KATIBU Mkuu wa Chama cha Aliance Demokratc Change (ADC) Doyo Hassan Doyo amesema suala la CCM kuzungumzia mchakato wa Katiba mpya kwamba imeridhia na wanasubiri Serikali ione namna gani linafufuliwa wamelipokea kwa mikono miwili.


Doyo aliyasema hayo leo mjini Handeni wakati akifungua Tawi Mtaa wa Mabanda Kata ya Mabanda Jimbo la Handeni Mjini  na kufanikiwa kupata wanachama zaidi ya 60 ambao walichukua kadi ya ADC  huku akiwashukuru wananchi kwa kukiunga mkono chama hicho .

Alisema hivi sasa wanasubiri Serikali iweze kuona namna gani jambo hilo linafufuliwa ili mchakato uanze huku akieleze wamelipokea kwa furaha japokuwa hawaamini kwamba CCM wana nia thabiti ya kujenga mifumo ya katiba ambayo watanzania wanaihitaji.

Alisema kutokana na wasiwasi huo wanaitaka Serikali ya CCM iweze kutoa tamko la haraka la kukubali huo mfumo na kwamba unaanza lini na mchakato wake utakuwaje kutokana na kwamba ni suala rahisi sana .

“Kwani sheria ya mabadiliko ya katiba imeshatungwa hivyo ni kuifufua tu na bunge bado linakaa na tunaamini kama Serikali ipo makini na suala ka katiba mpya na CCM imebariki hivyo itoa tamko haraka ni lini mchakato wa katiba mpya utaanza”Alisema Katibu Mkuu huyo.

Hata hivyo alisema suala la katiba mpya kwa watanzania ni muhimu sana na ndio maana wamekuwa wakilipigia kelele mara kwa mara ili kuhakikisha inapatikana.

Katika hatua nyengina Katibu huyo Mkuu aliwataka wananchi wa Kata hiyo kuhakikisha wanajitokea ,kwa wingi kuhesabiwa wakati wa zoezi la Sensa ya watu na Makazi linatalofanyika mwezi Agosti mwaka huu hapa nchini kutokana na kwamba ni tukio muhimu kwa nchi.

 

KATIBU Mkuu wa Chama cha Aliance Demokratc Change (ADC) Doyo Hassan Doyo akizungumza na wananchi wa Kata ya Mabanda Jimbo la Handeni mjini
KATIBU Mkuu wa Chama cha Aliance Demokratc Change (ADC) Doyo Hassan Doyo kulia akigaiawa kadi kwa wanachama wapya waliojiunga na chama hicho mara baada ya kuzindua tawi hilo
KATIBU Mkuu wa Chama cha Aliance Demokratc Change (ADC) Doyo Hassan Doyo kulia akigaiawa kadi kwa wanachama wapya waliojiunga na chama hicho mara baada ya kuzindua tawi hilo
KATIBU Mkuu wa Chama cha Aliance Demokratc Change (ADC) Doyo Hassan Doyo kulia akigaiawa kadi kwa wanachama wapya waliojiunga na chama hicho mara baada ya kuzindua tawi hilo


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...