Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mh. Reuben Mfune akiwa katika na picha ya pamoja na Wajumbe wote waliohudhuria warsh aya uzinduzi ya mradi wa utafiti wa utafiti wa usimamizi endelevu wa madakio ya maji kupitia tathimini ya kuimarisha mtiririko wa maji kwa mazingira na utekelezaji wake katika kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi kutokana na athari za shughuli za kibinadamu , Tanzani(EFLOWS).
Sehemu ya Wajumbe waliohudhuria katika uzinduzi wa Warsha ya uzinduzi wa Mradi ulioratibiwa na NEMC na SUA wa utafiti wa usimamizi endelevu wa madakio ya maji kupitia tathimini ya kuimarisha mtiririko wa maji kwa mazingira na utekelezaji wake katika kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi kutokana na athari za shughuli za kibinadamu , Tanzani(EFLOWS). Uzinduzi huo umefanyika Wilayani Mbarali.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) ambaye ni Meneja wa Utafiti kutoka NEMC Bi. Rose Salema Mtui akisoma hotuba ya ukaribisho katika uzinduzi wa mradi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt Samwel Gwamaka.
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mh.Reuben Mfune ambaye ni Mgeni Rasmi, akiongea wakati wa uzinduzi wa Mradi ulioratibiwa na NEMC na SUA wa utafiti wa usimamizi endelevu wa madakio ya maji kupitia tathimini ya kuimarisha mtiririko wa maji kwa mazingira na utekelezaji wake katika kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi kutokana na athari za shughuli za kibinadamu , Tanzani(EFLOWS). Uzinduzi huo umefanyika Wilayani Mbarali.

NI jukumu la kila mdau kama vile serikali za Mitaa, wakulima, wafugaji, jumuia za watumiaji maji, watunzaji wa mazingira na taasisi binafsi kuhakikisha kwamba rasilimali maji zote zinalindwa kikamilifu kwa ajili ya uendelevu wa madakio ya maji na maisha kwa ujumla.   


Hayo  yamesemwa  na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mh.Reuben Mfune ambaye alikua Mgeni Rasmi wakati wa warsha ya  uzinduzi wa Mradi wa utafiti wa usimamizi endelevu wa madakio ya maji kupitia tathimini ya kuimarisha mtiririko wa maji kwa mazingira na utekelezaji wake katika kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi kutokana na athari za shughuli za kibinadamu , Tanzani(EFLOWS) . Uzinduzi huo umefanyika Rujewa-Wilayani Mbarali katika Mkoa wa Mbeya.


Vilevile Mheshimiwa Mfune,  ametoa  shukrani kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhifadhi wa Mazingira (UNEP) kwa ufadhili wa kifedha katika mradi huo, pia Sekretarieti ya Azimio la Nairobi (Nairobi Convection Secretariat) ambayo ni msimamizi wa utekelezaji. Pamoja  na Waratibu wa mradi huo kutoka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kujitoa kwao kutekeleza mradi huu ambao ni mojawapo ya miradi iliyopo katika nchi zilizo kwenye Mpango Mkakati wa nchi za Magharibi mwa Ukanda wa Bahari ya Hindi 

 

Aidha, amesema kuwa anafurahi  kuona kwamba masuala ya mazingira kama vile umwagiliaji, kilimo kandokando ya kingo za mito, ufugaji wa mifugo ndani ya kidakio cha mto Mbarali na Bonde la Rufiji pamoja na ongezeko la watu, vinasimamiwa kwa uhifadhi kamilifu wa eneo la Magharibi mwa Ukanda wa Bahari ya Hindi. Na muhimu zaidi kwa ajili ya mtiririko endelevu wa maji kuelekea Mradi wa kufua umeme wa Mwalimu Nyerere (Julius Nyerere Hydro Power Project  - JNHPP).

Naye Mkurugenzi Mkuu wa NEMC katika hotuba yake  ya ukaribisho kwa mgeni Rasmi iliyosomwa kwa niaba yake na Meneja wa Utafiti-NEMC Bi Rose Salema Mtui amesema kuwa  NEMC kwa kushirikiana na taasisi za kitaaluma/utafiti zimekuwa zikitengeneza miradi/programu  na kufanya tafiti na mojawapo ni kama mradi huo uliozinduliwa kwa lengo la kutatua matatizo mbalimbali ya kimazingira. 

“Kupitia mradi huu, utekelezaji wa mtiririko wa maji kwa mazingira (env. flow) ni muhimu sana kwa uendelevu wa ikolojia ya mto; na natumaini wadau wote na Serikali kwa ujumla watakuwa tayari kutoa ushirikiano mkubwa kuhakikisha malengo ya mradi huu yametimia” alisema.


Akiongea katika warsha hiyo ya Uzinduzi Mkurugenzi wa Shahada za Juu Uhawilishwaji wa teknolojia za Kitafiti kutoka Chuo Cha Sokoine SUA Profesa Ezron Karimuribo  amesema kuwa kuna uharibifu mkubwa wa vyanzo vya maji Nchini na umetokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu kama vile ukataji miti, uchomaji misitu, kilimo pembezoni mwa vyanzo vya maji, uchimbaji madini,ufuagji na uchepushaji wa maji. Hivyo basi katika mradi huo  ambao utafanyika katika wilaya ya Mbarali  na wilaya hiyo imechukuliwa kama kianzio tu.


Mradi huo utafiti wa usimamizi endelevu wa madakio ya maji kupitia tathimini ya kuimarisha mtiririko wa maji kwa mazingira na utekelezaji wake katika kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi kutokana na athari za shughuli za kibinadamu , Tanzani(EFLOWS unaratibiwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...