Akizungumza wakati wa
kuzindua bodi hiyo Waziri Aweso amesema ikifanya kazi kwa ufanisi itaweza
kuisimamia vyema menejimenti na kuwezesha kufikiwa malengo ya mamlaka hiyo hasa
kwa kutembelea miradi na kufuatilia utekelezaji wake ili lengo la
Serikali la kuwafikishia wananchi Maji safi na salama litimie.
“‘Nendeni mkasimamie
menejimenti, msiwe bodi ya vikao, DAWASA inafanya kazi nzuri nendeni mkahakikishe kazi
hiyo inaendelea na kuleta matokeo chanya zaidi ili iwe mfano wa kuigwa kwa
Mamlaka nyingine za maji,” amesema Aweso.
Pia Aweso aliwakumbusha
wakurugenzi wa mamlaka nyingine za Maji hapa nchi kuiga mfano wa DAWASA na
kufanikisha lengo la kumtua mama ndoo kichwani na kuwasisitiza waje kujifunza
kupitia utendaji kazi wa Mamlaka hiyo iliwaweze kufikia malengo waliyojiwekea.
“Kazi kubwa inafanyika na
tunaiona sio vibaya kwa mamlaka nyingine kuja kujifunza hapa na Dawasa isiridhike
izidi kufikisha maeneo ya pembezoni,”. Alisema Aweso
Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja amemshukuru Waziri wa Maji Jumaa Aweso
kwa kuchagua Bodi nzuri mara baada ya Bodi iliyokuwepo kumaliza muda wake
iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake Jenerali mstaafu Davis Mwamunyange.
Amesema kazi iliyofanyika
DAWASA kwa miaka mitatu ni kubwa sana chini ya Bodi iliyomaliza muda wake
ikiwemo ya kuunganisha DAWASA na DAWASCO.
Amesema kwa kipindi kifupi
sana DAWASA waliweza kupanua huduma zake ambapo mpaka sasa inahudumia takribani
wananchi wapatao milioni tisa kutoka
mkoa wa Dar Es Salaam, Wilaya ya Bagamoyo, Mkuranga, Kihaba na Sehemu ndogo ya
Tanga pamoja na sehemu ndogo ya Morogoro.
“Kupitia bodi hiyo
iliyomaliza Muda wake DAWASA wameweza kuyakabiri maeneo sugu ambayo ni Segerea,
Kinyerezi, Kipawa, Ukonga, Goba, Mvumuni, Salasala, Madale, Kwamsuguli pamoja
Gongo la Mboto”. Alisema Luhemeja
Akizungumza kwa niaba ya
bodi hiyo Mwenyekiti Jenerali mstaafu
Davis Mwamunyange amesema watakahakikisha miradi yote inatekelezwa chini ya
mamlaka hiyo na watahakikisha wanatembelea miradi yote na kuisimamia DAWASA ili
kuweza kufikia lengo la kumtua mama ndoo kichwani.
Pia Waziri wa Maji Jumaa Aweso alitembelea na
kujionea uendeshaji wa Kituo cha TEHAMA cha kukusanya Taarifa za Mamlaka hiyo kabla ya kuzindua Bodi mpya
ya DAWASA itakayodumu kwa Miaka mitatu.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akitolea ufafanuzi kwa Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos
Makalla,Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira
Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA), Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange
pamoja na viongozi mbalimbali kuhusu uendeshaji wa Kituo cha TEHAMA cha
kukusanya Taarifa za Mamlaka hiyo wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Bodi
mpya ya DAWASA
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma
wakizindua Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa
Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) leo jijini Dar Es Salaam.
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) akikabidhi vitendea kazi Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira
Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA), Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange mara
baada ya kuzindua Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini
Dar es Salaam
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) akikabidhi vitendea kazi Katibu na Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam
(DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja mara
baada ya kuzindua Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini
Dar es Salaam
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) akikabidhi vitendea kazi kwa baadhi ya
wajumbe wa Bodi ya DAWASA mara baada ya kuzindua Bodi ya Wakurugenzi wa
DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso akizungumza na Wajumbe wa Bodi wapya na
wafanyakazi wa DAWASA pamoja na wageni waalikwa waliofika kwenye
uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya DAWASA pamoja na kuwapatia vitendea
kazi kwa kila mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga akizungumzia
namna Serikali ilivyojipanga kusimamia mamlaka za Maji kuweza kutekeleza
Miradi mikubwa pamoja na midogo ya maji wakati wa uzinduzi wa Bodi ya
Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa ufafanuzi kuhusu Bodi
iliyomaliza muda wake ilivyofanya kazi kwa miaka mitatu chini ya
Wenyekiti wake Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange wakati wa uzinduzi wa
Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt.
Christine Ishengoma akizungumza namana walivyojipanga kuweza kuzisimamia
Mamlaka za Maji hapa nchini ikiwemo Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) ili kuweza kufanikisha
upatikanaji wa Maji kwa wananchi wakati wa uzinduzi wa Bodi ya
Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti
wa CCM mkoa wa Dar es Salaam na Mjumbe Mpya wa Bodi ya DAWASA, Kate
Kamba akizungumza kuhusu namna Ilani ya Chama cha CCM inavyotaka
wananchi
wapatiwe maji safi na salama pamoja na kumshukuru Waziri wa Maji, Jumaa
Aweso kwa kumteua kuwa mjumbe wa Bodi mpya ya Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) leo jijini Dar es Salaam Baadhi
ya Wajumbe wa Bodi, wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa
Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)na wagei waalikwa wakifuatilia hotuba ya
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi
wa DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akimtambulisha Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange
anayeendelea tena kwa miaka mitatu mingine leo wakati wa kuzindua Bodi
ya Wakurugenzi wa DAWASA leo jijini Dar es Salaam. Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla akizungumza na waandishi wa
habari kuhusu namna alivyofurahishwa na utendaji wa DAWASA mara baada ya
kutembelea na kupata maelezo ya Kituo cha TEHAMA cha kukusanya Taarifa
za Mamlaka. Wa kwanza kulia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso na wa pili
kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa
Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja. Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira
Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA), Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange
akizungumza jambo mara baada ya Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA
kuzinduliwa na Waziri wa Maji Jumaa Aweso itakayodumu kwa miaka mitatu.
Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi
Anthony Sanga , Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA Jeneral
Mstaafu Davis Mwamunyange, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Baadhi ya wajumbe wa Bodi hiyo mara
baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Maji. Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi
Anthony Sanga , Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA Jeneral
Mstaafu Davis Mwamunyange, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na wakuu wa wilaya ya Kisarawe na Bagamoyo mara
baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Maji.
Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi
Anthony Sanga , Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA Jeneral
Mstaafu Davis Mwamunyange, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa DAWASA
baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Maji. Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi
Anthony Sanga , Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA Jeneral
Mstaafu Davis Mwamunyange, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Mamlaka za maji za mikoa mingine mara
baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Maji. Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi
Anthony Sanga , Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA Jeneral
Mstaafu Davis Mwamunyange, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Mamlaka nyingine pamoja na mashirika mara
baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Maji. Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi
Anthony Sanga , Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA Jeneral
Mstaafu Davis Mwamunyange, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja wa mikoa ya DAWASA mara
baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...