Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Lusajo Kafuko akizungumza na wamiliki na walezi katika vituo vya makuzi na malezi kwa watoto wachanga na watoto wadogo, mafunzo hayo yametolewa wilayani Mkuranga mkoani pwani.


KATIKA kuhakikisha watoto wanapata huduma za malezi, Makuzi na Maendeleo  ya awali kadiri ya  taratibu za serikali Shirika la Anjita Child Development Foundation kwa kushirikiana na serikali  limeendelea kutoa mafunzo kwa wamiliki na walezi wa vituo vya kulelea watoto wadogo na watoto wachanga  mchana.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani  Mkuranga Mkoani Pwani, Meneja Mradi wa Shirika la Anjia, Janeth Malela amesema kuwa mafunzo hayo yatasaidia uboreshaji wa  huduma kwa watoto  vituoni ikiwepo  wamiliki kuendelea kufanya  usajili wa vituo, kwani kwa  kufanya hivyo kunaongezea thamani vituo hivyo na kuvifanya  vitambulike  rasmi  kisheria.

Janeth amesema, watoto kuwepo  katika vituo  hivyo kunasaidia ulinzi na usalama wa watoto, kuwepo kwa ujifunzaji wa awali kwa  watoto na wazazi /walezi wanapata muda wa kufanya shughuli  za kiuchumi.

Amefafanua pia, program ya 'mafunzo kwa wote' yamewalenga wamiliki na walezi  wote  katika mikoa  ya Rukwa, Pwani, Mtwara, Lindi, Kagera, Arusha, Kilimanjaro, Njombe na Ruvuma. Ambapo kwa awamu  ya kwanza yamefanyika Rukwa, Pwani na Mtwara, na kwa mwaka wa fedha 2022/ 2023 mikoa iliyobakiwa  itatekelezwa.

Akizungumzia kuhusu serikali imejipangaje kuhusiana na huduma vituoni, Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Lusajo Kafuko amewaasa wamiliki wa vituo vya Malezi na makuzi kuvisajili Serikalini ili watambulike na shughuli zao zitambulike Serikalini.

Amesema usajili wa vituo hivyo ni bure kwani sheria ya mtoto namba 21 ya Mwaka 2009 kifungu cha 147 mpaka 152 na kanuni za watoto imetoa ufafanuai kuhusu vituo vya kulelea watoto wadogo na watoto  wachanga  mchana na  imeeleza taratibu za kufuata wakati wa kufungua vituo vya makuzi na malezi kuwa na vigezo vinavyohitajika.

Amesema kuwa wilaya ya Mkuranga inavituo 123 vinavyojulikana na ustawi wa jamii kati ya hivyo vimesajiliwa vituo 21.Hivyo ni  vema kwa kila  anaeanzisha  asajili  kwanza kwaajili  ya kumlinda mtoto.

Kwa upande wa Mwakilishi wa wamiliki Eva John, amelishukuru  shirika la Anjita na serikali  kwa utoaji wa mafunzo yaliyokuwa ya vitendo  zaidi na kusaidia uundaji wa umoja  wa wamiliki  wa day care centers -mkuranga na kutuelekeza vyuo vya malezi vinavyotambulika na serikali ambapo itasaidia kuongeza  ujuzi kwa wamiliki  na walezi.

Eva amesema, jitihada zote za Anjita na serikali zimesaidia kuongeza  uelewa kwao na kuanza kufanya  mabadiliko  chanya  ya kutoa  huduma  za vituo   kwa watoto na kuwepo  na umoja  huo utawasaidia  kujadiliana na kupeana uzoefu  katika eneo la huduma vituoni.

Eva amesisitiza pia serikali  na wadau wasichoke waendelee na jitihada hizo na ikiwezekana hadi  kwa wazazi/walezi yawafikie ingawaje  pia wao  kama wamiliki  na walezi vituoni watasaidia kutoa  elimu  ya malezi kwa wazazi/ walezi katika vituo.
Mratibu, Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto kutoka shirika la Anjita Child Development Foundation, Yasinta Mlay akitoa maelekezo kwa makundi wakati wa mafunzo ya Malezi na makuzi kwa watoto yaliyofanyika wilayani Mkuranga mKoani Pwani Novemba 20,2021.
Walezi wakifundishwa baadhi ya michezo ya watoto inayofuata sheria wakati wa mafunzo ya malezi na makuzi kwa wamiliki na walezi wa watoto wachanga na watoto wadogo.

Makundi ya wanaopewa mafunzo kwa watoto wachanga na watoto wadogo wakiendelea kufanya kazi walizopewa na mtoa mafunzo.
Mmpoja wa walezi wa watoto akitoa moja ya mchezo wa kumpongeza mtoto ambapo amefanya vizuri (Mpasho) wakati wa mafunzo kwa walezi na wamiliki wa vituo vya malezi kwa watoto wachanga na watoto wadogo mchana.
Mazoezi yakiendelea kwa walezi na wamiliki wa vituo vya malezi na makuzi kwa watoto katika mafunzo yaliyofanyika wilayani Mkuranga Mkoani Pwani Novemba 20,2021.


Wawasilishaji wa makundi wakiwasilisha majibu ya maswali waliyopewa na Mkufunzi wao wakati wa mafunzo yaliyofanyika wilayani Mkuranga Mkoani Pwani Novemba 20,2021.









Picha mbalimbali katika makundi ya wamiliki na walezi wa watoto wachanga na watoto wadogo wakati wa mafunzo yaliyofanyika wilayani Mkuranga Mkoani Pwani Novemba 20,2021.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...