Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amewataka wananchi wa mkoa huo
kuzingatia maelekezo ya serikali kuhusu udhibiti wa ugonjwa wa UVIKO 19
kwa kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima ikiwemo kuwa tayari kuchanjwa
chanjo itakopoanza kutolewa kwenye vituo vya afya.
Ametoa
rai hiyo leo (27.07.2021) mjini Sumbawanga wakati akitoa tamko kuhusu
wananchi kijikinga na tahadhari ya ugonjwa wa UVIKO 19 kwenye kikao cha
Kamati ya Afya ya Msingi mkoa wa Rukwa ambapo ameagiza viongozi wa
wilaya na dini kutoa elimu ya kujikinga kwa wananchi kila wanapokutana .
"Wananchi
katika mkoa wa Rukwa nawasihi kuzingatia maelekezo ya serikali na
wataalam kuhusu kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19 ikiwemo kuwaelekeza
kujiandàa kupata chanjo kwa wale watakaokuwa tayari" alisema Mkirikiti.
Mkuu
huyo wa mkoa ameongeza kusema mkoa wake unaendelea na kazi ya
kuhamasisha wananchi kujikinga ambapo amewasihi viongozi wa dini na na
serikali kufikisha elimu juu ya umuhimu wa chanjo katika kukabiliana na
ugonjwa wa virusi vya Kororna.
Katika
hatua za kuhakikisha umma unakuwa na taarifa sahihi Mkirikiti
ameviomba vyombo vya habari mkoani Rukwa kutenga muda mchache kwa
wataalam wa afya ili waweze kufikisha elimu ya kukabiliana na UVIKO
ikiwa ni kampeni maalum ya nchi.
"
Naomba vyombo vya habari mkoa wa Rukwa tengeni muda wa kufikisha ujumbe
wa kudhibiti UVIKO 19 kwa kutoa dakika chache kila siku wataalam wa
afya kuelezea njia za kujikinga na tatizo hili ili elimu ifike kwa
wanachi wengi hatua itakayopunguza kasi ya maambukizo", alisema
Mkirikiti .
Mkikikiri
aliwaondoa hofu wananchi kuwa chanjo itakayotolewa ni salama kwani
serikali lengo lake ni kuwalinda watu wake kuhakikisha usalama wa maisha
yao unaekuwepo vizazi na vizazi.
Alibainisha
hayo na kuongeza kuwa " hakuna serikali inayoweza kuleta chanjo ya
kudhuru wananchi wake, hivyo hii itakayotolewa ni salama " alihitimisha
Mku huyo wa Mkoa wa Rukwa.
Kwa
upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu amesema
chanjo ya Jansen ( Johnson & Jonson) ambayo serikali imeleta
nchini ni salama kiafya na kuwa wananchi wasiwe na hofu.
Dkt.
Kasululu alisema mkoa wa Rukwa unaendelea kujipanga kutoa chanjo za
UVIKO 19 kwa makundi ya kipaumbele ikiwemo watumishi wa afya, watu wenye
umri mkubwa zaidi ya miaka 50 na wenye matatizo ya magonjwa ya moyo
,kisukari, kifua kikuu ambapo itatolewa kwa hiari na bila malipo.
Kuhusu
takwimu za maambukizi Dkt. Kasululu alisema tangu Januari 2021 jumla
ya watu 80 walipokelewa kwenye vituo vya afya mkoani Rukwa ambapo kati
yake 16 walibainika kuwa na UVIKO 19.
"
Hadi sasa tunao wagonjwa nane (8) kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Rukwa ambapo kati yao wagonjwa wanne (4) wapo kwenye uangalizi maaluum,"
alisisitiza Dkt. Kasululu.
Katika
kikao hicho Dkt. Kasululu amewaomba viongozi wa serikali na na wale wa
dini kuwaelekeza na kuwafundisha wananchi kwa kuwaambia ukweli kuwa
Kinga ni Bora Kuliko Tiba.
Akiongea
kwa kwa niaba ya viongozi wa dini Askofu wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Tanganyika Ambele Mwaipopo ,alisema
anaishukuru serikali kwa kutoa elimu juu ya usalama na umuhimu wa chanjo
ya UVIKO 19 ambapo amesema watakwenda kuifikisha kwa waumini na
wananchi.
"Tumepokea
elimu hii ya kudhibiti UVIKO -19 sasa tunakwenda kufundisha ukweli huo
kwa waumini wetu ili hofu iondoke juu ya chanjo itakayotolewa na
serikali" alisema Askofu Mwaipopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...