Na.Khadija Seif, Michuzi TV
BAADHI
ya wafanaybiashara wa Halmashauri ya Manispaa ya ubungo wamejitolea kuwa
mabalozi wa kuhamasisha ulipaji wa Kodi Kwa hiari ili kusaidia
kuboreshwa Kwa Miundombinu na Miradi mbalimbali kwa kutumia Mapato ya
ndani ya Halmashauri.
Akizungumza
mara baada ya kufungua semina ya ulipaji kodi kwa hiari katika Afisa
biashara wa Manispaa ya ubungo Prisca Mjema amesema Kila Mfanyabiashara
ni muhimu kuhakikisha anajenga uelewa wa kulipa Kodi kwa hiari bila
shurti.
Hata hivyo Mjema
Amekiri kuwepo Kwa changamoto ya kusuasua kwa ulipaji wa Kodi Kwa hiari
na kubaini kuwa Wafanyabiashara wengi wemekosa Elimu ya kutosha kuhusu
kulipa Kodi, tozo pamoja na ushuru Kwa biashara ndogondogo hivyo wameona
Kuna umuhimu Kampeni hiyo kutumia Mitandao ya kijamii pamoja na
kukutanisha Wafanyabiashara kuwapatia semina.
"
Tumeona ni vyema kushirikishana katika hili na kuwa mabalozi lengo la
kutoa Elimu ya ulipaji Kwa kutumia Mitandao ya kijamii kama Instagram
,Facebook na Twitter kutokana na kuwepo Kwa utawandazi hivyo itasaidia
na kurahisisha kusaambaa Kwa elimu hii Kwa haraka zaidi."
Mjema
ametoa wito Kwa Wafanyabiashara kuhakikisha wanalipia leseni za
biashara Kwa wakati ndani ya siku 21 Ili kuepuka usumbufu wa fidia.
Nae
Mmiliki wa duka la vifaa vya ujenzi Fransic Woiso amebaini kuwepo Kwa
kadhia ya viongozi kutoka Manispaa kutoweka Mazingira rafiki Kwa
Wafanyabiashara na kuwajengea hofu kutokana na wakifika maeneo ya
Biashara wanawahi kutekeleza amri Yao pasipo kumpa elimu Mfanyabiashara
huyo Kwa jinsi gani Kodi yake itaweza kunufaisha Halmashauri yake
kimaendeleo.
"Nikiri
kumekuwepo Kwa Kadhia ya kutokuwepo Mazingira rafiki kati ya kiongozi wa
Halmashauri anapofika eneo la biashara na Mfanyabiashara mwenyewe ni
Miongoni mwa vitu vinavosababisha kutolipwa Kwa wakati Kodi ya Mapato."
Pia
Woiso amehaidi kuwa Balozi wa mfano kuhakikisha anawapatia
Wafanyabiashara Elimu ya ulipaji kodi kwa hiari kuanzia kwenye magroup
ya Mitandao ya kijamii Kwa Wafanyabiashara wote.
Afisa Biashara wa Halmashauri ya Manispaa ya ubungo Prisca Mjema
akizungumza na Wafanyabiashara mara baada ya kufungua semina ya siku 3
jijini Dar es salaam yenye lengo la kutoa Elimu kwa ulipaji kodi kwa
hiari Kwa Wafanyabiashara na kukusanya changamoto za Wafanyabiashara haoWafanyabiashara
wakiwa pamoja na viongozi kutoka Halmashauri ya Manispaa ya ubungo
ikiongoza na Afisa Biashara prisca Mjema pamoja na Mhasibu wa
Halmashauri hiyo Adam wakati wa kumaliza semina Wafanyabiashara kupitia
Kampeni kutoa Elimu ya ulipaji kodi kwa hiari
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...