Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili 1. LIPANDE SAID @ SIMWICHE [62] na 2. JUMA PIUS [32] wote wakazi wa Kapyo wilayani Mbarali mkoani Mbeya kwa tuhuma za kupatikana na nyara za serikali vipande saba [07] vya Meno ya Tembo.

Watuhumiwa walikamatwa tarehe Oktoba 20, 2021 majira ya saa 10:00 asubuhi huko Kijiji cha Kapyo kilichopo Kata ya Igurusi, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali baada ya Jeshi la Polisi mkoani hapa kupata taarifa za siri na kisha kufanya msako na upekuzi nyumbani kwa mtuhumiwa LIPANDE SAID @ SIMWICHE na kufanikiwa kukuta nyara hizo zikiwa zimefichwa kwenye mfuko wa sandarusi.

Aidha katika upekuzi huo, watuhumiwa walikutwa wakiwa na nyara nyingine za serikali ambazo ni kipande cha Ngozi ya Fisi Maji nacho kikiwa kimefichwa kwenye mfuko wa sandarusi.

Vipande hivyo saba vya Meno ya Tembo vina uzito wa kilogramu 33 na thamani ya Tshs. Milioni Sitini na tisa laki mbili kumi na nne elfu mia nne na kumi [Tshs.69,214,410/=] huku ikikadiriwa kuwa Tembo waliouawa ni wawili.

Upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani kwa kosa la kupatikana na nyara za serikali kinyume cha sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009 kifungu namba 86 na kosa la uhujumu uchumi kinyume cha sheria ya uhujumu uchumi ya mwaka 2019 kifungu namba 57 (First Schedule).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...