Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 

Washindi wa mwaka 2022 wa Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Afrika wanatarajia kutangazwa Alhamisi ya Januari 27, 2022 katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam, Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa wa ALAF Limeted, Hawa Bayumi amesema kuwa shughuli ya kutangazwa washindi hao itahudhuriwa na wadau mbalimbali wa Fasihi na Lugha ya Kiswahili.

“Kuna jopo la Majaji watatu watasoma baadhi ya kazi bora zilizoshindanishww na baadaye kutangaza Washindi wa jumla katika kila kipengele”, amesema Bayumi.

Bayumi amesema Tuzo ya Kiswahili ya MABATI-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika yenye thamani ya jumla ya Dola za Marekani 15,000 hutolewa kila mwaka kwa miswada bora, au kwa Vitabu vilivyochapishww miaka miwili kabla ya mwaka wa kutolewa zawadi katika fani za Riwaya, Ushairi, Wasifu, na Riwaya Picha.

“Miswada inayoshinda huchapishwa na Shirika la Uchapishaji Vitabu la East African Educational Publishers (EAEP), na mswada bora wa ushairi hufasiriwa kwa Kiingereza na kuchapishwa Kitabu na Shirika la Africa Poetry Book Fund”, ameeleza Bayumi 

Dhumuni la Tuzo hiyo iliyoanzushwa mwaka 2015 na Dkt. Lizzy Attree (Mkurugenzi wa Tuzo ya Coine) na Dkt. Mukoma wa Ngugi (Chuo Kikuu cha Cornell, Marekani) ni kuthamini Uandishi wa Lugha ya Kiafrika, kuhimiza sanaa ya tafsiri baina ya Lugha za Kiafrika zenyewe kwa zenyewe Pia kutafsiri maandishi ya Lugha nyingine kwa lugha za Kiafrika.
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa wa ALAF Limeted, Hawa Bayumi (wa katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu kutangazwa Washindi wa mwaka 2022 wa Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Afrika, washindi hao wanatarajiwa kutangazwa Alhamisi ya Januari 27, 2022 katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...