Na Ahmed Sagaff – MAELEZO

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka watendaji wa Serikali kuweka utaratibu wa kufuatilia kero zinazowakabili wawekezaji na kuzitatua.

Mhe. Rais ametoa agizo hilo leo alipokuwa katika ziara ya kikazi katika Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha.“Tunavuta wawekezaji wanakuja lakini wakifika na wakishajenga viwanda, tusiwaache wenyewe, tufuatiliena tujue kero zinazowakabili na tuzitatue,” ameagiza Rais Samia.

Tangu alipoingia madarakani Machi 19, 2021 Rais Samia amekuwa akichukuwa jitihada mbalimbali za kuwavutia wawekezaji na kuhakikisha wale waliopo wanaendesha shughuli zao kwa kufuata sheria bila kubughudhiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...