Na Khadija Kalili, Kibaha
JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani linawashikilia watu wawili jamii ya wafugaji kwa tuhuma za kumpigia na kumjeruhi Mwenyekiti wa Chama Cha Umwagiliaji Mpunga (CHAURU), Ruvu Mkoani Pwani aliyetajwa kwa jina la Sadaka Chacha.
Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ACP Nyigesa Wankyo kuwa Oktoba 25 saa tisa alasiri katika mashamba yanayomilikiwa na Chama Cha Umwagiliaji Ruvu (CHAURU) watuhumiwa hao wakiwa na wenzao watatu jumla walikua watano walilazimisha kuingiza mifugo Yao kwenye mabwawa ya kilimo cha Umwagiliaji Ili mifugo yao inywe maji.
RPC Wankyo aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Petro Ngilangu (25)na Robert Kambai (28) wote wakiwa ni wakazi wa Kijiji Cha Kidogozelo Kata ya Vigwaza.
Wafugaji hao walimshambulia Mwenyekit huyo wa CHAURU Chacha kwa kumpiga na kumjeruhi kichwani.
Tukio la kupigwa lilitokana baada ya Mwenyekiti huyo akijaribu kuzuia mifugo kuingia ndani ya mashamba hayo, ambapo Sadala akiambatana na Daniel Mwita Ofisa pamoja na askari Mgambo walielekea eneo hilo.
Walipofika mashambani Askari Mgambo walipoona wamezidiwa walitimua mbio na kuwaacha wenzao ndipo wakawavamia Chacha na Mwita wakawashambulia kwa kutumia fimbo na vitu vyenye ncha kali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...