Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamtafuta mwanamke ambaye bado hajafahamika kwa kosa la kutupa mtoto mchanga jinsi ya kike anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya siku tatu ambaye alikutwa amefariki dunia baada ya kutupwa ndani ya shimo la choo.

Tukio hilo limetokea mnamo Oktoba 20, 2021 majira ya saa 09:00 asubuhi huko Mtaa wa Makaburini uliopo Kata ya Kiwira, Tarafa ya Ukukwe katika Halmashauri ya Tukuyu. Mwili wa kachanga ulikutwa ndani ya shimo la choo kilichopo nyumbani kwa SALOME LUTENGANO [36] Mkazi wa Mtaa wa Makaburini na ndipo jitihada za kuutoa zilianza lakini tayari alikuwa amefariki dunia.

Jeshi la Polisi Mkoani hapa linalaani kitendo hicho cha mauaji ya mtoto asiyekuwa na hatia yoyote na linaendelea na msako dhidi ya mtuhumiwa wa tukio hili na mara baada ya kumkamata litamfikisha mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.


MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TATU AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKA CHOONI.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu FRANCIS MWAKAJOKA [16] wa shule ya sekondari Wigamba iliyopo Jijini Mbeya amefariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa matibabu baada ya kuanguka kwenye Koldo la choo shuleni hapo.

Tukio hilo limetokea Oktoba 20, 2021 majira ya saa 07:45 asubuhi huko Shule ya sekondari Wigamba iliyopo Jijini Mbeya. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kitabibu. Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa marehemu alikuwa na matatizo kwenye mapafu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...