Bodi ya watalaamu wa ununuzi na ugavi (PSPTB), imebaini bado kuna waajiri wanaoajili watu kufanya kazi za ununuzi na ugavi bila usajili wa Bodi hiyo. 

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Watalaamu wa ununuzi na ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi amesema kuwa kwenye taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) zimeonyesha ukiukwajili wa Sheria kwa Kitengo cha Ununuzi kuwa na Wakuu wa Vitengo wasio na sifa za Kitaaluma.

Pia Mbanyi amesema taarifa hizo zimebaini mapungufu makubwa kwenye ukidhi wa Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake na kupelekea hasara kwa Serikali.

"Kifungu cha 11 kimeweka sharti la ulazima kwa kila anayefanya kazi za ununuzi na ugavi awe amesajiliwa na PSPTB. Kifungu cha 46 kimezuia kuajiri au kufanya kazi za ununuzi na ugavi kwa mtu yeyote ambaye hajasajiliwa na PSPTB. Na kukiuka Kifungu tajwa ni kosa la jinai na adhabu yake ni kifungo kisichozidi miaka miwili Jela, au faini isiyozidi milioni mbili au vyote kwa pamoja." Alisema Mbanyi 

Mbanyi amesisitiza kuwa PSPTB inawataka wataalam wote wanaofanya kazi kwenye kitengo cha ununuzi na ugavi kuhakikisha wanafanya kazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao kwa mujibu wa PSPTB Code of Ethics and Conduct GN. 365/2009 inayowataka wataalamu kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo ili kutoa huduma yenye kukizi viwango.

Pia Mbanyi ametoa wito kuwa PSPTB inawaagiza watalamu wa ununuzi na ugavi wa sekta binafsi na umma kufanya kazi kwa weledi na kutoa ushauri kwa umakini bila hofu ili kupata thamani ya fedha.

"PSPTB inawataka waajiri wote kuwaondoa kwenye kitengo cha ununuzi na ugavi maafisa wote wasio na sifa za Kitaalam kwa mujibu wa muongozo wa usajili wa PSPTB na muondo wa utumishi wa kada zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango, Waraka No. 03 wa mwaka 2015." Alisema Mbanyi

PSPTB inawataka waajiri kuhakikisha wakuu wa vitengo vya ununuzi na ugavi wana sifa ya usajili wa ngazi ya juu (“authorized category”).
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Watalaamu wa ununuzi na ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uwepo wa wafanyakazi wanaofanya kazi bila kusajiliwa na Bodi hiyo uliofanyika katika ofisi zake zilizopo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee .
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...