Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato TRA Zanzibar akizungumza na Maafisa wa TRA na ZRB katika ufunguzi wa Kampeni ya elimu Kwa mlipakodi Mlango Kwa Mlango Kisiwan Unguja.
Afisa wa TRA  Martenus Mallya na ZRB Zuwena Said wakitoa Elimu ya kodi kwa mfanyabiashara maeneo ya Darajan Unguja.
Afisa Msimamizi wa Kodi  TRA Joyce Ng’oja akitoa elimu kwa mlipakodi maeneo ya Darajan.
Afisa Msimamizi wa Kodi Lameck Ndinda akitoa elimu kwa mfanyabiasha kisiwan Unguja maeneo ya Darajan.

Maafisa wa Mamlaka ya Mapato TRA na Bodi ya Mapato Zanzibar ZRB wakielekea katika zoezi lakutoa elimu ya kodi mlango kwa mlango Kisiwan Unguja Darajan Zanzibar


MAMLAKA ya Mapato Tanzania ( TRA ) kwa kushirikiana na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) wameanza kamapeni ya elimu  kwa mlipakodi mlango kwa mlango Zanzibar kisiwan Unguja ambayo litafanyika Kwa muda wa siku tano kuanzia tarehe 4/12/2021 hadi 8/12/2021.

Kampeni inalenga kutoa elimu kwa walipakodi ili kuwajengea uelewa wa kutosha juu ya maswala mbalimbali yanayohusu kodi, kusikiliza maoni yao kwa ajili ya kuboresha huduma za kikodi, Kuwakumbusha kulipa kodi stahiki na kwa wakati kuskiliza kero na changamoto walizonazo na hatimaye kuzitafutia ufumbuzi. 

Zoezi hilo lilifunguliwa rasmi tarehe 4/12/2021 na Naibu Kamishna wa TRA Zanzibar  Juma Bakari Hassan  tarehe 4/12/2021 ambapo katika ufunguzi huo aliongelea  maswala mbali mbali ikiwemo kutatua changamoto za wafanyabiashara waliotembelewa na kuweza kupata taarifa sahihi Kwa ajili kusajiliwa Kwa wale ambao hawajasajiliwa 

Vilevile aliwahiimiza maofisa wa TRA kutumia lugha nzuri na kuwaelemisha walipakodi kwa ufasaha juu ya  wajibu na haki zao , kuzingatia weledi uwajibikaji na uadilifu  pia awashukuru viongozi wa ngazi mbali mbali wa Serikali ya Zanzibar Kwa ushirikiano waliotoa katika maandalizi na utekelezaji wa  zoezi la Elimu ya kodi mlango kwa mlango.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...