BABA mzazi wa mfanyabiashara maarufu  wa Mjini Babati Mkoani Manyara, Samson Loi Mollel aliyefariki Mei 20 amezikwa jana nyumbani kwake jijini Arusha.

Marehemu mzee Mollel ni baba mzazi wa mfanyabiashara maarufu wa Mjini Babati, Emmanuel Mollel wa maduka ya vifaa vya ujenzi Manuu Hardware na nyumba za kulala wageni ya New Dream.

Marehemu mzee Mollel ambaye alizaliwa Mei 5 mwaka 1937 katika kata ya Sokoni 2 Mkoani Arusha amebahatika kupata watoto 17 wakiume nane na wakike tisa ila wanne wametangulia mbele ya haki.

Marehemu mzee Mollel ambaye katika kipindi cha uhai wake alijihusisha na kilimo na biashara alipata wajukuu 62 na vitukuu 25.

Akizungumza kwenye mazishi hayo mfanyabiashara maarufu Emmanuel Mollel (Manu Hardware) amewashukuru ndugu jamaa na marafiki waliofika kumsindikiza marehemu baba yake kwenye safari yake ya mwisho.

"Marafiki na jamaa zangu wengi wametoka Babati hadi huku Arusha kushiriki mazishi ya, baba yetu tunawashukuru sana kuja kutufariji, Baba yetu amevipiga vita vilivyo vizuri mwendo ameumaliza imani ameilinda" amesema.

Amesema siyo rahisi kumshukuru mtu mmoja mmoja kwa kadri ya uhusika wake, anawaomba wote kwa pamoja wapokee shukuranj za dhati.

"Baba yetu alikuwa mpenda watu, mcheshi na alitoa ushirikiano na jamii, hakuwahi kumbagua mtu yeyote yule na aliwapenda watu wa nyumba yake, Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe," amesema.

Mbunge wa viti maalum Vijana Taifa kupitia mkoa wa Manyara, Asia Halamga akizungumza kwenye mazishi hayo amesema amewawakilisha wabunge wa mkoa wa Manyara ambao hivi sasa wapo
Bungeni jijini Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Hiiti amesema kwenye mazishi yao wamewawakilisha madiwani wenzao akiwa na Diwani wa kata ya Bagara Yona Sulle.

Kada maarufu wa CCM Mjini Babati Cosmas Masauda amesema mfanyabiashara Manuu Hardware ni mtu wa kujitoa kwenye matukio mbalimbali ya watu ndiyo sababu amesindikizwa na watu wengi kutoka Mkoani Manyara.

Mdau wa maendeleo wa Mjini Babati, Emmanuel Khambay amesema wameshiriki kumfariji mdau mwenzao Manuu Hardware kwenye mazishi ya baba yake marehemu mzee Mollel.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...