Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ni Moja ya Taasisi zinazoshiriki maonesho ya utalii yanayofanyika katika viwanja vya michezo vya Kisongo(UWC) Jijini Arusha kwa lengo la kutangaza vivutio vinavyosimamiwa na Mamlaka hiyo.

Mkuu wa kitengo cha habari na Mahusiano wa TAWA Bw.Twaha Twaibu Amesema maonesho hayo ya siku mbili yataleta tija kubwa Sana kwa mamlaka hiyo kwani,kutawapa fulsa ya kubadilishana uzoefu katika masuala ya Utalii pamoja na kujitangaza.

Moja ya vivutio vinavyosimamiwa na Mamlaka hiyo ni mapori ya Akiba ikiwemo pori Pande lilikopo Jijini Dar Es salaam pamoja Pori la Akiba la Rukwa ambalo lina kivituo kikubwa Cha maporomoko ya Maji ya ndido yanayowafanya watalii wengi kupenda kutembelea Pori Hilo.

Pia mamlaka hiyo inasimamia Maeneo ya Urithi wa Dunia ya KILWA KISIWANI na SONGO MNARA pamoja na pori la Akiba Maswa.Maonesho haya yameanza leo tarehe 17 hadi 18 Septemba,2021 huku TAWA ikiwakirishwan ujumbe kutoka makao makuu ya Taasisi hiyo ukiongozwa na Mkuu wa kitengo cha habari na Mahusiano Bw.Twaha Twaibu.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...