Waziri Simbachawene akizungumza na Wananchi wake wa Kijiji cha Chaludewa, Kijiji cha Mlunduzi na Kijiji cha Chinyang’huku vilivvyopo Jimboni kwake alipowatembelea kwenye Ziara ya Kikazi tarehe 30/11/2021. Amewaomba kushirikiana na serikali ya Mtaa na ya Kijiji kuhakikisha kwamba wanaangalia usalama ili kudhibiti uhalifu pamoja na kutunza mazingira yanayowazunguka. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Baadhi ya wananchi wa jimbo la Kibakwe wakiwa kwenye mkutano na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene alipowatembelewa kwenye Ziara ya Kikazi jimboni kwake Kibakwe, tarehe 29/11/2021. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri Simbachawene akikagua Majengo ya Shule ya Msingi Chaludewa iliyopo Kijiji cha Chaludewa, Kata ya Mlunduzi , jimboni kwake ikiwa ni moja ya Ziara yake ya Kikazi jimboni na kuahidi kutoa mifuko mia moja (100) ya cement ili kujenga upya madarasa yaliyo haribiwa na upepo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...