ,kuangalia namna ya kuongeza vituo vya maji vitano huko Ruaruke ili kusogeza huduma ya upatikanaji wa maji kwa wakazi .

Alieleza ,serikali inatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya kutatua changamoto ya ukosefu wa maji mijini na vijijini ,hivyo wanaendelea kupeleka fedha katika miradi mbalimbali ikiwemo miradi viporo iliyofika hatua nzuri ya ujenzi kwa asilimia 70-90 .     
                               
Awali akiuliza swali, mkazi wa Mahege ,Jafari Ramadhan aliiomba serikali iwasaidie kutatua changamoto ya maji kwani wanataabika miaka mingi na huduma hiyo isogezwa maeneo ya shule.

"Imekuwa kama ahadi hewa ,tunataka kujua mradi unaanza lini na tutapata maji kuanzia lini ili wake na watoto wetu tupate kunufaika na maji safi kama ilivyo maeneo mengine"alisema Ramadhan.

Kwa upande wake ,meneja wa RUWASA Kibiti Kibanjulo alisema ,mradi wa Kijiji Cha Mahege utaanza agost-septemba na ujenzi wake utachukua miezi sita hadi mei 2022.

Alieleza ,kwasasa hakuna kupigana kalenda ,watapiga kambi agost mwishoni 2021 hadi ujenzi utakapokamilika na utanufaisha wanafunzi na walimu shule ya Mahege .

Kibanjulo alifafanua mradi wa Ruaruke ,ni ukarabati unagharimu milioni 62.406 .8 fedha zilizotumika milioni 45.757.2 utekelezaji umefikia asilimia 75.

Nae mkuu wa wilaya hiyo , Ahmed alisema hali ya upatikanaji wa maji Kibiti ,ni asilimia 69 vijijini na asilimia 65 mjini .

Alibainisha ,katika mwaka wa fedha 2021-2022 kupitia serikali kuu wakala wa maji , unaendelea na utekelezaji wa miradi mitatu ya maji Nyamisati milioni 239.264.5,mradi Miwaga milioni 351.726.6 na miradi mitatu ya malipo ya matokeo (PbR) ambayo ni mradi wa Ruaruke,Uponda na upanuzi wa mradi wa maji shule ya msingi Jaribu Mpakani.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...