Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV
KLABU ya Simba rasmi imetangaza kuachana na aliyekuwa Kocha Mkuu, Didier Gomes Da Rosa baada ya kuridhia ombi lake kuanzia leo Oktoba 26, 2021. Simba SC imeachana na Gomes Da Rosa sambamba na baadhi ya watu wake katika Benchi la Ufundi, akiwemo Kocha wa Makipa, Milton Nienov na Kocha wa Viungo, Adel Zrane.
Taarifa iliyotolewa na Menejimenti ya Klabu hiyo imeeleza kuwa hatua hiyo ya kuachana na Kocha Mkuu imekuja baada ya majadiliano ya kina ya pande zote kuafikiana kwa mujibu wa mkataba na manufaa kwa wote.
Pia imeeleza kuwa Kocha Msaidizi Thierry Hitimana atakuwa Kocha Mkuu katika kipindi cha mpito akisaidiwa na Kocha Msaidizi Suleiman Matola.
Klabu hiyo imewashukuru Kocha Gomes na wenzake katika kipindi chote cha mafanikio walichotumikia Simba SC pamoja na kuwatakia kheri waendako.
noce
ReplyDelete