Na John Walter-Babati
Aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu katika halmashauri ya mji wa Babati Bw. Faustine Masunga , amefariki dunia.
Alikuwa na umri wa miaka 51.

Taarifa iliyotolewa na ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Babati imeeleza kuwa kifo hicho kimetokea usiku wa kuamkia Mei 16,2022.

Awali alilazwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa na baadaye hospitali ya taifa ya Muhimbili ambapo alifariki dunia akiendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo.

Faustine Masunga alikaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Babati tangu alipoondooka aliyekuwa Mkurugenzi wa mji wa Babati Fortunatus Fwema baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko Agosti 2021.

Msiba upo nyumbani kwake katika mtaa wa Bagara mjini Babati.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...