Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango, leo Julai 24, 2021 amefanya ziara ya kustukiza katika stendi ya Mabasi ya Mangaka iliopo Wilaya ya Nanyumbu.
Makamu wa Rais amekasirishwa na uongozi wa Wilaya kufanya upotevu mkubwa wa fedha usiolingana na matokeo ya ujenzi wa mradi huo.Ujenzi wa majengo ya stendi hiyo umetumia shilingi bilioni 2.2 kiasi ambacho Makamu wa Rais amesema hakilingani na ujenzi huo.
Makamu wa Rais amemuagiza Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Dkt. Festo Dugange kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu Hamis Dambaya ili kupisha uchunguzi kutoka vyombo husika.
Amesema
viongozi hawana budi kusimamia fedha za serikali zinazopelekwa katika maeneo
yao ili kuwaletea maendeleo wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...