Na Mwandishi Wetu,Geita
MPANGO
wa kutoa mafunzo ya elimu ya usalama barabarani kwa lengo la kupunguza
ajali zinazotokea mara kwa mara nchini umewafikia wanafunzi 110,000
kutoka katika shule za msingi zaidi ya 100 katika mikoa ya Dar es Salaam
, Geita,Ruvuma, Dodoma na Visiwani Zanzibar.
Mbali na kupata
mafunzo ya usalama barabarani wanafunzi wamekuwa wakishindanishwa
kuchoro michoro inayotoa ujumbe unaolenga kuelezea usalama baarabarani
na kisha washindi kujinyakulia fedha ambazo zinatolewa na Kamuni ya Puma
ambayo ndio anayetoa elimu hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Amend.
Akizungumza
leo Oktoba 20,2021 wakati wa utoaji wa zawadi kwa wanafunzi walioshinda
katika uchoraji wa michoro ya usalama barabarani kutoka Shule tano za
msingi mkoani Geita, Ofisa Usalama ba Mazingira wa Kampuni ya Puma
Ambokege Minga ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo
amesema wanatambua umuhimu wa mafunzo hayo kwa wanafunzi.
Akifafanua
zaidi amesema Puma Energy Tanzania Ltd imetoa zawadi kwa wanafunzi wa
shule za msingi walioshinda shindano la michororo ya usalama barabarani
kwa mwaka 2020-2021 mkoani Geita na kwamba tukio hilo la utoaji zawadi
linahitismisha mradi huo kwa kipindi cha mwaka huu uliofanywa Kampuni
ya Puma kwa ushirikiano na Shirika lisilo la kiserikali la AMEND.
"Mpango
huu kaika Mkoa wa Geita ulihusisha mafunzo kuhusu usalama barabarani
katika shule tano na wanafunzi wasiopungua12,000 wamefikiwa pamoja na
shindano la uchoraji wa michoro inayo hamasisha usalama barabarani.
Katika
utoaji huo uliohudhuriwa pia na maofisa wa ngazi mbalimbali wa Jeshi la
Polisi ,Kikosi cha Usalama Barabarani, Mwakilishi huyo wa Kampuni ya
Puma amesema wameamua kuja Geita kwa sababu ya ukuaji wa haraka wa mji
huo ambapo shughuli za kijamii na ongezeko la watu na magari ambayo
yanahatarisha usalama wa watoto wanapokwenda shule na kurudi nyumbani.
"Mpaka
sasa tumeweza kufundisha jumla wanafunzi zaidi ya12,000.. wa shule za
msingi katika shule 5 (Tano) za mji wa Geita na hii ikiwa ni mara ya
pili kuendesha mafunzo haya mkoani Geita.Mafunzo haya ya usalama
barabarani na uchoraji ni kipaumbele chetu kwa lengo la kuwapa uelewa
watoto hususani wa shule za msingi juu ya namna bora ya matumizi ya
barabara.
"Lengo kubwa la mpango huu ni kuwafanya watoto hawa
kuwa na uelewa wa matumizi ya barabara wakiwa bado wadogo. Tunaamini kwa
kufanya hivyo tunawaongezea uelewa kuhusu dhima nzima ya usalama
barabarani kwa waTanzania wengi Zaidi. Mpango huu pia kwa mwaka huu
unategemea kufanyika katika mikoa ya Dar es salaam, Dodoma na visiwani
Zanzibar.
"Jumla ya shule 20 zimefikiwa kwa mpango huu kwa mwaka
2021. “Lengo letu kama kampuni ni kuongeza wigo ili kufikia shule
nyingi Zaidi nchi nzima. Mkurugenzi wakampuni ya Puma kupitia
mwakilishi wake ameahidi pia kuwa Puma Energy itaendelea kuwekeza katika
kampeni ya usalama barabarani ikishirikiana na serikali kupitia jeshi
la Polisi ili kuokoa maisha ya watanzania,"amesema..
Kwa upande
wake Mkaguzi Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya
Geita Emmanuel shagaya amewaomba wanafunzi waliopata mafunzo hayo
wameombwa kufikisha ujumbe unaohusu usalama barabarani.
"Watoto
mkifika nyumbani waiteni wazazi wote wawili kisha kaeni chini na baada
ya hapo waambieni baba na mama wazingatie usalama wao wawapo barabarani
pamoja na kuzingatia usalama wa wengine, tukifanya hivyo tutakuwa salama
na tutapunguza ajali za barabarani zitapungua na kuokoa Taifa.
Amesisitiza
elimu ya mafunzo ya usalama barabarani ni muhimu kwani kuwepo kwa
shughuli nyingi za kijamii zimechangia ongezeko la ajali,lakini kupitia
elimu hiyo ni matumaini yao zitapungua.
Kwa upande wake Diwani wa
Kata ya Kalangalala wilayani Geita Prudence Temba amesisitiza umuhimu
wa jamii kuzingatia matumizi sahihi ya barabarani huku akiwaomba
wanafunzi kufikisha elimu hiyo kwa wazazi au walezi.
Pia amesema
kuna wanafunzi ambao wamekuwa wakipanda bodaboda,hivyo wasikubali
kupanda bodaboda bila kuvaa kofia ngumu, amewasisitiza wanafunzi hao
wahakikishie wanapopakiwa katika magari na wazazi wao kama hawajafunga
mikanda,basi waambie wavae na kuwakumbusha ulazima wa kufuata sheria za
barabarani.
"Katika eneo letu la Kalangalala kuna muingiliano
mkubwa wa watu, hivyo tunaomba mtusaidie kupaka rangi katika maeneo ya
wavuka kwa miguu, alama zimefutika na kusabababisha kutoonekana
vizuri.Pia tunatoa ombi kwa Kampuni ya Puma itusaidie kutejengea ukuta
wa shule ya Msingi Kalangalala, matofali yapo, hivyo mtusaidie michanga
na mambo mengine, wala hatutaki fedha,"amesema.
Mgeni rasmi
kutoka Ofisi ya Ofisa Elimu Mkoa wa Geita amesema Masumbuko Magang'bila
amewasukuru Puma kwa kupeleka mafunzo hayo lakini ni vema wakaendelea
kutoa elimu hiyo muhimu yenye lengo la kuokoa maisha ya watu."Tunapotoa
mafunzo kwa wanafunzi maana yake tunakwenda kupeleka elimu hiyo ngazi
ya chini kabisa, wanafunzi ambao tunawaona shuleni wana wazazi na walezi
wao ndio sisi."
Pia amesema wamefurahishwa na shindano la
michoro kutoa elimu ya usalama barabarani na kubwa zaidi zawadi ya
Sh.milioni nne ambayo shule itakayotoa mshindi wa kwanza itatoa hamasa
kwa shule kuwa mabalozi wazuri, lakini kwa mwanafunzi atakayeshinda na
kushika nafasi ya kwanza kwa uchoraji sh.500,000 itakwenda kuongeza
hamasa kwa wanafunzi katika kuchora lakini kuwa balozi wa usalama
barabarani yeye na wazazi wake.
Mwalimu wa Shule ya Msingi
Nguzo Mbili amesema siri ya ushindi wa shindano hilo ni kujamini
,kujituma na kuwapa wanafunzi kutambua namna ya kutumia vipaji vyao na
hatimaye wameibuka kidedea na kushinda Sh.Milioni Nne wakati mshindi wa
kwanza kutoka shule hiyo ameibuka mshindi kwa kuchukua nafasi ya kwanza
na kushinda Sh.500,000.
Mshindi wa kwanza wa mashindano ya
kuchora mchoro wa usalama barabarani ni Victoria Michael wa Shule ya
Msingi Nguzo mbili,mshindi wa pili ni Zabibu Stanford Shule ya msingi
Nyankumbu aliyepata Sh.300,000 na mshindi wa tatu ni Paul Haruna wa
shule ya Msingi Nguzo Mbili aliyepata Sh.150,000.
Ofisa
Elimu Mkoa wa Geita Masumbuko Magang'bila( wa pili kushoto) akiwa na
viongozi kutoka kampuni ya Mafuta ya Puma Ambokege Minga, Shirika la
Amend na Mkaguzi wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya
ya Geita Emmanuel Shagaya( kulia) wakiwa makini kutafuta mchoro ambao
utatoa mshindi katika shindano la kuchora mchoro wa usalama barabarani
.Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania
kupitia mpango wake wa kutoa elimu ya usalama barabarani.Shule za msingi
tano za Geita zimenufaika na mpango huo
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nguzo mbili wakiwa na mwalimu wao Tunu Mjema( kulia) wakishangalia baada ya shule yao kuibuka mshindi wa jumla katika shindano la kuchora mchoro wa usalama barabarani ambalo limeandaliwa na Kampuni ya mafuta ya Puma .Shule tano za msingi mkoani Geita zimeshiriki shindano hilo pamoja na kunuifaika na mafunzo ya usalama barabarani.
Ofisa
Elimu Mkoa wa Geita Masumbuko Magang'bila akifafanua jambo wakati wa
utoaji huo wa zawadi kwa wanafunzi walioshinda michoro ya usalama
barabaraniDiwani wa Kata ya Kalangalala wilani Geita Prudence Temba
akitoa ombi kwa Kampuni ya Puma kusaidia kujenga ukuta wa uzio wa shule
ya Msingi Kalangalala
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Kalangalala wilayani Geita wakiwa makini kufuatilia majina ya wanafunzi walioshiriki kuchora michoro ya usalama barabarani .Shindano hilo limeandaliwa na kampuni ya Puma kupitia programu ya kutoa mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi
Ofisa Usalama na Mazingira wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Ambokege Minga ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo akielezea jambo wakati wa tukio la utoaji zawadi kwa washindi wa michoro ya usalama barabarani
Wawakilishi wa wanafunzi walioibuka kidedea katika shindano la kuchora michoro ya usalama barabarani wakipokea zawadi ya fedha kutoka Kampuni ya Mafuta ya Puma ambayo imekuwa ikiandaa mafunzo ya elimu ya usalama barabarani kwa kushirikiana na Shirika la Amend
Wanafunzi ambao wameingia 10 bora katika shindano la uchoraji michoro ya usalama barabarani( waliosimama nyuma) wakiwa katika picha na viongozi kutoka taasisi na mashirika mbalimbali walioshuhudia utolewaji wa zawadi kwa washindi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...