Na Amiri Kilagalila,Njombe
Mahakama
ya mwanzo Lugarawa halmashauri ya wilaya ya Ludewa mkoani Njombe
imemuhukumu Ombeni Ngwa'vi (25) kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa
la kuvunja nyumba ya Evaristo Mgimba na miaka miwili kwa kuiba debe moja
la maharage ambapo vifungo hivyo vitaenda kwa kufuatana na si sambamba.
Akisomewa
shitaka hilo Mwendesha mashtaka Asifiwe Asajile mbele ya hakimu Timoth
Mwakisambwe imedaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo Mei 12
mwaka huu majira ya mchana ambapo alivunja nyumba ya Evaristo Mgimba
kisha kuiba debe moja la maharage yenye thamani ya shilingi 30,000.
Mtuhumiwa
huyo amekiri kutenda kosa hilo ikiwa ni kinyume na kifungu cha sheria
namba 294(1)(a), 258(1) na 265 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya
16 marejeo ya 2019
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...