Walimu na Wanafunzi wa shule ya sekondari Soni day iliyopo Bumbuli Mkoani Tanga wamemshukuru Mbunge wao  January Makamba kwa kutimiza ahadi yake  ya vitanda 20 vyenye thamani ya mil.4.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi walisema 'hostel' ya shule yao iliungua mara mbili na tangu ikumbwe na kadhia hiyo walikumbana na changamoto ya ukosefu wa vitanda hivo kulazimika kulala chini kutokana na vitanda vilivyokuwepo kuungua wakati wajanga hapo shuleni kwao.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyefahamika kwajina la  Mashoo Mrema alisema kuwa msaada huo wa Mbunge umekuja wakati muafaka wakati wao wakiwa na uhitaji wa vitanda hivyo.

Mrema alisema kuwa pia vitanda hivyo vitawasaidia kuwapa nguvu ya kujisomea na kuondokana na mawazo na magonjwa ya kukohoa waliyokuwa wanayapata kutokana na kulala chini.

Ally Lwena ni Mkuu wa shule hiyoAlisema Kwanza anampa shukrani Mbunge wao kwa Kusikia Kilio hicho Cha vitandanda  vya wanafunzi wa kike katika shule hiyo.

Lwena alisema hatua hiyo itasaidia kupata wanafunzi wengi watakaokaa Hostel na hivyo kuwaongezea Muda Mwingi Wakujisomea hatimaye Kuongeza Ufaulu wa Shule Na Halmashauri kwa Ujumla.

Pia Mkuu huyo wa shule alieleza kuwa kutokana na kukosekana kwa vitanda Wanafunzi walikuwa wakipigwa na baridi kali iliyokuwa inatoka kwenye sakafu na kuwapata moja kwa moja wanafunzi Ilisababisha magonjwa kama vile kukohoa , kubanwa na mbavu na hata vichomi.

Kwa upande wake Mbunge Makamba alisema tangu ameingia madarakani amekuwa akisadiana na  wananchi wake kutatua changamoto mbalimbali pamoja na kutekeleza ahadi anazoahidi.

Makamba alisema wakati shule hiyo imekumbwa na kadhia ya janga la moto yeye kama Mbunge alitoa fedha zake mfukoni na fedha kutoka kwa marafiki zake waliweza kununu vitanda 100 na bati 200 nakwamba ahadi iliyokuwa imebaki ni hiyo ya vitanda ambayo inakamilika Sasa.

Hata hivyo alieleza kuwa lengo la kusaidia katika shule hiyo ni kutaka kuunga mkono  jitihada za kuinua kiwango Cha elimu na ufaulu   katika jimbo lake.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...