Na Said Mwishehe, Michuzi TV

TAASISI ya Teknolojia Dar es Salaam(DIT) imeweka wazi mikakati mbalimbali iliyowekwa kuutekeleza mradi wa RAFIC utaokwenda kuwezesha Watanzania wengi zaidi bila kujali viwango vyao vya elimu kupatiwa mafunzo ya kuwa na uelewa kuhusu masuala ya TEHAMA yakiwemo ya kutumia mitandao ya simu za mkononi.

Kupitia mradi huo wa RAFIC ,DIT imepatiwa Dola za Marekani milioni 16.25 ambazo ni sawa na Sh.bilioni 37 ili kuutekeleza mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano.DIT imeamua kutumia mradi huo kujikita katika utoaji elimu na ujuzi katika TEHAMA na lengo lao ni kuwa wabobezi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla na uwezo huo wanao kwani wanaowakufunzi wabobezi katika mambo ya TEHAMA.

Wakizungumza wakati wa semina maalumu iliyoandaliwa DIT kwa waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari , Waratibu wa mradi huo wa RAFIC Dk.Joseph Matiko na Daud Mbomba wakiongozwa na Mkuu wa DIT Profesa Preksedis Marco wamefafanua kwa kina kuhusu mradi huo ambao mchakato wake upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na unakwenda vizuri.

Akifafafanua kuhusu mradi wa RAFIC, Profesa Marco amesema kuwa mchakato wa mradi huo ulianza mwaka 2019 lakini fedha za kuanza utekelezaji zilitolewa mwaka 2020, na DIT wao wamechukua eneo la eneo la TEHAMA na kiasi cha fedha Sh.milioni 37(dola milioni 16.25) zitatumika kwa muda wote wa utekelezaji ambao ni wa miaka mitano.

"Thamani ya mradi ni dola za Marekani milioni 75 na fedha hizo ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na unalenga kusaidia zetu katika kuendeleza kutoa ujuzi kwa watanzania.Mbali ya sisi DIT kupata hizi fedha , pia kuna taasisi nyingine tatu nazo zimepatiwa kiasi sawa ambacho DIT tumapata cha dola za Marekani milioni 16.25(sawa na Sh.bilioni 37),"amesisitiza.

Awali akielezea mradi huo, Mratibu wa RAFIC Dk.Matiko amesema taasisi hiyo imekuwa na mipango mikubwa ya kuhakikisha wanakuwa wa kimataifa na huko ndiko ambako wamekwenda na kwamba wameweka mipango ya miaka 100 lakini kikubwa ambacho kinaleta furaha ni kuona kasi waliyonayo katika kukimbia ili kutatua changamoto zinazoikabili jamii."Kwa sasa kupitia mradi wa RAFIC hapa DIT tumamua kujikita katika TEHAMA,tunacho kituo cha umahiri wa TEHAMA ambacho kinaitwa RAFIC.

"Pamoja na mambo mengine kwetu hapa DIT mojawapo la eneo la kimkakati tunataka kuwa watalaam wa Cyber Crim(uhalifu mtandaoni) tunajua Serikali imehamia katika mifumo ya kidigijitali , ukusanyaji wa mapato unafanyika mtandaoni, DIT tunataka kuwa na askari ambao watapambana kuulinda mfumo wa kidigitali na tuko tayari kwa hilo.

"Kwa hiyo tutahudumia hapa nchini na Afrika Mashariki, kwa hiyo tunaendelea na huo mradi wa RAFIC pamoja na miradi mingine mingi. Nisisitize mradi wa RAFIC unalenga kuendeleza ujuzi, kwa malengo ya mradi kikanda lengo la kwanza ni kuongeza udahili, tuwe tunadahili wanafunzi wengi na lengo la pili hao wanaofundishwa waweze kujiajiri.

"Wakati lengo la tatu  wanafunzi wetu waweze kufanya kazi hata katika nchi nyingine, mradi huu wa RAFIC unafadhiliwa na Benki ya Dunia, ni mradi wa kikanda, na nchi tatu zinashiriki,nchi hizo ni Ethiopia, Kenya na Tanzania.Kwa Ethiopia unatekelezwa katika vituo saba, Kenya vitano na kwetu unatekelezwa katika vituo vinne,"amesema Dk.Matiko.

Aidha amesma kuna maeneo ya kimkakati ambayo Serikali imeona iwekeze, hivyo hata mradi huo umeangalia maeneo ya mkakati, mradi huo unatekelezwa Chuo cha Ufundi Arusha ambapo wao wamejikita katika nishati na chuo hicho kimepewa Dola za Marekani milioni 16.25(Sh.bilioni 37.

Wakati Kampasi ya Mwanza itajikita katika uchakati wa ngozi na imepewa kiasi cha dola milioni 16.25, Chuo cha Usafirishaji cha Taifa(NIT)chenyewe kitajikita katika usafirishaji wa anga na wao wamepewa dola za Marekani milioni 16.25 na wao DIT wamejikita katika TEHAMA.

Alipoulizwa kwanini DIT wameamua kujikita katika TEHAMA, Dk.Matiko amejibu hivi "tuliona tujikite katika eneo la ujuzi wa kidigital, elimu ya kidigital inahitajika sana, kwa hiyo lazima elimu hiyo ifike kwa kila mmoja wetu.Kuna ombwe kubwa ndio maana watu wanaibiwa fedha kwenye simu, hivyo kila mtanzania ni vema akawa na elimu ya awali kuhusi matumizi ya digitali.

"Tunaangalia katika nyanja tatu , kwanza tunamuangalia mtu ambaye hana elimu kubwa lakini tunataka apate elimu itakayomuwezesha kutumia vifaa vya TEHAMA kwa ufanisi, mfano anayetumia simu.Kwa hiyo tutaangalia jamii nzima bila kuangalia viwango vya elimu, tutakuwa na programu ambayo itatuwezesha kutoa elimu ya namna ya kutumia mitandao ya kidigitali.

"Pili tutaangalia ni namna gani tutaboresha mitalaa yetu, mtu yoyote bila kujali taaluma yake awe na uelewa wa kutumia angalau Lptop kwa ajili ya masuala yake.Pia tutaangalia viwango vya elimu na kutoa mafunzo , hivyo hakuna mtu ambaye ataachwa.Tunakwenda huko kwasababu tuafahamu huduma nyingi zinakwenda katika mndao, zamani cheti cha kuzaliwa ilikuwa lazima uende RITA lakini sasa unakipata mtandaoni".

Aidha amesema katika mradi wa RAFIC kuna baadhi ya vitu wanatakiwa kufanya na mojawapo  ni kupata cheti cha kutambulika kimataifa(ISO 21001) na mchakato unakwenda vizuri na matarajio yao DIT itakuwa taasisi ya kwanza kupata kupata hiyo ISO.


Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam(DIT) Profesa Preksedis Marco akielezea jambo wakati wa semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine amezungumzia jinsi ambavyo wanautekeleza mradi wa RAFIC katika eneo la TEHAMA.




Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Taasisi ya Tekbolojia Dar es Salaam(DIT) Amani Kanana akielezea sababu za kuandaa semina hiyo kwa waandishi wa habari.

Mkuu wa Kitengo cha na Viwanda wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam(DIT) Dk.John Msumba akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa semina , ambapo ametumia nafasi hiyo kuelezea hatua mbalimbali wanazochukua katika kutoa mchango wao ukiwemo wa kutumia watalaamu wao kutengeneza vifaa mbalimbali ambavyo vinatumika kutatua changamoto zinazoikabili jamii ikiwemo wakati wa majanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...