Na. John Mapepele

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan ameipongeza Timu ya Taifa ya Walemavu ya Mpira wa Miguu (Tembo Warriors) kwa kufuzu Kombe la Dunia nchini  Uturuki Oktoba 2022.

"Nawapongeza  viongozi wa Wizara na TFF na nawataka  mfanye maandalizi mazuri zaidi kuelekea  michuano hiyo ili tuwe na timu bora itakayotutangaza  vyema". imesema taarifa aliyoitoa Mhe. Rais kwenye mtandao wake wa Twitter.

Naye, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Kassim Majaliwa leo akiwa jijini Mbeya  ameipongeza Timu ya Tembo kwa kufuzu kuingia kwenye mashindano ya Dunia.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa  ambaye ameongoza watanzania  kuwapa hamasa wachezaji wakati wa mechi hiyo amewapongeza wachezaji na  Kamati  maalum aliyoiteua kuratibu iliyokuwa inasimamiwa na Katibu Mkuu wa Wizara yake Dkt. Hassan Abbasi.

Akizungumza na wachezaji mara baada ya kushinda mechi ya kufuzu dhidi ya  Cameroon magoli 5-0 Mhe. Bashungwa amesema  Serikali itaendelea kuisaidia timu hiyo ili kuhakikisha inaendelea kulilitea heshima taifa katika mashindano ya dunia yanayokuja.

Kwa upande wake Dkt. Hassan Abbasi amesema amefurahishwa na hatua ya timu hiyo kazi iliyobaki ni kuhakikisha kombe hilo la CANAF 2021 linabaki Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...