JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

 

 

 

 

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA  MADELU (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA

SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO

YA MAPATO NA MATUMIZI KWA

 MWAKA 2022/23

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

14   Juni 2022                          Dodoma


 


 I.                             UTANGULIZI

1.            Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu lipokee, lijadili na kukubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2022/23. Bajeti hii inawasilishwa kwa mujibu wa Ibara ya 137 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na Kifungu cha 23 (3) cha Sheria ya Bajeti, Sura 439 pamoja na Kifungu cha 124 (4) cha Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Juni 2020.

2.                  Mheshimiwa Spika, pamoja na hotuba hii ninawasilisha vitabu vinne vinavyoelezea kwa kina Bajeti ya Serikali. Kitabu cha Kwanza ni Makadirio ya Mapato; Kitabu cha Pili ni Makadirio ya Matumizi ya Kawaida kwa Wizara, Idara Zinazojitegemea na Wakala wa Serikali; Kitabu cha Tatu ni Makadirio ya Matumizi ya Kawaida kwa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa; na Kitabu cha Nne ni Makadirio ya Matumizi ya Maendeleo kwa Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2022 pamoja na Muswada wa Sheria ya Matumizi ya Serikali wa mwaka 2022 nayo ni sehemu ya bajeti hii.

3.            Mheshimiwa Spika, makadirio ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23 yameandaliwa kwa kuzingatia nyaraka na miongozo mbalimbali ikiwemo: Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 - 2025/26 ambao umeandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020; Dira ya Maendeleo ya Afrika Mashariki 2050; Ajenda ya Maendeleo ya Afrika 2063; Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030; Mwongozo wa Ushirikiano wa Maendeleo; na makubaliano mengine ya kikanda na kimataifa ambayo Tanzania imeyaridhia.

 

4.            Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23. Kwa namna ya pekee nitumie fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini katika dhamana hii ya kuongoza Wizara ya Fedha na Mipango.

 

 

 II.       MWENENDO WA MAPATO NA MATUMIZI  2021/22

 

Mwenendo wa Mapato

5.            Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2021/22, Serikali ilitarajia kukusanya jumla ya shilingi trilioni 37.99 kutoka katika vyanzo vyote vya ndani na nje ambapo hadi Aprili 2022, kiasi cha shilingi trilioni 29.84 kimekusanywa. Mchanganuo wa mapato yaliyopatikana hadi Aprili 2022 ni kama ifuatavyo:

                  (i)         Mapato yaliyokusanywa kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), yalikuwa ni shilingi trilioni 17.20,  ambapo lengo la mwaka ni shilingi trilioni 21.78;

                (ii)         Mapato yasiyo ya kodi yalifikia shilingi trilioni 2.03, ambapo lengo la mwaka ni shilingi trilioni 3.05;

              (iii)         Mapato ya Halmashauri yalifikia shilingi bilioni  759.0, ambapo lengo la mwaka ni shilingi bilioni 863.9;

              (iv)          Misaada na mikopo yenye masharti nafuu kutoka kwa Washirika wa Maendeleo ilifikia shilingi trilioni 3.93, sawa na asilimia 92.0 ya lengo la mwaka la shilingi trilioni 4.27;

                 (v)         Mikopo kutoka vyanzo vya ndani ilifikia shilingi trilioni 4.12, ambapo lengo la mwaka ni shilingi trilioni 4.99; na

              (vi)          Mikopo yenye masharti ya kibiashara ilifikia shilingi trilioni 1.81, ambapo lengo la mwaka ni kukopa shilingi trilioni 3.05.

 

Mwenendo wa Matumizi

6.            Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022, jumla ya shilingi trilioni 29.40 zimetolewa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo. Kati ya kiasi hicho, shilingi trilioni 18.79, zilitolewa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ambazo zinajumuisha shilingi trilioni 6.73 kwa ajili ya mishahara, shilingi trilioni 4.79 Matumizi Mengineyo na shilingi trilioni 7.27 kugharamia deni la Serikali.  Jumla ya shilingi trilioni 10.61, sawa na asilimia 74.1 ya lengo la mwaka zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kiasi hiki hakijumuishi baadhi ya fedha zilizopelekwa moja kwa moja kwenye utakelezaji wa miradi (D-fund). Fedha hizi zitajumuishwa kwenye hesabu za Serikali mwishoni mwa mwaka wa fedha pindi taratibu za kihasibu zitakapokamilika.

 

 

 

Tathmini ya Uhimilivu wa Deni la Serikali

7.            Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, deni la Serikali lilikuwa shilingi trilioni 69.44, sawa na ongezeko la asilimia 14.4 ikilinganishwa na shilingi trilioni 60.72 Aprili 2021. Kati ya kiasi hicho, deni la ndani ni shilingi trilioni 22.37, sawa na asilimia 32.2 na deni la nje ni shilingi trilioni 47.07, sawa na asilimia 67.8. Kati ya deni la nje, deni lenye masharti ya kibiashara ni shilingi trilioni 14.27, sawa na asilimia 30.3. Hivyo, sehemu kubwa ya deni la nje ni mikopo yenye masharti nafuu.

8.            Mheshimiwa Spika, tathmini ya uhimilivu wa deni la Serikali iliyofanyika Novemba 2021 kwa mujibu wa Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada Sura 134 ilionesha kuwa viashiria vya deni la Serikali viko ndani ya wigo unaokubalika kimataifa katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu. Katika Tathmini hiyo, viashiria vinaonesha kuwa: uwiano wa thamani ya sasa ya deni la Serikali kwa Pato la Taifa ni asilimia 31.0 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 55; uwiano wa thamani ya sasa ya deni la nje kwa Pato la Taifa ni asilimia 18.8 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 40; na uwiano wa thamani ya sasa ya deni la nje kwa mauzo ya nje ni asilimia 142.4 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 180. 

 

Tathmini ya Kukopesheka kwa Nchi (Credit Rating)

9.             Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, zoezi la tathmini na ukadiriaji wa kukopesheka kwa nchi (credit rating) ambalo lilisimama hapo awali lilianza tena kupitia benki ya Citibank ambayo ilikuwa mshauri wa Serikali. Hadi kufikia mwezi Mei 2022, Serikali imefikia hatua za mwisho za kukamilisha taratibu za ununuzi ambapo imefanikiwa kuchagua kampuni mbili ambazo zinatambulika kimataifa na kupitia mikataba yao. Aidha, Serikali inaendelea na mazungumzo na kampuni hizo pamoja na kuandaa takwimu mbalimbali ambazo zitatumika katika zoezi la tathmini na ukadiriaji wa kukopesheka. Serikali inategemea kukamilisha zoezi hili ndani ya mwaka 2022/23. Naomba nichukue fursa hii kuziomba taasisi za Serikali, za binafsi na benki zitakazopata nafasi ya kuhojiwa na wataalamu wa Kampuni hizo kutoa ushirikiano kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi. Kukamilika kwa zoezi hili kutatuwezesha kuongeza wigo wa wakopeshaji kwa Serikali na makampuni binafsi hususan katika masoko ya mitaji ya kimataifa (International Capital Markets).

 

III.                          BAJETI  YA MWAKA WA FEDHA 2022/23

10.       Mheshimiwa Spika,  Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23 ni ya pili katika utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 - 2025/26 wenye dhima ya Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu”. Aidha, dhima kuu ya bajeti ya mwaka 2022/23 kama ilivyokubaliwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Kuongeza Kasi ya Kufufua Uchumi na Kuimarisha Sekta za Uzalishaji kwa ajili ya Kuboresha Maisha”. Katika utekelezaji wa dhima hiyo kwa mwaka 2022/23 kipaumbele kitakuwa katika sekta za uzalishaji zikiwemo Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Nishati, Uwekezaji na Biashara. Lengo la Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM ni kujenga uchumi, kukabiliana na umasikini pamoja na ukosefu wa ajira hasa kwa vijana.

 

Shabaha za Uchumi Jumla

11.       Mheshimiwa Spika, kutokana na mambo yaliyozingatiwa katika uandaaji wa bajeti hii, shabaha za uchumi jumla katika kipindi cha mwaka 2022/23 ni kama ifuatavyo:

(i)        Ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kufikia asilimia 4.7 mwaka 2022 na asilimia 5.3 kwa mwaka 2023;

(ii)      Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa asilimia kati ya 3.0  hadi 7.0 katika muda wa kati;

(iii)    Mapato ya ndani kufikia asilimia 14.9 ya Pato la Taifa mwaka 2022/23;

(iv)    Mapato ya kodi kufikia asilimia 11.7 ya Pato la Taifa mwaka 2022/23; na

(v)       Kuwa na akiba ya fedha za kigeni kwa kiwango cha kukidhi mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje kwa kipindi kisichopungua miezi minne (4);

 

IV.     MAMBO MUHIMU KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23

12.       Mheshimiwa Spika, nchi zote duniani zinapita kwenye athari kubwa za UVIKO 19 na vita kati ya Urusi na Ukraine iliyoanza Februari 2022 ambayo imeendelea kuleta athari katika mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania kutokana na mwingiliano wa shughuli za kiuchumi na kijamii. Madhara ya UVIKO-19, yamekuwa na makali zaidi baada ya uchumi kuanza kurejea, kwa kuwa nchi zilikuwa katika “lockdown” na nyingine kupunguza uzalishaji wa bidhaa. Uchumi unaporejea katika hali ya uzalishaji mataifa yote yanahitaji bidhaa ambazo ziliachwa kuzalishwa hivyo kusababisha upungufu. Kungali hali iko hivyo, vita kati ya Urusi na Ukraine imeongeza upungufu wa bidhaa kwa kuathiri uzalishaji na mnyororo wa usambazaji. Kwa mujibu wa Shirika la Chakula Duniani, nchi za Urusi na Ukraine ni kati ya nchi zenye uzalishaji na uuzaji mkubwa wa mazao mbalimbali ikiwemo ngano, mafuta ya kula na shayiri.

 

13.       Mheshimiwa Spika, nchi ya Urusi ni ya pili katika uzalishaji wa gesi asilia na bidhaa za mafuta ya petroli duniani. Kadhalika, nchi ya Ukraine ni miongoni mwa nchi zinazozalisha mafuta ya alizeti kwa wingi duniani.  Kufuatia madhara haya ya vita, ni dhahiri kuwa uchumi na gharama za maisha duniani hazitabaki zilivyokuwa awali. Ndio maana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM ameelekeza bajeti hii ya Serikali ijikite kuchukua hatua za kutoa unafuu kwa wananchi na kufufua uchumi. Bajeti hii itatilia mkazo Sera za Mapato, Sera za matumizi, kujali ufanisi (Value for Money), mapambano ya vitendo vya rushwa na kuwekeza kwenye Sekta za uzalishaji ili kutengeneza ajira  kwa vijana.

 

Mikakati ya kuongeza Mapato  Mwaka 2022/23

 

14.       Mheshimiwa Spika, nawapongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania na taasisi zingine zinazokusanya mapato na maduhuli ya Serikali. Tumepiga hatua kubwa kwenye makusanyo ya ndani. Hadi Aprili 2022, ukusanyaji wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi ikijumuisha mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa umefikia shilingi trilioni 19.99, sawa na asilimia 93.3 ya makadirio ya kukusanya shilingi trilioni 21.42 katika kipindi hicho. Kati ya kiasi hicho, mapato ya kodi yamefikia shilingi trilioni 17.20, sawa na asilimia 94.5 ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 18.2, mapato yasiyo ya kodi yamefikia shilingi trilioni 2.03, sawa na asilimia 81.2 ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 2.5 na mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa yamefikia shilingi bilioni 759.0, ikiwa ni asilimia 104.8 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 724.1 katika kipindi hicho.

15.       Mheshimiwa Spika,  pamoja na mafanikio hayo, bado kuna vitendo vya rushwa kwenye ukusanyaji wa mapato, hasa kwenye kodi kubwa, mapato ya Mamlaka za Serikali za mitaa na ardhi. Kuna mapato ya Serikali yanaingia kwenye mifuko ya watu binafsi. Hii inafanyika kwa kukadiria viwango vya juu ili katika majadiliano ya kwenda kwenye kodi stahiki kinapunguzwa kiasi chini ya kile kinachostahili na kilichopunguzwa kinaingia mifuko binafsi. Serikali imeshapokea taarifa kadhaa za matukio ya aina hii na inaendelea kulifuatilia kwa umakini sana jambo hili. Wale wanaokataa kutoa rushwa ndio wanaoonewa zaidi, ndio wanaobambikwa makadirio yasio halisi kwa kuwakomoa, ndio wanaotishiwa kufilisiwa. Jambo hili halikubaliki. Nitoe rai jambo hili liachwe mara moja. Tuache utaratibu wa kufanya majadiliano (bargaining) kwenye kulipa kodi. Watumishi wa umma wanaokusanya kodi na maduhuli ya Serikali wanaowaomba wafanyabiashara wawapunguzie wanachotakiwa kulipa ili kisichoingia serikalini wapate wao wanafanya makosa ya uhujumu uchumi. Kadhalika wapo wafanyabiashara na wauza maduka wanaowaambia wananchi nikupe bei ya risiti ya TRA au bila risiti, na bei ile isiyo na risiti inakuwa ndogo kuliko bei ya risiti ili kuwashawishi wakwepe kulipa mapato ya Seriakili na wao wenyewe wabaki na kodi ya Serikali. Huu ni uhujumu uchumi. Naagiza vitendo hivyo vikome mara moja na ambaye hataacha atakutana na mkono wa sheria.

 

16.       Mheshimiwa Spika, nitoe rai kwa watanzania wote kulipa kodi wanayostahili kulipa, wala wasiogope vitisho, na wala wasidhanie kuwa kuna wakati watakulipizia kisasi, toa taarifa ofisi ya TAKUKURU iliyo karibu nawe, ama toa taarifa Idara ya Usalama wa Taifa iliyo karibu nawe. Watumishi wa aina hiyo  watakaobainika hutawakuta tena ofisi za umma, wala hatutawahamisha, Tutawafukuza kazi. Mheshemiwa Rais anachukizwa sana na ukosefu wa maadili na uaminifu wa baadhi ya watumishi wa umma. Asitokee anayedhani ana haki sana ya kuwa mtumishi wa umma, hii ni dhamana tu. Wala asitokee anayedhani vijana wahitimu wa kitanzania walioko mtaani na hawana kazi akadhani hawana haki ya kuwa watumishi wa umma. Tunao uwezo wa kupangua safu nzima ya utumishi wa umma na tukapanga safu mpya ya vijana hawa walioko mtaani. Kwenye uadilifu na uaminifu, hata tusibabaishane,  Tutawakamata, Tutawashitaki na Tutawafunga. Lazima tukomeshe kabisa vitendo vya rushwa kwenye mapato na matumizi.

 

17.       Mheshimiwa Spika, mambo mengine tunayotarajia kuyafanya kwenye sera ya mapato ni kuimarisha matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kufanya makadirio ya kodi kwa wafanyabiashara wadogo ambao hawana uwezo wa kutunza kumbukumbu na kutengeneza hesabu za biashara zao (Presumptive Regime), kuwekeza kwenye matumizi ya teknolojia ili kurahisisha uwasilishaji wa ritani za kodi kielektroniki (electronic filing) na ulipaji kodi kwa wakati; Kuimarisha Mfumo wa Serikali wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Mapato (GePG) na kuhimiza malipo ya Serikali kutumia Namba ya Kumbukumbu ya Malipo; na kuimarisha mifumo ya usimamizi katika Mashirika, Taasisi za Umma na Wakala za Serikali ili kuongeza ufanisi na kuhakikisha gawio na michango stahiki inawasilishwa kwa wakati. Ili kukuza mchango wa sekta binafsi katika kukuza uchumi, kutoa ajira na kuongeza mapato, Serikali inapanga kuendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara na kuipa nafasi zaidi sekta binafsi. Aidha, Serikali imepanga kuendeleza uanzishwaji wa vituo vya pamoja vya utoaji huduma ili kuwezesha huduma muhimu zinazohitajika katika kuanzisha na kufanya biashara kupatikana sehemu moja.

 

Mkakati wa Kubana Matumizi

18.       Mheshimiwa Spika, Sera za matumizi katika mwaka 2022/23 zitakuwa za kubana na kuondoa matumizi yasiyo ya lazima. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali inatarajia kudhibiti ununuzi na matumizi ya magari kwa kuzingatia Waraka wa Rais na.1 wa mwaka 1998 kuhusu hatua za kubana matumizi ya Serikali na Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Na. 2 wa mwaka 2021 kuhusu utaratibu wa kutumia magari, aina na stahili za magari kwa viongozi katika utumishi wa umma ili kubana matumizi. Baadhi ya maeneo yenye gharama kubwa sana kwa serikali ni Ununuzi wa magari, Ununuzi wa mafuta ya uendeshaji, Ununuzi wa vipuli na matengenezo. Tunapanga kuchukua hatua za muda mfupi na za muda mrefu. Lazima, matumizi ya Serikali na matumizi ya watumishi wa umma yote yaakisi ugumu wa maisha wanayopitia wananchi wetu kufuatia athari za majanga hususan ya UVIKO-19 ili fedha zinazopatikana zifanye mambo muhimu hapa nchini.  Hatua za muda mfupi zitakazochukuliwa ni kupunguza safari za ndani na nje, kukata fedha za ununuzi usio wa lazima, kupunguza ukubwa wa uwakilishi kwenye mikutano ya ndani na nje, na tutapimiana mafuta ya magari ya Serikali kila mwezi kufuatana na shughuli za lazima. Utaratibu huu unatumika kwa wabunge, na hawajaacha kufanya shughuli majimboni mwao, BOT wanapimiwa, baadhi ya Taasisi za UN wanapimiwa. Namwelekeza Mlipaji Mkuu wa Serikali afanye uchambuzi wa wastani wa mahitaji ya mafuta kufuatana na aina ya majukumu, ulazima wa majukumu na ngazi katika utumishi.

19.       Mheshimiwa Spika,  kwa upande wa hatua za muda wa kati na  muda mrefu, napendekeza Serikali kubadili kabisa utaratibu  uliopo kwa kuwakopesha magari watumishi wenye hadhi ya kuwa na gari la Serikali wawe na magari yao wenyewe, wafanye matengenezo wenyewe, wanunue vipuri wenyewe na masuala ya mafuta yaangaliwe kwa utaratibu utakaoonekana unafaa. Kwa sasa Serikali ina magari zaidi ya 15,742, pikipiki 14,047 na mitambo 373 na inatumia zaidi ya shilingi 558,453,134,226.05 kwa mwaka kwa ajili ya ununuzi wa magari, ununuzi wa mafuta ya uendeshaji, ununuzi wa vipuri na matengenezo ambapo kwa sasa ni zaidi ya shilingi bilioni 500. Ukiondoa vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na Mahakama, upande wa Serikali wabaki viongozi wakuu wa Wizara, Mashirika, wakala, mikoa, wilaya na Miradi ambao wasimamizi watakuwa eneo la mradi (site) muda mwingi ambapo kwenye makundi haya hawatazidi watano kwa taasisi, wengine wote wenye stahili ya gari la Serikali wakopeshwe, watumie magari yao, watasimamia vizuri matumizi, matengenezo, mafuta na vipuri. Tutaondoa utaratibu uliozoeleka, dereva na gari anapitishwa chini, bosi anapanda ndege mpaka Mwanza au Mbeya kutoka Dar es Salaam na kurudi hivyo hivyo. Kuna utafiti wa siri ulifanywa, kwa siku moja yalibainika magari ya Serikali yaliyotoka Dodoma kwenda Dar es Salaam yalikuwa 132, na yaliyokuwa yanatoka Dar es Salaam yakipishana kuja Dodoma yalikuwa 76, na mengine 8 yalikuwa yamepinduka. Je kwa mwezi ni gharama kiasi gani?

20.       Mheshimiwa Spika, kwa utaratibu huo gharama za matumizi ya magari serikalini zitakuwa takribani shilingi 50,508,038,843.09. Zaidi ya shilingi billion 500 zitaokolewa na kuelekezwa kwenye ununuzi wa dawa muhimu hospitalini, kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma vyuo vya kati, na kutekeleza miradi ya maendeleo. Tumezidi kupenda ubosi, magari makubwa kwa kila mtu serikalini, matumizi ya starehe, wakati katika nchi yetu bado kuna watu wanapata shida kupata mlo mmoja. Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania ameielekeza Wizara ya Fedha na Mipango  ifanyie kazi jambo hili la kuelekeza fedha kwenye matumizi ya msingi tu.  Jambo hili halitaathiri mtumishi bali litafanyika gradually, yaani by phasing out, yaani tunabadilisha kadri watu wanavyopanda kustahili kukopa na kutokuajiri madereva kadri wanavyostaafu na kadri maafisa wanavyohamia skimu za kukopa. Madereva wengine watabaki kwa viongozi, magari ya miradi ya site, na magari ya pool. Mtoto wa Dereva sio lazima naye aje awe dereva.

 

21.       Mheshimiwa Spika, sambamba na hayo,  Serikali itaachana na mfumo wa sasa wa Ununuzi wa Umma (Transactional Procurement) ambao umeshindwa kuleta tija kwa kuwa msingi wake mkubwa ni ulinganishaji wa zabuni zilizofunguliwa badala ya bei za bidhaa na huduma ambazo tunazijua. Mara nyingi bei hizi za ununuzi zimekuwa kubwa kuliko zile zilizopo sokoni kwa jumla na hata rejareja (wholesale and retail) na ingekuwa tunanunua kwa ajili ya nyumbani kwetu au kwa ajili ya kampuni zetu tusingekubali bei hizo. Napendekeza kuwa, ununuzi wa umma uwe wa kimkakati (Strategic Sourcing) kwa kuzingatia ukubwa wa ununuzi wa Serikali na sekta ya umma kwa ujumla (Economies of Scale) pamoja na uwiano na mfanano wa bidhaa na huduma zinazotumika serikalini na sekta ya umma yaani synergies. Sasa Serikali ni moja, bidhaa zinafanana, hata ofisi zilizoko mkoa mmoja, ila inatokea kila mmoja anakuwa na bei zake licha ya bidhaa kufanana. 

 

22.       Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti matumizi, Serikali imepanga kufanya maboresho katika mfumo wa ununuzi wa umma ili kuhakikisha ununuzi wa umma unakuwa wenye tija na unaoendana na ubora na thamani ya fedha. Tutaendelea kuboresha Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (TANePS) ikiwemo kuweka ukomo wa bei za bidhaa na huduma zinazotumika serikalini ili kudhibiti matumizi ya fedha za Serikali; Wizara ya Fedha na Mipango itahakikisha kuwa, bei zote za bidhaa na huduma zinazotumika sokoni kwa jumla na rejareja (Price Catalogue) zinaingizwa kwenye mfumo wa TANePS na kuwa kikomo (limit) cha bei zitakazotumika Serikalini. Hii itasaidia kuhakikisha kwamba mfumo wa TANePS hauruhusu watoa huduma na wakandarasi au wauza bidhaa wanaotoa bei zilizo zaidi ya soko kupata zabuni (tender) kwenye sekta ya umma.

 

23.       Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza hatua hii, Wizara ya Fedha na Mipango itatoa Waraka wa Hazina kuelekeza idara na taasisi nunuzi kununua bidhaa zinazofanana kwa bei ya kikomo. Endapo kutakuwa na ulazima wa kununua magari kwa wingi, Serikali itafanya mazungumzo na Toyota Tanzania na Japan (kwa njia za kidijitali) ili kufanya makubaliano ya jumla (framework agreement) yatakayowezesha Serikali kupata bei nafuu kama ilivyo kwa mashirika makubwa ya kimataifa kama vile UNDP. Hii itasaidia kuokoa fedha katika ununuzi wa magari pamoja na vipuri. Zoezi hili litafanywa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi. Fedha zitakazookolewa kutokana na hatua hizi Serikali itazielekeza katika ujenzi wa vyuo vya ufundi kwenye Wilaya zetu kwa ajili ya watoto wetu.

24.        Mheshimiwa Spika, napendekeza matumizi ya mifumo ya TEHAMA iwe chaguo namba moja katika utekelezaji wa shughuli za Serikali ili kubana matumizi. Kuanzia mwaka ujao wa fedha ofisi za serikali zianze paperless operations kwenye shughuli zake. Kila shughuli zifanyike kwa mtandao, mbona Bunge mmeweza? Kumbi  za Mikoa na Wilaya zote ziwe na miundombinu ya mikutano ya njia ya Mtandao (Virtual Meeting). Hata wabunge mtaweza kushiriki vikao vya Mabaraza ya Madiwani mkiwa Dodoma au hata nje ya nchi. Utaratibu wa kuitana Wakuu wa Mikoa nchi nzima, Wakuu wa Idara, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, na magari kwa nchi nzima na umbali wote  kuja kukaa mahali na kusikiliza ni mzigo kwa walipa kodi.  Tumekopa fedha kwa ajili ya mkongo wa taifa, tunalipa deni, ila tunatumia gharama kubwa kwa kufanya kazi manually. Mheshimiwa Rais anajenga chuo kikubwa cha TEHAMA, lakini tunaogopa TEHAMA. Tunataka kufuta usemi wa Government works on papers” Sasa tunasema “Government works on records”. Tumeongea na Wizara ya Kisekta kama alivyoelekeza Mheshimiwa Rais kujadili utekelezaji wa jambo hili, Wizara tafuteni mtu wa kusimika hiyo mitambo kila Wilaya. Eti mkurugenzi anakuja tokea Wialaya ya pembezoni gharama yote ile eti ameleta barua, au anakuja kutoa ufafanuzi, au wanakuja nchi nzima kwenye kikao ila anaongea mmoja kwa uwakilishi. 

 

25.       Mheshimiwa Spika, kuhusu ufanisi katika Miradi ya Maendeleo, Mheshimiwa Rais ameelekeza kuangalia upya taratibu za ununuzi na thamani ya fedha kwenye Miradi ya Maendeleo. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali - CAG ilionesha bado kuna dosari katika matumizi ya Serikali hususani kwenye ununuzi mkubwa na miradi ya maendeleo. Serikali imefuatilia eneo hili na kugundua mfumo wa kufanya ukaguzi wa taratibu za ununuzi (Compliance Audit) na wa kifedha (Financial Audit) ina upungufu. Yapo mazingira ya taratibu zote kufuatwa katika ununuzi, sheria zote za ununuzi kufuatwa, na hatua zote za ukaguzi kufuatwa lakini fedha ya umma kuibiwa. Hii inatokana na baadhi ya watumishi wa umma wasio waaminifu kupanga njama na wafanyabiashara wasio wazalendo kupandisha bei za bidhaa kwenye zabuni na kujipangia hata huyo aliyeshindania kwa kiwango cha chini anakuwa mbali na bei ya soko au gharama halisia. 

26.       Mheshimiwa Spika, kwenye mchezo wa aina hii, wanafuata sheria ya ununuzi, wanafuata taratibu za kumchagua aliyeshinda bei ya chini, ila kwa kuwa hiyo iliyoshindaniwa kwa bei ya chini ni ya chini tu ikilinganishwa na wazabuni wengine ambapo zabuni imefanywa kwa njama basi bei hizo zinakuwa juu sana ikilinganishwa na bei za bidhaa hizo hizo kwa bei ya soko. Hawa ni watu wanaoiba japo wamezingatia sheria. Serikali itaendelea kumjengea uwezo  CAG ili  kumwezesha kukagua thamani ya fedha  kwenye miradi yote mikubwa (Value for Money) na kufanya ukaguzi kwa wakati ili kukabiliana na tatizo hili. Mheshimiwa Spika, napendekeza kumwongezea fedha Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu  wa Hesabu za Serikali (CAG) ili apate watumishi wa kutosha kwa kuajiri na kuwahamisha watumishi kutoka idara yoyote ya Serikali na kuwajengea uwezo kwa mafunzo na weledi wa ukaguzi wa thamani ya fedha ili kuweza kukabiliana na tatizo hili. Mheshimiwa Spika, Serikali itafanyia marekebisho Sheria ya Ununuzi wa Umma ili kuziba mianya inayotoa fursa ya miradi kutekelezwa bila kujali thamani ya fedha (Value for Money) kama alivyoelekeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania.

27.       Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha vitengo vya ukaguzi wa ndani kwa kuvijengea uwezo wa kitaaluma na kuongeza idadi ya watumishi katika fani mbalimbali kama vile TEHAMA, uhandisi, ukadiriaji majenzi, wakemia, wanasheria na fani nyingine ili kuondokana na dhana ya wakaguzi wa ndani kuwa na taaluma ya fedha pekee. Aidha, Serikali itafanya marekebisho ya Kanuni za Fedha za Umma kwa kuziwezesha Kamati za Ukaguzi kuwa na wajumbe wa nje watatu ikiwemo Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi ili kuongeza uhuru na ufanisi wa kamati za ukaguzi kupitia Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2022. Pamoja na mambo mengine, marekebisho ya Kanuni hizo yatazitaka Kamati za Ukaguzi kuwasilisha taarifa za ukaguzi wa ndani kwa Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali kila robo mwaka.

 

28.       Mheshimiwa Spika, Serikali itafanya tathmini ya muundo na majukumu ya Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali ikiwemo kufanya stadi ya kujifunza kutoka nchi nyingine zenye Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu Serikali kama Tanzania ili kuangalia muundo unaostahili na kukidhi mahitaji ya Idara hiyo kutekeleza majukumu yake kwa uhuru na ufanisi. Vilevile napendekeza  Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali kuwa na fungu lake (Independent Vote) pamoja na kuongeza idadi ya wakaguzi wa ndani ili kuimarisha na kuboresha ufanisi katika utendaji.  Napendekeza kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 taarifa za wakaguzi wa ndani zipelekwe moja kwa moja kwa Internal Auditor General (IAG) kama alivyoelekeza Mheshimiwa Rais wakati anapokea taarifa ya CAG. IAG atakuwa anawasilisha taarifa hizi kwenye Baraza la Kazi chini ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ili kila Waziri wa kisekta aweze kupokea hoja  zinazomhusu, kuzifanyia kazi na kuchukua hatua za kinidhamu. Wakaguzi wa ndani wa ofisi mbalimbali watatoa msaada na ushauri kwa maafisa masuhuli husika ila taarifa zote ziende kwa IAG na nakala zipelekwe kwa viongozi walio juu ya maafisa masuhuli. Kwenye ngazi za Halmashauri, nakala ziende kwa wenyeviti, mamea na wakuu wa Wilaya; kwa Sekretarieti za Mikoa, nakala ziende kwa Mkuu wa mkoa; Kwa wizara, nakala ziende kwa mawaziri; na kwa taasisi, mashirika na wakala, nakala ziende kwa wenyeviti wa Bodi.

 

29.       Mheshimiwa Spika, kuna wakati inatokea tunaona miradi ikikamilika, fedha zote zikiwa zimetumika lakini miradi ikiwa chini ya viwango, jengo au mradi unakamilika ungali bado unanukia rangi lakini ukiwa umetapakaa nyufa kila kona, sementi na tofali zikiwa ni mchanga. Katika kukabiliana na hali hiyo, Serikali inamwelekeza IAG pamoja na vitengo vya ukaguzi wa ndani kuanza kufanya Technical Audit badala ya (Financial Audit) peke yake na kuanza kufanya ukaguzi kwa wakati (Real Time Audit) na ukaguzi wa mifumo (Systems Audit) ili kupunguza uwezekano wa upotevu fedha kupitia mifumo ya ukusanyaji au matumizi mabaya ya fedha za umma.

 

30.       Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la usimamizi wa fedha za umma, Serikali itahakikisha kuwa Sheria ya Fedha za Umma SURA 348 inasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo na pale itakapotokea sheria na taratibu za usimamizi wa fedha zimekiukwa ikiwa ni pamoja na kushindwa kujibu hoja zilizotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali pamoja na hoja za wakaguzi wa ndani,  Afisa Masuuli wa Fungu husika pamoja na Maafisa wake wa chini watachukuliwa hatua kulingana na Kanuni za fedha zinazohusiana na adhabu (Surcharge and Penalties) za mwaka 2005. Baadhi ya hatua hizo ni pamoja na kuwakata mshahara kati ya asilimia 5 hadi 30 kwa mwezi kulingana na uzito wa kosa waliloshiriki kulitenda na kupendekeza kwa Mamlaka zao za nidhamu, kuvuliwa wadhifa  alionao au kuondolewa dhamana ya kuwa Afisa Masuuli wa fedha za Fungu husika.

 

31.       Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine, Serikali imetoa mwongozo wa ufuatiliaji na tathimini (Monitoring Evatuation) yaani (M&E), na sasa inaandaa Sera ya M&E, na baadae Sheria ya M&E. Mheshimiwa Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania anakerwa sana na udhaifu uliopo katika eneo la M&E serikalini. Eneo hili litaongezewa rasilimali watu na fedha na litapewa malengo yanayopimika. Pamoja na hayo, napendekeza kuanzia mwaka ujao wa fedha taarifa za M&E ziwasilishwe kwenye Baraza la Kazi chini ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

 

32.       Mheshimiwa Spika, Vitendo vya Rushwa vinasababisha utekelezaji wa miradi kuwa chini ya viwango kwa kuwa fedha zilizopangwa kwenda kwenye mradi mingine zinachepushwa na kwenda kwenye mikono ya watumishi wasio wazalendo. Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelikemea vikali jambo hili. Watu wanapanga kuanzia wakati wa maandalizi ya bajeti, wanafuatilia mchakato wote, siku ikipitishwa na Bunge wanakesha wakishangilia bajeti yao imepita, mradi unaposainiwa wanaanza kugawana fedha kabla ya utekelezaji wa mradi. Serikali itaendelea kuimarisha Technical Audit, Value for Money Audit na Real Time Audit katika mwaka ujao wa Fedha. Aidha, Serikali haitawanyima fedha wananchi wa halmashauri yoyote kwa sababu ya hati chafu, wala  haitarudisha fedha kwenye Mfuko Mkuu kwa sababu hazijatumika kutokana na sababu za uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma. Wananchi hawahusiki na hati chafu. Tutawabaini wazembe, Tutawakamata, Tutawashitaki na Tutawafunga.

 

33.       Mheshimiwa Spika, watumishi wa umma ni kiungo muhimu sana katika maendeleo ya nchi. Mikataba yote inaingiwa na watumishi wa umma; ununuzi wowote wa Serikali unafanywa na watumishi wa umma; miradi yote ya Serikali inatekelezwa na watumishi wa umma; na mapato yote yanakusanywa na watumishi wa umma. Wananchi waliwasomesha watumishi wa umma kwa kujinyima, wamewaamini wakusanye na kutumia kodi zao kwa kuwapa huduma. Bado kuna vitendo vingi kwenye utumishi wa umma vinavyopunguza ufanisi katika Taifa lao.  Wage bill yetu ni kubwa kuliko viwango vinavyotakiwa kiuchumi na wakati huo huo ikama hazijatimia na kila mtaa tuna kijana anatafuta kazi. Hii ina maana kuna watu wanalipwa bila kufanya kazi au wanalipwa bila kuwa na ufanisi kazini.

 

34.       Mheshimiwa Spika, imezoeleka kwa mfano Makatibu Wakuu, Manaibu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya, wakurugenzi, wakuu wa taasisi mbalimbali, wakuu wa idara mbalimbali tangu uhuru wakitenguliwa huendelea kulipwa mshahara ule ule sawa na aliyeko kazini mpaka anastafu. Unaweza kukuta nchi ina Wizara 25 ila ina Makatibu Wakuu 50 au zaidi, au Halmashauri 184 lakini kuna wakurugenzi 300 au zaidi na hivyo hivyo kwa nafasi nyingine. Wengine wamesabaisha upotevu na hasara kwa Taifa, wote wanaendelea kuwabebesha mzigo watanzania na wanaziba nafasi ya ajira mpya kwa vijana kwa kulipwa mshahara wa nafasi walizotolewa. Napendekeza yeyote aliyetokea kwenye nafasi yake ya kuteuliwa akitolewa akabaki kwenye utumishi wa umma arejee  pia kwenye mshahara wake wa zamani ili kuwapunguzia watanzania mzigo wa kuwalipa watu waliokaa benchi huku wakiziba nafasi za vijana wapya kuajiriwa. Mambo haya hayavutii lakini lazima tuambizane ukweli. Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anakerwa kuona fedha nyingi zinakwenda kwenye matumizi ya kawaida

 

35.       Mheshimiwa Spika, napendekeza mashirika yote ya umma yenye kufanya kazi kwa misingi ya kibiashara yafanye kazi kwa ufanisi na faida. Yale yasiyofanya kazi kibiashara tutayapima kwa namna wanavyowezesha uchumi kuchangamka na jinsi wanavyoimarisha huduma wanazozitoa kwa jamii. Mashirika mengi ni mzigo kwa Serikali kwa kutegemea ruzuku kutoka serikalini ili yajiendeshe. Kwa nchi zilizoendelea, mapato makubwa ya Serikali yanatoka kwenye mashirika yake ili kuwapunguzia mzigo maskini wa kulipa kodi ili ziendeshe mashirika hayo lakini pia kupunguzia Serikali kutegemea kukusanya fedha kutoka kwa watu maskini. Napendekeza wakuu wote wa mashirika ya umma wafanyiwe usahili kwa ushindani. Napendekeza nafasi zianze kutangazwa  punde nafasi ikiwa wazi ili wenye sifa wajitokeze na wafanyiwe usaili na iwe hivyo hivyo kwa bodi. Wenye sifa ndio wafanyiwe upekuzi kufanyiwa uteuzi na kupewa mkataba wenye malengo yanayopimika. Mashirika na taasisi zingine,  bodi na Menejimenti  zimezidisha urafiki sana na wanaendesha ofisi kirafiki, hakuna uwajibikaji wa kutosha, hii inakiuka misingi ya mashirika kuwa na bodi za wakurugenzi. Hii inasababisha watu wakikabidhiwa shirika la umma wanageuza ni mali yao au  duka.

 

36.       Mheshimiwa Spika, natambua kuna maeneo yatakayogusa sheria na kanuni mbalimbali, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametuelekeza isiwepo sheria yoyote inayotumika kama kikwazo cha kuwaletea watanzania ufanisi. Serikali, itafanyia marekebisho Sheria mbalimbali na kanuni zitakazoguswa na maelekezo ya mheshimiwa Rais yanayolenga kuongeza ufanisi Serikalini. Najua maswala ya udhibiti wa matumizi, udhibiti wa vitendo vya rushwa, udhibiti wa uzembe, udhibiti wa ununuzi usiozingatia thamani ya fedha (value for money) yanagusa maslahi ya watu na yatanifanya niwe unpopular Finance Minister, na hata siku nikitoka kwenye nafasi hii marafiki watakaoona nilikwamisha dili zao potelea mbali watabaki wananchi wa Iramba ambao huwa wanabaki nami hata nikiwa nje ya uwaziri. Mheshimiwa Rais amenielekeza niyafanyie kazi maeneo haya ya mapato na matumizi ya nchi, nami nitayasimamia, nawaomba waheshimiwa wabunge tumuunge mkono mheshimiwa Rais wetu, hii ni nia njema ya kuwakwamua watanzania kwenye umasikini.

 

Sekta za Uzalishaji

37.       Mheshimiwa Spika, kuhusu Sekta za Uzalishaji na Ajira  kwa Vijana, Taifa letu ni Taifa la Vijana, (wastani wa miaka 18). Miaka ya sitini, miaka ya sabini na miaka ya themanini vijana walikuwa wanahudumia wazee na watoto. Njia ilikuwa rahisi kwa wahitimu wakitafutwa wangali masomoni wachague wanataka kwenda kufanya kazi taasisi gani. Hali haiko hivyo sasa. Kwa sasa, wazee ndio wanahudumia vijana na watoto wao. Ni kawaida sasa kukuta mzee wa kijijini au mstaafu akiwahudumia vijana wahitimu. Uwiano huu sio mzuri kwa Taifa letu kuwa na nguvu kazi kubwa ambayo haiko kazini licha ya uwekezaji mkubwa uliowekwa katika sekta za uzalishaji.  Mipango yetu sasa na Sera zetu sasa lazima zijibu mahitaji ya vijana wa Tanzania.

 

Sekta ya Kilimo

38.        Mheshimiwa Spika,  katika kuwekeza kwenye sekta za uzalishaji na zinazotengeneza ajira kwa vijana, Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeongeza bajeti ya Kilimo kutoka shilingi billion 294 hadi shilingi bilioni 954 na itaendelea kuongezeka kila mwaka. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa sekta ya kilimo inakua kwa zaidi ya asilimia 10 ifikapo mwaka 2030. Bajeti ya mwaka 2022/23 ni msingi muhimu kufikia lengo kuu hilo. Malengo mengine ni kujitosheleza kwa mahitaji ya chakula ndani ya nchi na kuuza nje ya nchi, kuongeza thamani ya mauzo ya mazao nje ya nchi kutoka dola za Marekani bilioni 1.2 hadi zaidi ya dola za Marekani bilioni 5 ifikapo mwaka 2030 ili kuongeza uhimilivu wa deni la Taifa. Serikali inakusudia kuongeza mauzo ya Mazao ya Bustani (Horticulture) kutoka dola za Marekani milioni 750 kwa mwaka hadi dola za Marekani bilioni 2 mwaka 2030.

 

39.       Mheshimiwa Spika, ili kupunguza umaskini kwa watanzania, Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan inalenga kutengeneza ajira kwa vijana na wanawake zaidi ya milioni 3 katika sekta ya kilimo  ifikapo mwaka 2025. Hii itafanyika kwa kuongeza eneo la umwagiliaji kufikia hekta 8,500,000, sawa na asilimia 50 ya eneo lote linalolimwa nchini ifikapo 2030. Serikali kupitia Wizara ya Kilimo itatekeleza Schemes ndogo za umwagiliaji kote nchini. Tunataka vijana watoke mjini kuelekea kwenye mashamba ya umwagiliaji kwa kujenga miundombinu ya umwagiliaji ikiwemo ujenzi wa mabwawa ya kuvunia maji ya mvua. Tuna Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika, Ziwa Nyasa na mito mikubwa, kama Malagarasi, Ruvuma, Rufiji, Mara, Pangani, Ruvu nk, haya maji tutayatumia kwenye skimu za Umwagiliaji. Kwa ardhi, maji na watu tulio nao, ni jambo la aibu kwa Tanzania kulia shida ya ngano, shida ya mafuta ya kula kwa sababu ya vita vya Ukraine na Urusi, sisi tunayo fursa ya kuilisha Afrika, Ulaya na Asia katika baadhi ya mazao.

 

40.       Mheshimiwa Spika,  Serikali inakusudia kuongeza idadi ya mashamba makubwa (Block Farms/Commercial Farms) kutoka 110 mwaka 2020 hadi 10,000 mwaka 2030 na kufanya mwelekeo wa uzalishaji wa kilimo kuwa cha kibiashara. Kwa kilimo cha michikichi, tuache kung’ang’ania mchikichi mmoja mmoja kila familia, Mkoa wa Kigoma ndio kitovu cha Michikichi na upanuzi utafuata mikoa ya Tabora, Katavi, Pwani, Geita na Kagera. Wakulima wawezeshwe kuunganisha mashamba ili yawe mashamba makubwa (plantations). Kila mmoja anakuwa mmiliki ili itengenezwe miundombinu ya pamoja. Hivyo ndivyo tunavyoweza kuitikisa dunia. Kwa alizeti hivyo hivyo. Serikali inatarajia kufanya tathmini ya kupunguza au kuhamisha mifugo michache iliyopo katika ranchi ya Kongwa ili hekta karibu elfu 38 zitumike kwa kilimo cha alizeti na kiwanda kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki. Aidha, eneo la Mtanana ambapo huwa tunasumbuka kuweka madaraja pale maji yanapokata barabara tuweke Bwawa kubwa ili bonde lote liwe la “outgrowers” wa alizeti. 

 

41.       Mheshimiwa Spika,  mpaka sasa Tanzania hatujajitosheleza kwa vitu vingi tu ambavyo tuna uwezo wa kuzalisha. Bidhaa nyingi tunazoagiza kutoka nje tuna uwezo wa kuzizalisha hapa, hizo ni ajira za vijana wa kitanzania ambazo tumewapa vijana wa mataifa tunakoagiza bidhaa. Serikali imekusudia kuhakikisha upatikanaji wa malighafi kwenye viwanda vya kuongeza thamani ya mazao na bidhaa za kilimo kufikia asilimia 100 ifikapo 2030, na kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kupitia kilimo cha umwagiliaji kutoka asilimia 10 hadi asilimia 50. Mafuta ya alizeti yale ni mengi tu yakipangwa pembezoni mwa barabara, machungwa, mananasi, ni mengi tu yakipangwa pembezoni mwa barabara, ukiweka viwanda vya masaa 24 kwa siku 7, vya kuwafanya vijana wafanye kazi kwa zamu (shift), viwanda vitawashwa wiki tatu tu, upungufu wote wa malighafi ni ajira za vijana tunazozikosa.

 

Sekta ya Mifugo

42.       Mheshimiwa Spika, idadi ya mifugo hapa nchini ni takriban ng’ombe milioni 35.3; mbuzi milioni 25.6; na kondoo milioni 8.8; kuku milioni 92.8; na nguruwe milioni 3.2. Hata hivyo, mchango wa sekta hii kwenye fedha za kigeni bado mdogo, na mchango wa kubadilisha maisha ya wafugaji bado ni mdogo. Licha ya idadi hiyo ya mifugo, viwanda vyetu vilivyopo Rukwa, Longido, Kibaha, na Mwanza havina malighafi, na wakati huo huo tuna vijana hawana ajira. Sababu kubwa ni utofauti wa malengo kati ya mfugaji na mwenye kiwanda. Malengo ya wafugaji wengi tulionao siyo ya kibiashara, anafuga ili idadi iongezeke, hana mpango na kiwanda. Mheshimiwa Spika, ndugu zangu wa usukumani hata ngombe akivunjika mguu anafungwa POP, hata akiwa na shughuli ya kifamilia hachinji ngombe wa zizini, anakwenda kununua mnadani. Wale wa kwenye zizi wote wana majina, chitamakuwi, maagulya, nshoshawiye na majina ya shangazi, mjomba, bibi, hawachinjwi halafu mwenye kiwanda anaweka kiwanda kutokana na takwimu tu za mifugo katika mkoa huo.

 

43.       Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeongezewa ukomo wa bajeti kwa kiasi cha shilingi bilioni 100. Kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 40 ni za sekta ya mifugo na shilingi bilioni 60 ni za sekta ya uvuvi. Hivyo, bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeongezeka kutoka shilingi 168,252,007,000 hadi kufikia shilingi 268,252,007,000. Kati ya fedha hizo, Shilingi 92,050,824,000 ni kwa ajili ya Sekta ya Mifugo na shilingi 176,201,183,000 ni kwa ajili ya sekta ya uvuvi. Ongezeko hilo la bajeti linalenga kuimarisha sekta ya mifugo ili ufugaji uwe wa kisasa zaidi na wenye tija (modernization). Katika mwaka 2022/2023, Serikali itaimarisha mashamba ya kuzalisha mitamba ya Sao Hill, Kitulo na Mabuki kwa kuyapatia ngombe wazazi na vitendea kazi, ikiwemo matrekta matatu (3) na vifaa vyake. Aidha, Serikali  itanunua madume ya mbegu  366  kwa ajili ya kuboresha mbari za mifugo; na itazalisha mitamba 3,500 na kuisambaza kwa wafugaji. Serikali inakusudia kuongeza uzalishaji wa vyakula ambapo mpaka sasa uzalishaji wa vyakula vya mifugo umeongezeka kutoka tani 1,200,000 mwaka 2020/2021 hadi tani 1,380,000 mwaka 2021/2022.

 

44.       Mheshimiwa Spika, Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM inakusudia kuanzisha vituo nane (8) vya kukuza ujuzi wa vijana (Youth Incubation Center) kwa kuanzia  na wanufaika takriban 1000  kwa ajili ya vijana watakaofanya kazi ya kunenepesha ng’ombe na kuuza kwenye viwanda hivi vinavyokosa malighafi.  Serikali imepanga kutumia mitambo ya kuchimba mabwawa kwa ajili ya wafugaji wadogo wadogo. Aidha, napendekeza Wizara inayohusika na mifugo itunge kanuni za kukusanya na kulinda fedha kwa kila Wilaya kwa makundi ya mifugo yanayozidi mia moja kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu. Mheshimiwa Spika,  Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji zaidi katika viwanda vya kuchakata na kusindika nyama kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi hususani nchi za Mashariki ya Kati ambapo kwa sasa kuna machinjio na viwanda 24 vinavyokidhi vigezo vya kuuza nyama nje ya nchi ambapo vitano kati ya hivyo vimeanza kufanya mauzo nje ya nchi. Viwanda vya kutengeneza bidhaa za ngozi vina uwezo wa kuzalisha jozi 2,855,600 za viatu kwa mwaka. Kwa upande wa maziwa, idadi ya viwanda vya kusindika maziwa nchini imeongezeka kutoka 99 mwaka 2020/2021 vilivyosindika lita milioni 75.9 hadi viwanda 105 mwaka 2021/2022 vilivyosindika lita milioni 77.6 ikiwa ni ongezeko la asimilia 2.3

 

Sekta ya Uvuvi

45.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021, sekta ya uvuvi ilikua kwa asilimia 2.5 na ilichangia asilimia 1.8 kwenye Pato la Taifa.  Aidha, sekta ya uvuvi inatoa ajira kwa watanzania takriban milioni 4.5 katika mnyororo mzima wa thamani ambapo ajira za moja kwa moja kwa wavuvi ni 194,804 na wakuzaji viumbe maji ni 31,998. Serikali imepanga: Kuanza ujenzi wa bandari ya uvuvi katika eneo la Kilwa Masoko - Lindi; ununuzi wa meli mbili (2) za uvuvi katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari; ununuzi wa vifaa vya kuvutia samaki (Fish Aggregate Device - FADs); ununuzi na usambazaji wa boti 250 za kisasa za aina ya fibre kwa vyama vya ushirika wa wavuvi; kuendelea na ufufuaji wa Shirika la Uvuvi Tanzania - TAFICO; kuwajengea uwezo wataalamu wa uvuvi; kuimarisha Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi - FETA; kuimarisha Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania - TAFIRI; kukamilisha ujenzi wa mialo ya kupokelea samaki ya Igabiro, Mbamba Bay na Chifunfu na kujenga masoko sita (6) ya samaki kwenye maeneo mbalimbali ya kimkakati; kukarabati kituo cha ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi cha Bukoba; kununua boti mbili (2) kwa ajili ya utalii wa baharini; ujenzi na ukarabati wa vituo vya ukuzaji viumbe maji; na kuimarisha shughuli za ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya sekta ya uvuvi ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kama ulivyopangwa.

 

Sekta ya Fedha

46.       Mheshimiwa Spika, sekta ya fedha imeendelea kutoa mikopo kwa wafanyabiashara na uchumi. Pamoja na juhudi hizo, kumekuwepo na wafanyabiashara wasiolipa mikopo yao kwa wakati na kupelekea kudhoofisha ustawi wa mabenki na ustawi wa uchumi kwa ujumla. Hadi kufikia Machi 2022, mikopo chechefu ilikuwa asilimia 8.12. Hiki ni kiwango kikubwa sana ikilinganishwa na vigezo vilivyowekwa na Benki Kuu ya Tanzania. Jambo hili linasababishwa na ukopaji usiozingatia kanuni na unaohusisha ukosefu wa weledi na uaminifu wa baadhi ya watumishi wa benki. Unakuta mtu amekopa mabenki zaidi ya matano na kote hajalipa. Akidaiwa anabakia kuonesha ufundi wa kujificha, baadae akichoka kujificha anakimbilia mahakamani. Tuache utapeli unatuchafulia nchi na unapozesha uchumi, "Ukikopa Lipa". Nitoe rai kwa vyombo vya dola na vyombo vya sheria kuwa wakali kwenye utapeli wa aina hii.

47.       Mheshimiwa Spika, niwapongeze sana wanawake, taarifa za kitafiti nilizopewa zinaonesha wanawake wengi wanajitahidi kurejesha mikopo kwa uaminifu. Hata mikopo ya familia kama imekopwa na wanawake, mingi huwa inafanya kazi iliyokusudiwa na hivyo inarejeshwa kwa uaminifu kuliko iliyokopwa na wanaume wengi ambao huwa hawarejeshi. (Niweke sawa, Niliposema wanaume wengi ni ukimwondoa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu). Tujenge utaratibu wa kukopa kwa kuzingatia kanuni, uwezo wa kulipa na tujenge utaratibu wa kurejesha mikopo kwa uaminifu ili kuimarisha sekta ya fedha na kukuza uchumi.  Kwa upande mwingine, wako baadhi ya watumishi wa mabenki wasio waaminifu kwa kushirikikiana na madalali wao wanapenda kutamani dhamana za wateja wao na kutafuta wateja wa kununua dhamana za wateja wangali wameshalipa zaidi ya asilimia tisini ya deni. Tena wanauza dhamana kwa kiwango cha chini ukilinganisha na thamani ya dhamana iliyowekwa. Jambo hili linawatia umaskini watanzania. Nitoe rai kwa vyombo vya ulinzi na usalama kufuatilia kwa karibu kila inapofanyika minada kwa madalali wa dhamana na bandarini.

 

 

Sekta ya Nishati

48.       Mheshimiwa Spika, mafanikio tuliyoyapata katika sekta ya nishati ni pamoja na kuendelea kutekeleza: Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere - MW 2,115 ambapo hadi Aprili 2022 utekelezaji umefikia asilimia 60.22; miradi ya Kupeleka Umeme Vijijini - REA; mradi wa ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline - EACOP) kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania; na mradi wa kusindika na kuongeza kasi ya usambazaji gesi asilia. Aidha, Serikali imeendelea kuwashirikisha wazawa ambapo shughuli za uendeshaji wa mitambo ya uchakataji, usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia unafanywa na watanzania.

49.       Mheshimiwa Spika, katika sekta ya nishati, Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme. Kwa mwaka 2022/23, Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM itaendelea na utekelezaji wa mradi mkubwa wa Kuimarisha Gridi ya Taifa  (National Grid Stabilization Project) kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini pamoja na kutekeleza miradi ya nishati vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Miradi mingine itakayotekelezwa inahusisha Ruhudji (MW 358), Kinyerezi I - Extension (MW 185), Rusumo (MW 80) na Kikonge (MW 300). Aidha, Serikali itaendelea kujenga njia za mzunguko pete (ring circuit) ili kuzuia upotevu wa umeme kwa kuwezesha umeme kupita njia mbadala pale miundombinu inapopata hitilafu. Miradi ya njia ya umeme wa msongo itakayoendelea kutekelezwa ni pamoja na kV 400 Rufiji - Chalinze - Dodoma na Chalinze - Kinyerezi; kV 400 Singida - Arusha - Namanga; kV 400 North - West Grid Extension (Iringa - Mbeya - Sumbawanga - Mpanda - Kigoma - Nyakanazi); pamoja na kujenga miundombinu ya umeme kwa ajili ya SGR.

 

50.       Mheshimiwa Spika, Serikali itakamilisha uunganishaji wa mikoa miwili yaani Kigoma na Katavi kwenye Gridi ya Taifa.  Mradi wa Nyakanazi – Kakonko – Kasulu - Kigoma KV33 unaojengwa na Mkandarasi Sinotech, Mradi wa Nyakanazi - Kigoma KV 400 Mkandarasi yuko site kwa gharama ya dola za Marekani milioni 168, fedha zipo! Kadhalika mradi wa kufua umeme wa Malagarasi mw 49.5 fedha tayari zipo kwa ajili ya mradi huo. Serikali itaendelea na miradi mikubwa miwili pia ya kuunganisha umeme kutokea Sumbawanga – Katavi - Kigoma na ule wa Tabora – Katavi - Kigoma. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mkoa wa Katavi, tayari mkandarasi yuko site ukianza na ujenzi wa sub station Ipole Sikonge, Inyonga wenye thamani ya bilion 124. Napenda niwahakikishie wananchi wa mikoa hiyo kuwa umeme wa Grid ya Taifa utafika kama alivyoeleza Waziri wa Nishati. Wabunge wa Kigoma na wabunge wa Katavi mliokuja kuweka kambi Wizara ya Fedha na Mipango mkifuatilia ahadi ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, mtarudi mikoani kwenu mkiwa mashujaa na mtatembea kifuambele.

 

Ujenzi na Uchukuzi

51.       Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa - SGR kwa kipande cha Dar es Salaam - Morogoro (km 300) umefikia asilimia 96.54; na kipande cha Morogoro - Makutupora (km 422) asilimia 85.02. Aidha, Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa SGR kwa kipande cha tatu cha kutoka Makutopora mpaka Tabora (km 368) wenye thamani ya shilingi trilioni 4.4. Serikali iko katika hatua za mwisho ya kusaini mktaba wa kipande cha Tabora - Isaka (km 163) (dola za Marekani milioni 695.7). Serikali imeanza mchakato wa kutafuta mkandarasi kwa kipande cha Tabora - Kigoma km 514 (dola za Marekani bilioni 2.1) na kipande cha Uvinza – Malagarasi – Msongati – Gitega - Kindu (DRC)

 

52.       Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa jumla ya kilometa 216.26 za barabara kuu na kilometa 34.8 za barabara za mikoa kwa kiwango cha lami. Aidha, kilometa 307.41 za barabara za mikoa zilikarabatiwa kwa kiwango cha changarawe. Vilevile, Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje - Outer Ring Road (km 112.3) katika Jiji la Dodoma pamoja na kuendelea na upanuzi wa njia nane wa barabara ya Kimara - Kibaha (km 19.2). Kadhalika, Serikali imekamilisha ujenzi wa madaraja ya Tanzanite (Dar es Salaam), Kiyegeya (Morogoro), na Ruhuhu (Ruvuma) na kuendelea na ujenzi wa madaraja ikijumuisha daraja la J.P Magufuli (Kigongo - Busisi, Mwanza) ambalo ujenzi umefikia asilimia 40.2, Kitengule, Kagera (asilimia 90) na Wami, Pwani (asilimia 72.9). Serikali pia imeendelea na ukarabati wa viwanja vya ndege vya Songea, Mtwara, Iringa, Musoma na Songwe.

 

53.       Mheshimiwa Spika, Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM itaweka msisitizo katika ujenzi wa barabara za kufungua fursa za kiuchumi na zile za kuunganisha Tanzania na nchi jirani kwa utaratibu wa EPC + F ikiwemo  (1) barabara za Kidatu - Ifakara - Lupilo - Malinyi - Londo - Lumecha (Songea), (km 499); (2) Handeni - Kibirashi - Kibaya - Kwa Mtoro - Singida (km 460); (3) Karatu - Mbulu - Haydom - Sibiti River - Lalago - Maswa (Simiyu) (km 389);  (4) Daraja la Juu la Magomeni-Jangwani-Fire-Bibi Titi (5) Kibaha - Mlandizi - Chalinze - Morogoro Expressway (km 158); (6) Igawa - Songwe - Tunduma (Expressway) (km 218.0), ambazo zitawekewa road toll pamoja na daraja la Tanzanite kwa kuwa lina sifa zote za kufanya hivyo. Serikali itamalizia barabara zinazounganisha Mikoa ambayo wakandarasi wako kazini ikiwepo Tabora - Kigoma na Nyakanazi - Kigoma na  kuweka kipaumbele kwenye kujenga barabara muhimu za kiuchumi kama Barabara ya Makongorosi-Itigi - Mokiwa, Mafinga-Mtwango-Nyololo - Mgololo, Kahama -Nyang – wale - Geita  na nyinginezo. 

 

54.       Mheshimiwa Spika, Serikali ya awamu ya sita imeonesha dhamira ya dhati ya kuboresha bandari ili kurahisisha shughuli za kiuchumi za usafirishaji kwa njia ya maji na uvuvi katika kina kirefu cha bahari. Katika kufanikisha hilo, Serikali imendelea na miradi ya ujenzi, upanuzi na ukarabati wa miundombinu ya bandari zilizopo katika ukanda wa Bahari ya Hindi. Miradi hiyo ni pamoja na: kukamilika kwa ujenzi wa gati maalumu la kuhudumia meli za magari (RoRo), yadi ya kuhudumia makasha pamoja na kuboresha gati namba 1 - 7 katika Bandari ya Dar es Salaam; kusainiwa kwa mkataba na mkandarasi China Harbour Engineering Co. Ltd kwa ajili ya ujenzi wa bandari ya Uvuvi, Kilwa Masoko - Lindi; kukamilika kwa ujenzi wa gati moja lenye urefu wa mita 300; kuendelea na ujenzi wa uzio na sakafu ngumu katika eneo la mita za mraba 75,807 katika Bandari ya Mtwara; na kukamilika kwa uongezaji wa kina kwenye lango la kuingia meli kutoka mita nne (4) hadi mita 13 pamoja na kuweka vifaa vya kuongoza meli katika Bandari ya Tanga. Aidha, Serikali inaendelea na majadiliano na wawekezaji watakaowekeza kwenye Eneo Maalum la Uwekezaji Bagamoyo hususani katika miradi ya msingi mitatu (3) ambayo ni: Bandari ya kisasa (Modern Seaport Component); Sehemu ya Kanda Maalum kwa ajili ya mizigo na usafirishaji (Logistics Park); na Sehemu ya Mji wa Viwanda (Port side Industrial City).

 

55.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali ilikamilisha ujenzi wa chelezo cha kujengea na kukarabati meli katika Bandari ya Mwanza pamoja na ukarabati wa meli za New Butiama Hapa Kazi Tu na New Victoria Hapa Kazi Tu. Aidha, serikali imeendelea na ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza Hapa kazi Tu yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo, ambapo ujenzi umefikia asilimia 66. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali inatarajia kujenga meli mpya: moja (1) katika Ziwa Victoria; mbili (2) katika Ziwa Tanganyika; na moja katika Bahari ya Hindi. Aidha, Serikali itaendelea na ujenzi wa meli ya MV. Mwanza katika ziwa Victoria pamoja na ukarabati wa Meli za MV Umoja, MT Sangara, MV Liemba - Ukerewe, MT. Nyangumi na boti moja (1) ya mwendokasi (Sea Warrios) - Ziwa Tanganyika. Aidha, Serikali itafanya ukaguzi wa kina wa Meli ya MV Mwongozo katika Ziwa Tanganyika pamoja na kuendelea kufungua mifumo ya TEHAMA katika vituo vya Maziwa makuu (Victoria, Tanganyika na Nyasa).

 

56.       Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa kuboresha Shirika la Ndege Tanzania ambapo katika kipindi cha mwaka 2021/22 Serikali imepokea ndege tatu (3). Kati ya hizo, ndege mbili (2) ni aina ya Airbus A220  300 na ndege moja ni aina ya Dash 8 Q400. Vilevile, Serikali imefanya malipo ya awali ya ununuzi wa ndege mpya tano (5) ambazo ni ndege mbili (2) aina ya Boeing 737-9, ndege moja (1) aina ya De Havilland Dash 8-Q400, ndege moja (1) aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, na ndege moja (1) ya mizigo aina ya Boeing 767-300F. 

57.       Mheshimiwa Spika, uboreshaji wa viwanja vya ndege unaendelea katika maeneo mbalimbali nchini. Katika kutekeleza hilo, Serikali imesaini mkataba kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato awamu ya kwanza itakayohusisha ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege pamoja na jengo la abiria. Aidha, Serikali imekamilisha upanuzi wa njia ya kutua na kuruka ndege na kufungwa kwa mfumo wa kuongoza ndege katika Kiwanja cha Ndege cha Dodoma; pamoja na usanifu na kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Mwanza. Viwanja vinavyoendelea kufanyiwa ukarabati na ujenzi ni viwanja vya ndege vya Songea (asilimia 96), Mtwara (asilimia 89), Iringa (asilimia 44.65), Songwe (asilimia 95) na Musoma (asilimia 10). Vilevile, Serikali inaendelea kufanya maandalizi ya ujenzi na upanuzi wa viwanja vya ndege vya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Sumbawanga vitakavyogharimu Euro milioni 50 sawa na shilingi bilioni 136.85.

 

Elimu, Sayansi na Teknolojia

58.       Mheshimiwa Spika, Serikali imewezesha ujenzi wa madarasa 15,000 katika shule za sekondari na vituo shikizi na mabweni 50 kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum. Ujenzi wa miundombinu hii umewezesha wanafunzi wote 907,803 waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2021 kupata nafasi ya kuanza kidato cha kwanza Januari 2022 bila kusubiri chaguo la pili. Kadhalika, Serikali imekamilisha maboma 560 ya vyumba vya madarasa katika shule za sekondari kutokana na tozo za miamala ya simu ambapo shilingi bilioni 7.0 zilitolewa; Aidha, Serikali imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 569 kwa wanafunzi 177,777 wa elimu ya juu.

59.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23 Serikali itaenda kutekeleza mradi wa “Higher Education for Economic Transformation” (HEET) wenye thamani ya dola za Marekani milioni 425. Mradi huu utahusisha ujenzi wa miundombinu katika vyuo vikuu mama na katika mikoa kadhaa ambayo haina vyuo vikuu ikiwemo Lindi, Kagera, Rukwa, Katavi, Manyara na kukamilisha ujenzi wa Institute of Marine Science Zanzibar na kujenga chuo kipya cha TEHAMA Dodoma.

 

60.       Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kugharamia programu ya elimumsingi bila ada ambapo hadi Aprili 2022, jumla ya shilingi bilioni 244.5 zilitolewa. Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM ameguswa sana na watoto kukatisha masomo kwa ajili ya sababu mbalimbali. Miongoni mwa sababu zinazosababisha kukatisha masomo ni umaskini wa kipato kwenye familia zetu, mimba za utotoni, mwamko duni wa elimu kwa baadhi ya jamii na utoro na wale wasioendelea kufuatana kwa mujibu wa sheria (Ufaulu).  Ili kukabiliana  na utoro (drop out) wa wanafunzi wanaotoka familia maskini, bado tuna watoto wanaoshindwa kumudu mahitaji ya lazima licha ya kuwepo kwa programu ya elimu bila malipo  na hivyo wanasaidiwa na wabunge, madiwani na wengine kuchangiwa na wasamaria wema. Napendekeza kuanzisha dirisha maalum  (Special Fund) kupitia TASAF itakayosaidia watoto wanaotokea familia maskini. Kwa msingi huo napendekeza kuanza na bilion 8 kwa ajili ya watoto masikini watakaopatikana kwenye database ya TASAF na taarifa za wabunge na madiwani.

 

61.       Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na mimba za utotoni, Serikali itaendelea kujenga mabweni kwenye maeneo hatari kwa watoto wa kike. Aidha, ili kutoa fursa kwa watoto wasioendelea na vidato na vyuo, Serikali itaendelea kuimarisha elimu ya ufundi hususan katika vyuo vya kati kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kujiajiri ama kuajiriwa. Mpaka sasa Wilaya 77 zina vyuo vya Ufundi VETA kati ya Wilaya 138 nchini kote. Tuna mikoa 25 ina Vyuo vya Ufundi kati ya mikoa 26. Bado mkoa wa Songwe hauna kabisa Chuo cha VETA  na wabunge wa mkoa wa Songwe wamekuwa wakishinda Ofisini wakifuatilia ahadi waliopewa na Mheshimiwa Rais. Bado kuna wilaya 36  ambazo hazina vyuo wala vyuo vya Mkoa. Napendekeza kutoa bilioni 100 kwa ajili ya ujezi wa vyuo vya ufundi kwa Mkoa wa Songwe na wilaya 36 ambazo hazina vyuo ili kufanya wilaya zote 138 kuwa na chuo cha Ufundi (VETA). Waheshimiwa wabunge, Huyo ndio SAMIA.

62.       Mheshimiwa Spika, kwa sasa wanafunzi wa kidato cha tano ni takriban 90,825 na kidato cha sita ni 56,880. Mahitaji ya fedha ni shilingi 10,339,350,000. Ili kuwapunguzia gharama watoto hao kama Mheshimiwa Rais alivyoielekeza Wizara, napendekeza kufuta ADA kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita. Kwa hatua hiyo, Elimu bila Ada ni kuanzia shule za msingi mpaka kidato cha sita. Serikali itajipanga kuangalia namna ya kusaidia vyuo vya kati kadiri hali ya uchumi itakavyotengemaa. Nani kama SAMIA? Nani kama Mama? Nani kama CCM? CCM ni Na. 1. 

 

Sekta ya Afya

63.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali imewezesha ujenzi, upanuzi na ukarabati wa miundombinu ya afya ikiwemo: majengo 66 ya wagonjwa mahututi - ICUs; majengo 100 ya dharura - EMDs; nyumba 150 kwa ajili ya watumishi wa Afya; Hospitali za Rufaa za Mikoa 7 na hospitali maalum 1 (Mirembe); na vituo vya Afya 304 ili kuboresha huduma ya mama na mtoto. Aidha, Serikali imetoa ruzuku ya shilingi bilioni 23.32 kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kukamilisha ujenzi wa maboma 564 ya zahanati. Serikali pia imeendelea na ujenzi wa hospitali 99 na kuanza ujenzi wa hospitali mpya 28. Vilevile, Serikali imewezesha ujenzi wa vituo vya afya 234 kwa kutumia tozo ya miamala ya simu yenye thamani ya shilingi bilioni 86.0.

 

64.       Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuimarisha huduma za afya kwa kuboresha huduma za uchunguzi wa magonjwa ambapo hadi sasa katika hospitali zetu mbalimbali kuna jumla ya mashine 11 za CT scan, mashine 7 za MRI na mashine 105 za digital X Ray zinazofanya kazi.  Kati ya hizo, mashine 42 za digital X Ray zipo katika hospitali za ngazi ya taifa, kanda na maalumu na rufaa za mikoa na mashine 63 zipo katika hospitali zilizo chini ya OR-TAMISEMI.  Serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika eneo hili ambapo ununuzi zaidi wa vifaa vya uchunguzi wa magonjwa umekamilika na vifaa hivyo vitasimikwa katika hospitali na taasisi zetu mbalimbali.  Vifaa ambavyo vimeshaagizwa  ni pamoja na, MRI 4; CT “Scan 31; Digital X Rays” 130; mini angio suite moja na “Echo Cardiography” 7. Aidha, Serikali inaendelea na usimikaji wa vinu ya kuzalisha na kujaza hewa tiba ya oksijeni ambapo hadi sasa vinu 13 vimesimikwa katika hospitali zetu mbalimbali na hivyo kusogeza huduma za kitabibu kwa wananchi.

 

65.       Mheshimiwa Spika, Serikali ya CCM inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM itaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kujenga, kukarabati na kupanua miundombinu ya kutolea huduma za afya ikiwemo: Ujenzi wa Hospitali Maalum ya Mama na Mtoto Jijini Dodoma; kuanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Magharibi; kukamilisha ujenzi wa Hospitali (5) za Rufaa za Mikoa katika Mikoa mipya ya Katavi, Geita, Njombe, Songwe na Simiyu; na kukamilisha upanuzi wa hospitali nane (8) za Rufaa za Mikoa. Aidha, Serikali itaendelea kuboresha huduma za matibabu ya ubingwa bobezi katika Hospitali ya Taifa na Kanda kwa kuimarisha miundombinu na ununuzi wa vifaa na vifaa tiba katika Taasisi ya JKCI, Hospitali za Rufaa za Kanda za Chato, Mtwara, KCMC, Bugando na Mbeya.

 

Sekta ya Maji

66.       Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wetu amewezesha kukamilika kwa miradi 303 ya maji vijijini na miradi 40 mijini ikiwemo miradi mikubwa ya Misungwi, Orkesumet, Chalinze-Mboga na Longido; kuongezeka kwa kiwango cha upatikanaji wa huduma za maji nchini kutoka asilimia 72.3 vijijini na 86 mijini mwaka 2020/21 hadi asilimia 74.5 vijijini na 86.5 mijini; kuimarika kwa usimamizi wa rasilimali ya maji kwa kuendelea kutambua, kuweka mipaka na kuhifadhi vyanzo 178 vya maji pamoja na kuandaliwa kwa mipango ya utunzaji wa maeneo ya vidakio vya maji katika mabonde yote nchini.

67.       Mheshimiwa Spika, Serikali pia imekamilisha taratibu za ununuzi wa seti 25 za mitambo ya kuchimba visima ambayo itasambazwa kwa kila mkoa isipokuwa Dar es Salaam; seti 5 za mitambo ya ujenzi wa mabwawa ambazo zitapelekwa kwenye kila kanda; na seti 4 za vifaa vya utafiti wa maji chini ya ardhi. Mitambo hii inatarajiwa kupokelewa mwishoni mwa mwezi Juni, 2022. Aidha, mnamo tarehe 6 Juni 2022, Serikali ilisaini mikataba ya kusambaza maji kwa miji 28, ambazo ni fedha za mkopo wenye thamani ya dola za Marekani milioni 500 kutoka Exim bank - India. Kati ya fedha hizi, dola milioni 35 zitatekeleza miradi ya maji Zanzibar.

 

Sekta ya Mali Asili na Utalii

68.       Mheshimiwa Spika, Aprili mwaka huu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alizindua filamu ya The Royal Tour” ambayo imelenga kuonesha uwezo na fursa zilizopo Tanzania katika sekta ya utalii na uwekezaji. Hivyo, kupitia Bunge hili, napenda kuendelea kuwakaribisha diaspora wa Tanzania na wawekezaji kutoka kona zote za dunia kuja kutalii na kuwekeza katika fursa za uwekezaji zilizopo nchini kwani Tanzania tuna “JAMBO LETU” kwenye kuinawirisha sekta binafsi katika uwekezaji. Tumejipanga na kujizatiti kuifanya Tanzania kuwa KITOVU na MFANO” wa sehemu ya uwekezaji salama, haraka, rahisi, wenye tija na manufaa kwa pande zote. Kufuatia ziara hiyo kwenye kanda za utalii Tanzania, tayari booking zimejaa mpaka Desemba 2022 kwenye maeneo mengi. Naomba kutoa wito kwa wawekezaji wote kuwa, Tanzania kumenoga, milango iko wazi, njooni muwekeze kwa maslahi mapana ya pande zote.

 

 Sekta ya Madini

69.       Mheshimiwa Spika, chini ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita, mchango wa sekta ya madini umeongezeka kutoka asilimia 6.7 mwaka 2020 hadi asilimia 7.2 mwaka 2021 ambapo ukuaji huu uliifanya sekta hii kushika nafasi ya tano miongoni mwa sekta nyingine za kiuchumi nchini. Aidha, kasi ya kukua kwa shughuli za madini hapa nchini imekuwa ikiendelea kuongezeka ambapo katika mwaka 2021, sekta ya madini ilikua kwa asilimia 9.6 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 6.7 mwaka 2020, na hivyo kuwa ya tatu miongoni mwa sekta nyingine kwa kiwango cha ukuaji katika kipindi hicho. Mwenendo huu wa ukuaji wa sekta umetokana na ongezeko la uwekezaji uliofanyika kupitia uchimbaji mkubwa, wa kati na mdogo nchini. Lengo la Serikali ni kuona sekta ya madini inachangia asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025 kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025.

 

70.       Mheshimiwa Spika, kwa upande wa wachimbaji wadogo kushiriki uchumi wa madini, Serikali imezihamasisha taasisi za fedha na benki nchini kutoa mikopo kwa wachimbaji hao ili kuwawezesha kukua na kufanya uchimbaji wenye tija. Baadhi ya benki ikiwemo NMB, NBC, CRDB na KCB zimeridhia na kuanza kutoa mikopo ambapo jumla ya shilingi bilioni 36 zimekopeshwa kwa wachimbaji hao. Hizi ni miongoni mwa juhudi ambazo Serikali imezifanya ili kuhakikisha wachimbaji wadogo wanakua na kufikia  hadhi ya kiwango cha kati na hatimaye wakubwa, wanashiriki uchumi wa madini na kuchangia katika Pato la Taifa. Aidha, kufuatia Serikali kuendelea kuwawezesha wachimbaji wadogo, mchango wao katika maduhuli ya Serikali umeongezeka hadi kufikia takriban asilimia 40 ya maduhuli yote. Kutokana na mchango wao, Serikali itaendelea kuwawezesha ili waendelee kuchangia zaidi katika uchumi wa Taifa.

 

71.       Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia Tanzania - GST imeweza kufanikisha ugani wa jiolojia kwa asilimia 96 ya nchi nzima, ugani wa jiofizikia kwa skeli ndogo (Low Resolution) asilimia 100 na skeli kubwa (High Resolution) asilimia 16 na ugani wa jiokemia asilimia 25 ya nchi nzima. Kupitia tafiti hizo Serikali imefanikiwa kugundua maeneo mapya yenye rasilimali madini na kuyatangaza kwa lengo la kuvutia uwekezaji mkubwa. Baadhi ya rasilimali zilizogunduliwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita ni pamoja na dhahabu (Malinyi - Morogoro na Liwale - Lindi), gesi ya helium (Masware - Babati na Ziwa Natroni - Arusha), chokaa na feldispa (Kiteto - manyara), chokaa (Mkalama - Singida).

 

72.       Mheshimiwa Spika, migodi mikubwa iliyopo kama GGML, Bulyanhulu North Mara na mgodi mpya wa Kabanga Nikeli na Nyanzaga imetokana na taarifa za awali za jiolojia zilizofanywa na GST miaka ya nyuma. Kutokana na mafanikio hayo, Serikali itaendelea kuiwezesha GST ili iweze kufanya utafiti zaidi wa jiofizikia kwa skeli kubwa (High Resolution) kwa lengo la kufikia asilimia 65 kutoka asilimia 16 iliyopo sasa. Manufaa yanayotarajiwa ni pamoja na; Uwezekano wa kuanzishwa kwa migodi mipya ambayo itachangia Pato la Taifa kupitia sekta ya madini; ukuaji wa sekta mtambuka ambazo hutegemea sana sekta ya madini kama vile kilimo, ujenzi na maji; uanzishwaji wa viwanda vinavyotegemea upatikanaji wa malighafi za madini kama vile viwanda vya saruji, mbolea na marumaru; na kuongezeka kwa ufahamu zaidi wa jiolojia ya nchi na hivyo kuchochea shughuli za utafiti na uchimbaji wa madini ambao utachangia katika maendeleo ya Taifa.

 

73.       Mheshimiwa Spika, kila mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi. Ili kutimiza amza hiyo, Serikali inakusudia kutoa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) kwa kila mtanzania mwenye umri wa kuanzia miaka 18 au zaidi. Kwa kuwa utaratibu wa usajili wa namba ya utambulisho wa Taifa (NIDA) unamtaka kila mwananchi mwenye umri wa miaka 18 au zaidi kujisajili NIDA, napendekeza kuwa wale wote wenye NIDA kwa sasa (wanaofikia milioni 19 nchi nzima) wapatiwe namba ya TIN na itumike kwenye miamala yote inayofanyika katika ununuzi na mauzo yanayofanyika ndani ya nchi. Kila mwenye namba ya mlipakodi atapata makadirio yake kwa njia ya simu na kulipa kodi husika kwa njia ya mtandao.

 

74.       Mheshimiwa Spika, vijana wetu wa bodaboda wanapata shida kufuata leseni yalipo makao makuu ya mkoa, yaani mtu atoke Mererani kwenda Babati makao mkuu ya mkoa wa Manyara, atoke Kakonko kufuata leseni Kigoma, atoke Wilaya ya mwisho kule mpakani na Lindi, Mtwara na Ruvuma kufuata leseni Morogoro ili hali taarifa zake zote ziko kwenye kitambulisho cha NIDA. Napendekeza taarifa zilizopo kwenye kitambulisho zitumike kutengeneza leseni, akishakufuzu ajiandikishe atoe namba yake ya NIDA, TRA na Jeshi la Polisi wafanye kazi ya kuoanisha taarifa na wamtumie mhusika leseni yake kwa simu. Aidha, napendekeza wananchi wote wenye namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) wapeleke ritani za kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa mwaka mara moja. Utaratibu huu utachachua utamaduni wa kulipa kodi miongoni mwa Watanzania na hivyo kuiongezea Serikali mapato yatokanayo na sekta ambazo hazichangii kwenye makusanyo ya Serikali kwa sasa licha ya kuwa na mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa kama vile sekta za mifugo, kilimo, uvuvi na nyinginezo.

 

 Bunge

75.       Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uzito wa majukumu ya Bunge na hivyo itaendelea kuhakikisha kwamba Bunge linawezeshwa kifedha na kujengewa uwezo ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake ya msingi ya kutunga sheria, kushauri na kusimamia Serikali. Kwa kulitambua hilo, katika mwaka wa fedha 2022/23, Bunge limeongezewa kiasi cha shilingi bilioni 5 kwa ajili ya matumizi mengineyo ili kuwezesha  utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo kuwajengea uwezo wabunge ili waweze kuisimamia vizuri Serikali. Serikali pia imeongeza bajeti ya mfuko wa Jimbo ili kuwawezesha wabunge kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kuchochea maendeleo katika majimbo yao. Serikali itahakikisha kuwa fedha kwa ajili ya shughuli za Bunge zinatolewa kwa wakati. Aidha, Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa Bunge lako Tukufu kwa kulipatia taarifa zote muhimu zinazohitajika na kwa wakati ikiwepo taarifa za kila robo mwaka za kitengo cha Tathmini na Ufuatiliaji ili ziwasaidie wabunge wanapofanya ziara za kukagua miradi kama nilivyopendekeza awali.

 

Utawala Bora

76.       Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mahakama, Serikali itaendelea kuimarisha usimamizi wa mifumo ya haki na utoaji haki kwa kuendelea kuwezesha mhimili wa Mahakama kuongeza kasi ya kusikiliza mashauri na hivyo kupunguza mrundikano wa mashauri mahakamani. Aidha, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya utoaji haki kupitia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya mahakama ikiwa ni pamoja na kuimarisha matumizi ya TEHAMA hususan mfumo wa mkutano mtandao na mfumo wa kielektroniki wa usimamizi na uendeshaji wa mashauri. Utekelezaji wa masuala haya unalenga kuboresha ufanisi wa mahakama na kufanya usimamizi wa mahakama kuwa wa kisasa zaidi na hivyo kuwawezesha wananchi kupata haki sawa na kwa wakati.

 

77.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali itaendelea kugharamia utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali zinazolenga katika utoaji haki kwa wananchi na kupambana na rushwa. Shughuli zitakazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa vituo jumuishi vya utoaji haki na kutafsiri sheria ambapo kiasi cha shilingi bilioni 5.7 zimeongezwa kwenye bajeti ya awali.  Aidha, Serikali imeongeza kiasi cha shilingi bilioni 20 kwenye bajeti ya Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali kwa ajili kugharamia mashahidi wa makosa ya jinai na ujenzi wa vituo jumuishi vya utoaji haki.

 

Ulinzi na Usalama

78.       Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali kupitia majeshi yetu imeendelea kudumisha amani na usalama nchini na hivyo kuwezesha watanzania kutembea kifua mbele na kutekeleza shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi bila wasiwasi. Aidha, Serikali imeendelea kuimarisha ushirikiano wa kiulinzi na kijeshi na nchi mbalimbali na tunaamini kuwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vitaendelea kutimiza wajibu wake wa kulinda mipaka na amani ya nchi yetu kwa moyo wa kizalendo na hivyo kuzidi kuimarisha mazingira ya amani na utulivu ya kuvutia biashara na uwekezaji. Katika mwaka 2022/23, Serikali itaendelea kuviimarisha na kuvijengea uwezo vyombo vya ulinzi na usalama ili kuendelea kutekeleza wajibu wake kwa weledi na uzalendo.

79.       Mheshimiwa Spika, sambamba na zoezi la anuani za makazi linaloendelea, Serikali itaimarisha shughuli za usalama ngazi ya kaya ili kujidhatiti na aina mpya ya uhalifu ambao tumeusikia kwa baadhi ya majirani zetu. Utaratibu huo ni pamoja na kuhakikisha viongozi wa mitaa na shehia wanahusika kwenye upangishaji wa nyumba za kuishi ili kila nyumba ya kupanga itumie mkataba wa Serikali ya vijiji/mitaa uliopigwa muhuri wa ofisi ya vijiji/mitaa husika. Kadhalika, mauziano ya mali zisizohamishika lazima zihusishe uongozi wa Serikali husika hata kama wahusika wana mawakili binafsi ila viongozi wa serikali za vijiji/mitaa wawe na taarifa za mambo yanayoendelea katika maeneo yao.

 

Uhusiano wetu na Washirika wa Maendeleo

80.       Mheshimiwa Spika, jitihada za kuimarisha ushirikiano na Washirika wa Maendeleo pamoja na mataifa mbalimbali duniani zinazofanywa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, zimewezesha kusainiwa kwa mikataba ya misaada na mikopo mbalimbali. Baadhi ya mikataba ya miradi iliyosainiwa ni pamoja na:  Uboreshaji wa Umiliki wa Ardhi; kuboresha Elimu ya Msingi; na mradi wa Maboresho ya Mahakama ili kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi. Aidha, baadhi ya mikataba ya miradi inayotarajiwa kusainiwa ni pamoja na: Mradi wa Kufungamanisha Uchukuzi ambao una lengo la kuboresha na kuunganisha njia kuu za barabara na viwanja vya ndege vya mikoa (TanTIP); na Mpango Kabambe wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu - TSMP II.

 

81.       Mheshimiwa Spika, Serikali inakamilisha majadiliano ya upatikanaji wa mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia wenye thamani ya dola za Marekani milioni 500, sawa na shilingi bilioni 1,167. Aidha, Serikali imefikia makubaliano ya kupata mkopo nafuu wenye thamani ya shilingi bilioni 2,567, sawa na dola za Marekani bilioni 1.1 kupitia dirisha la Extended Credit Facility (ECF) chini ya Shirika la Fedha la Kimataifa - IMF. Mkopo huo wa IMF utatolewa kwa awamu saba katika kipindi cha miezi 40 kuanzia Julai 2022 hadi Julai 2025. Fedha hizo zitaelekezwa katika kuimarisha sekta za uzalishaji, huduma za jamii pamoja na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji na kuinua sekta zilizoathiriwa na vita ya Ukraine na Urusi.

 

Maslahi ya Watumishi wa Umma na Wastaafu

82.       Mheshimiwa Spika, tuzo ya watumishi wachapakazi na wazalendo ni ipi? Matunda ya utumishi wa kujitoa na uadilifu wa watumishi hao ni yapi? Lakini Je, ni nani wa kuyatambua na kuyapa thamani halisi mambo hayo? Sauti zenye maswali haya zilitawala masikio ya Mheshimiwa Mama yetu mwenye usikivu, unyenyekevu na anayejali, na hatimaye maswali haya yamejibiwa na kalamu yenye mamlaka ya Mheshimiwa Rais wetu kwa kuridhia nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kwa asilimia 23.3 kwa watumishi wa umma. Kwa kuendelea kuonesha kujali na kuthamini utumishi wa umma, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM amefanya maboresho kwenye viwango vya posho. Aaminie katika wema na kujali, hutenda na kuuishi wema. Hivyo, Mheshimiwa Rais wetu ni mfano sahihi wa maneno haya katika jambo hili. Watumishi wa Umma wanauliza Nani kama Mama Samia? na wanasema Asante sana Mama!

 

83.       Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na jitihada za kulipa madai ya Watumishi wa Umma pamoja na kupandisha madaraja watumishi wanaostahili. Tutaendelea kuboresha mazingira ya kazi na maslahi yao kadri uchumi wa nchi utakavyoruhusu bila kuathiri makundi mengine ya wananchi, huduma mbalimbali pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Katika kuhakikisha maslahi ya wastaafu wetu waliotumikia Taifa hili kwa uzalendo, uadilifu na bidii kubwa wananufaika na michango waliyochangia katika mifuko ya hifadhi ya jamii, Serikali sikivu ya Mama yetu imeridhia kuongeza malipo ya mkupuo kwa wastaafu kufikia asilimia 33 badala ya asilimia 25 iliyopendekezwa mwaka 2018.

 

84.       Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na mikakati mbalimbali ya kulipa madeni ya mifuko ya hifadhi ya jamii. Katika mwaka 2021/22, Serikali ilitoa hatifungani maalumu yenye thamani ya shilingi trilioni 2.18 kwa ajili ya kulipa deni la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma - PSSSF linalohusu michango ya watumishi waliokuwa kwenye utumishi kabla ya mwaka 1999. Mwaka 2022/23, Serikali itaendelea na uhakiki wa madeni ya mifuko ya hifadhi ya jamii na kulipa deni stahiki. Lengo ni kuhakikisha watumishi wanalipwa kwa wakati mafao yao mara baada ya kustaafu pamoja na pensheni zao za kila mwezi.

 

Mazingira ya  Biashara ndogo na Sekta Binafsi

85.       Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha azma ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ya kuwapanga, kuwasimamia, kuwalinda na kuwawezesha wafanyabiashara wadogo inafikiwa, Serikali itaendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha wajasiriamali hao wadogo wanaboreshewa mazingira ya kufanyia biashara. Aidha, Serikali itaendelea kuwatambua na  kuwaunganisha na Taasisi za fedha ili waweze kupata mikopo nafuu. Vilevile, Serikali itaendelea kutenga maeneo na ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya wajasiriamali wadogo. Katika kuhakikisha utatuzi wa changamoto za machinga unakuwa shirikishi, Mheshimiwa Rais ameahidi kutoa shilingi milioni 10 kila mkoa kwa ajili ya kuimarisha uongozi wa machinga pamoja na ujenzi wa ofisi za machinga. Aidha, napendekeza kufanya mgao mpya wa mapato ya ndani ya halmashauri kama ifuatavyo: Asilimia 10 ya mapato ya vyanzo vya Halmashauri,  napendekeza  asilimia 5 iwe kwa ajili ya miundombinu na masoko ya machinga; asilimia 2 kwa vijana; asilimia 2 wanawake; na asilimia 1 kwa wenye ulemavu. Aidha, Serikali imetenga shilingi bilioni 45 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa miundombinu na mtaji kwa machinga ambapo kila mkoa, machinga walioko kwenye maeneo yaliopangwa wawe na revolving fund ya shilingi bilioni 1 kwa utaratibu utakaowekwa .

86.       Mheshimiwa Spika, katika kuongeza jitihada za kurasimisha sekta isiyo rasmi ili inufaike na kuwa sekta rasmi, Serikali imepanga kuweka mazingira rafiki ya kisheria na kikanuni katika usajili na uendeshaji wa biashara, kuharakisha usajili wa biashara kwa kuhakikisha usajili unakamilika ndani ya siku moja iwapo muombaji amekidhi masharti yanayohitajika, kuongeza upatikanaji wa mikopo kwa biashara zinazorasimishwa, kuongeza upatikanaji wa huduma kama miundominu ya biashara, mafunzo teknolojia na masoko. Vilevile, Serikali imepanga kuongeza vituo atamizi vya kukuza  biashara na maeneo maalumu ya viwanda.

 

87.       Mheshimiwa Spika, kwa kutambua mchango wa sekta binafsi katika uwekezaji, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara Nchini ili sekta binafsi iweze kushiriki kikamilifu katika kukuza uchumi wa nchi. Mwaka 2021/22, Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi ilishiriki majadiliano ya kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo katika kufanya biashara katika masoko ya nchi mbalimbali ikiwemo Kenya ambapo vikwazo visivyo vya kikodi 42 kati ya 64 vimepatiwa ufumbuzi. Hali hiyo iliwezesha ustawi wa biashara baina ya Tanzania na Kenya. Aidha, kupitia Sheria ya Fedha 2022/23, Serikali inapendekeza kufanya maboresho ya jumla ya maeneo 19 ya sheria mbalimbali ili kuboresha zaidi mazingira ya biashara na uwekezaji kama nitakavyoeleza baadae.

 

88.       Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuratibu ushiriki wa watanzania katika miradi ya kimkakati na uwekezaji unaofanyika hapa nchini (Local Content) ambapo jumla ya ajira 72,395 za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja zilizalishwa katika mwaka 2021. Vilevile, miradi ya kimkakati ilitoa kandarasi ndogo ndogo kwa kuingia mikataba na kampuni 2,019 za watanzania kwa huduma za chakula, ulinzi, biashara, bidhaa za ujenzi kama vile saruji, nondo, kokoto, mchanga, kampuni za usafiri, kampuni za bima na kampuni za mafuta. Kadhalika, Serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa na mikataba ya uwekezaji inasomana na sheria za kodi kwa ajili ya kutatua changamoto ya kutotekelezeka kwa baadhi ya miradi ya uwekezaji kutokana na kukinzana na sheria za kodi.

 

Ubia wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP)

89.       Mheshimiwa Spika,  katika utekelezaji wa miradi ya PPP, jumla ya miradi mitano (5) ipo katika hatua ya ununuzi wa mbia. Aidha, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Kwanza umepata mbia wa uendeshaji ambapo hatua inayofuata ni majadiliano na mbia husika. Hatua hii itaongeza ufanisi wa uendeshaji na utoaji wa huduma na mradi huu utakuwa mradi wa kielelezo uliopitia hatua zote zinazotakiwa kwa mujibu wa Sheria ya PPP, Sura 103. Upatikanaji wa wabia katika miradi ya PPP utaleta ahueni katika bajeti ya Serikali na hivyo kuwezesha kuongeza rasilimali fedha katika maeneo mengine na hivyo kuwaletea maendeleo watanzania. Serikali itaendelea kufanya tathmini ili kuboresha na kuipa nafasi sekta binafsi kushiriki katika kutekeleza miradi ya Serikali kwa mfumo wa Ubia na hivyo Serikali kujikita zaidi katika kuweka mazingira wezeshi na kuboresha huduma za kijamii.

90.       Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na mazingira wezeshi ya uwekezaji na ufanyaji biashara nchini, Serikali itaendelea kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Kufanya Biashara kwa kuimarisha miundombinu wezeshi ya usafirishaji na nishati; kuhakikisha uhimilivu wa viashiria vya uchumi jumla; na kuwianisha tozo na ada mbalimbali zinazotozwa na Wizara na Mamlaka za Udhibiti kwa lengo la kupunguza na kurahisisha ulipaji wake na kuzifuta baadhi ya tozo na ada za kero. Aidha, mwaka 2022/23, Serikali  itaendelea kufanya marekebisho ya viwango vya kodi, tozo na ada zinazotozwa chini ya sheria mbalimbali. Marekebisho hayo yanalenga kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi, hususan katika sekta ya viwanda, uwekezaji na biashara pamoja na kuongeza ajira, mauzo nje, mapato na akiba ya fedha za kigeni. Vilevile, katika kuepusha malimbikizo ya marejesho ya Kodi ya Ongezeko la Thamani - VAT na kupunguza mzigo wa madai ya fedha kutokana na ucheleweshaji wa marejesho kwa sekta binafsi, Serikali itaanza mchakato wa kuhakiki marejesho ya VAT kwa njia ya kielektroniki kuanzia mwaka 2022/23.

 

Sensa ya Watu na Makazi

91.       Mheshimiwa Spika, kipaumbele kingine katika bajeti ya mwaka 2022/23 ni ugharamiaji wa Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika tarehe 23 Agosti 2022. Ili kuwezesha zoezi hili muhimu, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 400.9. Aidha, napenda kutumia nafasi hii kupitia Bunge lako Tukufu kuhimiza wananchi wote kutoa ushirikiano siku hiyo hasa ukizingatia zoezi hili ni jukumu la kila mtu. Ushiriki wetu utaiwezesha Serikali, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na sekta binafsi kupata takwimu sahihi zitazokuwa msingi wa kuandaa, kutekeleza na kutathmini sera na mipango mbalimbali ya maendeleo katika nchi yetu.

 

Lugha ya Kiswahili

92.       Mheshimiwa Spika, lugha ya kiswahili ndio lugha ya Taifa, ndio lugha ya ofisini, ndio lugha ya pili kwa watoto wa vijijini na lugha ya kwanza kwa watoto waliowengi wa sasa, ndio lugha ya msingi, ni lugha ya Bunge, na nikiwa Waziri wa Katiba na Sheria nilileta mapendekezo kuifanya kuwa lugha ya Mahakama na lugha ya hukumu. Aidha, Kiswahili ni lugha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambapo tumeipeleka wenyewe, ikiwa ni pamoja na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa  Afrika (SADC) na Umoja wa Afrika (AU). Vilevile, UNESCO wameitambua na watakuwa wanaiadhimisha tarehe 7 Julai kila mwaka. Hii ndiyo lugha yetu, kwa nini usaili wa mtoto wa kitanzania anapotafuta kazi unafanyika kwa lugha ya Kingereza? Yaani afisa kilimo, afisa mifugo, mtumishi wa Serikali anakazi ya kuhudumia watanzania tunapima akili zake kwa kupima kingereza chake kwa ajili ya nini? Napendekeza saili zote zifanyike kwa Kiswahili, na kumbi zote za mikutano na ofisi za Serikali ziwe na vifaa vya kutafsiria lugha za kigeni na watafsiri ili tuweze kuienzi lugha yetu ya Taifa.

 

Sekta ya Michezo

93.       Mheshimiwa Spika, Serikali itarejesha bahati nasibu ya taifa kwa utaratibu wa kutumia Sekta Binafsi. Sambamba na hiyo Serikali kupitia  Bodi ya Michezo ya kubahatisha, TRA na Sekta Binafsi wataanza kuendesha bahati nasibu kwa kupitia risiti za EFD ili kuchochea wananchi kudai risiti wanaponunua bidhaa. Aidha, Serikali itatumia sehemu ya Mchango wa Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (Corporate Social Responsibity) kwa kiwango kisichozidi asilimia 2 kwa ridhaa ya Waziri mwenye dhamana ya masuala ya fedha ili kuendeleza michezo nchini ambapo makampuni yataruhusiwa kukitambua kiasi hicho kwenye mapato yanayostahili kutozwa kodi. Nitumie nafasi hii kuwahakikishia watanzania kuwa tutaweka nyasi bandia kwenye viwanja vitano kwa kuanzia Mwanza, Arusha, Tanga, Dodoma na Mbeya ili kukuza mchezo hapa nchini. Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 msamaha wa kodi kwenye nyasi bandia na vifaa ambata vyake utakwenda mpaka ngazi ya Halmashauri. Nitumie fursa hii kuzipongeza timu zetu za Serengeti Girls na Tembo Warriors zilizokata tiketi za kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya Dunia. Niitakie kila la heri timu yetu ya Taifa Stars ambayo bado iko kwenye kampeni za kutafuta tiketi ya mashindano ya kimataifa.

 

Mkakati wa Uchumi wa Buluu

94.       Mheshimiwa Spika, uchumi wa buluu kwa hapa Tanzania siyo jambo jipya kwani shughuli mbalimbali zimekuwa zikifanyika katika maeneo yenye fursa hizi za kiuchumi. Katika maeneo hayo, fursa za uwekezaji zinazopatikana ni za uvuvi wa samaki, ufugaji wa samaki, madini ya chumvi, utafutaji wa gesi na mafuta, kilimo cha mwani, utalii wa fukwe, usafiri na usafirishaji, utunzaji wa mazingira, na kilimo cha umwagiliaji. Hata hivyo, licha ya kuwepo kwa fursa nyingi katika eneo hili, bado mchango wake katika uchumi ni mdogo ikilinganishwa na uwezo uliopo. Hii ni kutokana na kukosekana kwa mfumo madhubuti  wa kuongoza na kuelekeza uvunaji na matumizi endelevu ya rasilimali hizo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo. Mheshimiwa Spika, sekta zilizoko katika eneo hili hazijawa na uratibu mzuri na kila moja inajifanyia shughuli zake bila utaratibu maalum na ushirikishaji wa kutosha wa wadau katika tasnia hii. Kama fursa hizo zingetumika kikamilifu, zingeweza kuwa kichocheo cha kukua kwa uchumi, chanzo cha chakula na ajira, msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, kukuza viwanda, kupunguza umaskini na kuongeza mapato ya Serikali.

 

95.       Mheshimiwa Spika, kufuatia umuhimu wa sekta hii, Serikali inakamilisha maandalizi ya Mkakati wa Uchumi wa Buluu ili kutambua mchango wa sekta hiyo katika uchumi na ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, Ibara ya 27. Mkakati huo unaandaliwa kwa njia shirikishi inayohusisha wadau wa sekta ya umma, sekta binafsi, washirika wa maendeleo na jamii kwa ujumla. Mheshimiwa Spika, shughuli nyingi zinazofanywa katika sekta za uchumi wa buluu ni biashara. Hivyo, sekta binafsi inatarajiwa kuwa na jukumu muhimu katika kufadhili mkakati huo. Serikali itajikita zaidi katika kujenga mazingira wezeshi ili kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi. Fedha za Serikali zitaelekezwa maeneo ambayo sekta binafsi ina hamu ndogo ikiwa ni pamoja na miundombinu wezeshi, kuweka mifumo ya kisera, kisheria na kitaasisi ya usimamizi na matumizi endelevu ya rasilimali hizo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.

 

Mikakati ya Kupunguza Makali ya Maisha kwa Mwananchi

96.       Mheshimiwa Spika, Serikali itachukua hatua za makusudi ili kupunguza makali ya maisha kwa mwananchi yaliyotokana na athari za vita. Hatua  zitakazochukuliwa kukabiliana na hali hiyo ni kama ifuatavyo: kuhusu ongezeko la bei za mafuta ya petroli: Serikali imepunguza tozo mbalimbali zilizokuwa kwenye ukokotoaji wa bei ya nishati ya mafuta. Aidha, Serikali imetoa ruzuku ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya kupunguza bei za nishati ya mafuta hapa nchini. Vilevile, Serikali inachukua hatua nyingine katika suala hili ikiwemo: kuendelea kutoa ruzuku kwa ajili ya kupunguza bei ya nishati ya mafuta; kuruhusu watu wenye uwezo wa kuleta mafuta kwa bei nafuu; kuanzisha mfuko wa kuhimili ukali wa bei za mafuta (Fuel Price Stabilization Fund) baada ya bei za mafuta kutulia katika soko la dunia; kuanzisha hifadhi ya mafuta ya kimkakati (National Strategic Petroleum Reserve); na kuanzisha upokeaji wa mafuta katika ghala moja (Single Receiving Terminal - SRT).

 

97.       Mheshimiwa Spika, kuhusu ongezeko la bei za mafuta ya kula: Serikali itaweka mikakati ya kikodi ili kutoa unafuu wa uagizaji wa mafuta ghafi ya kula kwa wachakataji wa ndani kwa lengo la kuongeza uzalishaji, kupunguza bei ya bidhaa hiyo na kuongeza ajira. Aidha, Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa Mbegu za Kilimo imesafisha na kusambaza kwa wakulima tani 2,000 za mbegu za alizeti zenye thamani ya shilingi bilioni 5.84 kwa utaratibu wa ruzuku kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula ambapo wastani wa tani 400,000 za alizeti na tani 100,000 za mafuta zinatarajiwa kuzalishwa. Vilevile, Wakala umezalisha mbegu-miche ya michikichi 121,292 ili kuongeza uzalishaji wa mafuta ya michikichi. Hatua hizi kwa pamoja zitasaidia kuongeza upatikanaji wa mafuta na hatimaye kupunguza kasi ya kupanda kwa bei. Napendekeza  kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha sifuri kwenye mafuta ya kula yanayozalishwa nchini.

 

 

98.       Mheshimiwa Spika, kuhusu ruzuku ya mbolea: Wote tunatambua umuhimu wa kilimo katika uchumi wetu na maendeleo ya wananchi. Sekta hii inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, tija ndogo pamoja na athari zinazoikumba dunia hivi sasa kutokana na vita kati ya nchi za Urusi na Ukraine. Katika kuongeza tija na uzalishaji wa sekta hii na kumpunguzia mzigo mkulima, Serikali imejipanga kutoa unafuu wa upatikanaji wa pembejeo ikiwemo mbolea, zana za kilimo, viuatilifu, mbegu bora na kuimarisha kilimo cha umwagiliaji. Katika kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa mbolea nchini, Serikali itatoa ruzuku ya mbolea  na kuvipa kipaumbele viwanda vya ndani vya mbolea katika matumizi ya chokaa ili kupunguza gharama za uzalishaji. Napendekeza  kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha sifuri kwenye mbolea inayozalishwa nchini. Kiwango hiki kitahusu tu wazalishaji wa mbolea. Kadhalika, napendekeza kupunguza tozo ya mrahaba kwenye madini ya kuzalisha nishati na mbolea viwandani.

 

99.       Mheshimiwa Spika, Serikali inachukua hatua hizi zote ili kupunguza makali ya maisha kwa watanzania. Serikali imekubali kupunguza mapato yake ili mwananchi au mtanzania apate unafuu. Ruzuku kwenye nishati ni kwa ajili ya wananchi siyo kwa ajili ya makampuni. Wafanyabiashara tusitumie majanga kujinufaisha kwa gharama ya kuwaumiza wananchi kwa kutengeneza faida kubwa kuliko kipindi cha majanga. Kipindi cha matatizo ya kiuchumi kila mmoja anatakiwa kubadili makadirio yake ya kiuchumi. Tunatoa ruzuku ili kupunguza gharama za uzalishaji na hivyo, kuleta unafuu kwa mwananchi. Naelekeza mamlaka zote zinazosimamia sekta za huduma wasimamie haki za wananchi ili azma ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ya kumpa nafuu mtanzania iweze kuwanufaisha watanzania.

 


V.       MABORESHO YA MFUMO WA KODI, ADA, TOZO NA HATUA NYINGINE ZA MAPATO

 

100.  Mheshimiwa Spika, kuanzia kipindi cha mwaka 2019/20, Dunia imepita kwenye changamoto kubwa ya kiuchumi kufuatia kuenea kwa janga la UVIKO-19 na baadaye kuzuka kwa vita ya Urusi na Ukraine Februari 2022. Hii imeathiri si tu upatikanaji wa bidhaa muhimu katika soko la Tanzania lakini pia imesababisha mfumuko wa bei, kupanda kwa gharama za maisha na kuathiri ukuaji wa uchumi nchini. Athari za kiuchumi zilizoanza kujitokeza ni pamoja na kupungua kwa uzalishaji viwandani na mashambani kulikosababishwa na changamoto ya upatikanaji wa malighafi muhimu za viwandani na kilimo kama vile ngano, mbolea na mafuta ghafi. Hatua za mapato kwa mwaka 2022/23 zinalenga Kuongeza kasi ya Kufufua Uchumi na Kuimarisha Sekta za Uzalishaji kwa ajili ya Kuboresha Maisha ya Watanzania”.

 

101.  Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maelezo hayo, napenda kuwasilisha mapendekezo ya kufanya marekebisho ya mfumo wa kodi, ikiwemo baadhi ya viwango vya kodi, tozo na ada zinazotozwa chini ya Sheria mbalimbali na kurekebisha taratibu za ukusanyaji na usimamiaji wa mapato ya Serikali. Marekebisho haya yamezingatia dhamira ya Serikali ya kuendelea kuwa na mfumo wa kodi ambao ni tulivu na wa kutabirika. Vilevile, marekebisho yanatarajiwa kujibu maswali na kukidhi kiu ya jamii ya Watanzania yakilenga kuchachua shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ndani ya nchi kwa kuweka mkazo katika sekta za kimkakati kama vile kilimo, ufugaji na uvuvi, miundombinu ya umeme, uchukuzi na usafirishaji na sekta za kijamii za elimu na afya ili kuboresha uzalishaji, kukuza uchumi jumla, kukuza ajira na hatimaye kupunguza ukali wa maisha ya wananchi. Aidha, hatua hizi zinalenga kuimarisha usimamizi, ukusanyaji wa mapato ya ndani ya nchi na kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali. Marekebisho yanayopendekezwa yanahusu sheria zifuatazo:

 

(a)       Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, SURA 148;

(b)       Sheria ya Kodi ya Mapato, SURA 332;

(c)       Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147;

(d)       Sheria ya Usimamizi wa Kodi, SURA 438;

(e)       Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, SURA 290;

(f)         Sheria ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, SURA 263;

(g)       Sheria ya Madini, SURA 123;

(h)      Sheria ya Korosho, NAMBA 18;

(i)         Sheria ya Usafirishaji Bidhaa Nje ya Nchi, SURA 196,

(j)         Sheria ya Posta na Mawasiliano ya Kielektroniki, SURA 306;

(k)       Sheria ya Bima, SURA 394;

(l)         Sheria ya Magari ya Kigeni, SURA 84;

(m)    Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania, SURA 197;

(n)      Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya mwaka 2004;

(o)       Utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mfumo wa Udhibiti wa Biashara (Blueprint) kwa kurekebisha Ada na Tozo mbalimbali; na

(p)       Marekebisho madogo madogo katika baadhi ya Sheria za Kodi na Sheria nyingine mbalimbali.

 

(a)   Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, SURA 148

 

102.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, Sura 148 kama ifuatavyo:

 

(i)         Kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye miti ambayo haijachakatwa (standing tree). Lengo la hatua hii ni kuchochea ukuaji wa sekta ya misitu, kuongeza ajira na kuwa na usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu. Hatua hii itapunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 8,814. Hata hivyo, mapato yatakayoongezeka kutokana na ukuaji wa sekta ya misitu na mnyororo wake wa thamani ni shilingi milioni 16,125 na hivyo kuleta ongezeko katika sekta hii kwa kiwango cha shilingi milioni 7,311;

 

(ii)      Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye malighafi zinazotumika kuzalisha mitungi ya gesi zinazotambulika kwa HS Code 7229.90.00, 3810.90.00, 3401.19.00, 7904.00.00, 4016.93.00, 8481.10.00 na 8309.90.90. Lengo la hatua hii ni kuwapa unafuu wazalishaji wa mitungi ya gesi na kulinda viwanda vya ndani. Aidha, msamaha husika utatolewa baada ya mzalishaji kusaini Mkataba wa Utekelezaji (Performance Agreement) na Serikali;

 

(iii)    Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ili kutambua mikopo mbadala inayofuata misingi na taratibu zilizo nje ya sekta ya fedha kwa asili yake ishughulikiwe sawa sawa (treated) na mikopo inayotolewa na benki katika utaratibu wa kawaida. Lengo la hatua hii ni kuchachua ukuaji wa bidhaa nyingine zenye lengo la kuchochea ukuaji wa biashara na uchumi na kuweka usawa katika ulipaji kodi;

 

(iv)     Kutoza Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa Kiwango cha asilimia 0 kwenye bidhaa za mafuta ya kula yanayozalishwa nchini kwa mwaka mmoja ili kuleta unafuu wa bei ya mafuta ya kula iliyopanda kutokana na mdororo wa uchumi;

 

(v)       Kutoza Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa kiwango cha sifuri kwenye mbolea inayozalishwa nchini kwa mwaka mmoja. Kiwango hiki kitahusu tu wazalishaji wa mbolea tu. Lengo la hatua hii ni kuleta unafuu kwa wakulima hasa katika kipindi hiki cha mdororo wa uchumi duniani;

 

(vi)     Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ili kumpa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya Fedha, mamlaka ya kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa wawekezaji mahiri maalumu baada ya kuidhinishwa na NISC kwa mujibu wa kifungu cha 20(8) cha Sheria ya Uwekezaji SURA, 38 pamoja na kupata ridhaa ya Baraza la Mawaziri. Lengo la hatua hii ni kufanikisha maendeleo ya sekta ya uwekezaji nchini na kuondoa mgongano wa kisheria kuhusu utoaji wa vivutio vya ziada vya kikodi kati ya Sheria ya Uwekezaji na Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani;

 

(vii)  Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 11 (10) cha Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ili kuhusisha bidhaa za mtaji zinazotambulika kwa heading 87.16 na HS Code 8701.20.90 kwenye bidhaa za mtaji (capital goods) zinazostahili kupata ahirisho la Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT deferment). Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za uwekezaji na kuchochea maendeleo ya viwanda nchini;

 

(viii)   Kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifaa vya kupima kiwango cha maji na unyevunyevu kwenye udongo (chameleon sensor reader) zinazotambulika kwa HS Code 9026.10.00, kifaa cha kupima kiasi kilichochukuliwa na udongo hasa katika eneo la mizizi ya mmea (wetting front detectors) kinachotambulika kwa HS Code 9031.80.00, kifaa cha kupima kiwango cha chumvi katika maji (electronic conductivity meter) kinachotambulika kwa HS Code 9027.80.00, na kifaa cha kupima kiwango cha naitrojeni katika hali ya naitreti (nitrate test strips) kinachotambulika kwa HS Code 9027.90.00. Lengo la hatua hii ni kukuza utafiti na kuendeleza sekta ya kilimo kwa ukuaji endelevu pamoja na kuongeza tija. Msamaha utatolewa baada ya kupata uthibitisho wa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kilimo ili kuhakikisha msamaha husika unatumika kwa manufaa ya wakulima na si vinginevyo. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 2,995;

 

(ix)    Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vyandarua vinavyotumika katika uzalishaji wa mbogamboga na maua (Agro-net) vinavyotambulika kwa HS Code 56.08. Lengo la hatua hii ni kukuza sekta ya kilimo na kuongeza tija kwenye uzalishaji;

 

(x)       Kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifaa vya kupima kiwango cha unyevunyevu (moisture meter) vinavyotambulika kwa HS Code 9003.18.00, kifaa cha kupima kiwango cha mvua iliyonyesha (rain gauge for weather stations) kinachotambulika kwa HS Code 9023.00.90, kifaa cha kupima hali ya alkaline na tindikali (PH meters) kinachotambulika kwa HS Code 3822.00.90; kifaa cha kuzalisha miche/mbegu kwa chupa (tissue culture equipment) kinachotambulika kwa HS Code 8419.89.60; na kifaa cha kupima uwezo wa kuvutika (tension meters) kinachotambulika kwa HS Code 9031.80.00. Lengo la hatua hii ni kuboresha utabiri wa hali ya hewa, kufahamisha mipango sahihi na kupunguza hatari zinazohusiana na kutokuwa na uhakika wa hali ya hewa na hali ya udongo. Msamaha utatolewa baada ya kupata uthibitisho wa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kilimo ili kuhakikisha msamaha husika unatumika kwa manufaa ya wakulima na si vinginevyo. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 1,634.52;

 

(xi)    Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye magari yenye jokofu (refrigerated trucks) yanayotambulika kwa HS Code 8704.21.90, 8704.22.90, 8704.23.90, 8704.31.90, 8704.32.90, 8704.90.90 na vyumba vya ubaridi (cold rooms) vinavyotambulika kwa HS Code 9406.10.10 na 9406.9010.  Hatua hii inalenga kuzuia mazao kuharibika baada ya mavuno na kuchochea kilimo cha kisasa. Msamaha utatolewa baada ya kupata uthibitisho wa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kilimo na au Waziri mwenye dhamana ya masuala ya mifugo na uvuvi ili kuhakikisha msamaha husika unatumika kama ilivyokusudiwa na si vinginevyo. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 3,744.47;

 

(xii)  Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye malighafi za kutengeneza mbolea zinazotambulika kwa HS Code 2528.00.00, 2710.99.00 na 3505.20.00 na mashine za kutengeneza mbolea zinazotambulika kwa Sura (Chapter) 84 na 85 ya Kitabu cha Ushuru wa pamoja wa Forodha wa Afrika Mashariki.  Hatua hii inalenga kutoa unafuu kwa wazalishaji wa mbolea na kuvutia uwekezaji nchini. Msamaha utatolewa baada ya kupata uthibitisho wa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya viwanda ili kuhakikisha msamaha husika unatumika kwa manufaa ya wazalishaji wa mbolea na si vinginevyo. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 139;

 

(xiii)  Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vanila ya kijani isiyochakatwa inayotambulika kwa HS Code 0905.10.00 ili kuleta usawa na mazao mengine yasiyochakatwa ambayo husamehewa Kodi ya Ongezeko la Thamani. Hatua hii inalenga vanilla isiyochakatwa kutoka nje ya nchi kuingizwa na kuchakatwa hapa nchini na hivyo kuongeza ajira na fedha za kigeni. Vanila inayolimwa hapa nchini haitoshelezi mahitaji ya kiwanda cha kuchakata zao hili. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 38;

 

(xiv)   Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye kamba za katani zinazozalishwa nchini. Lengo la hatua hii ni kukuza zao la katani na kuongeza ajira;

 

(xv)   Kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye mtindi (yoghurt) na maziwa yanayozalishwa kwa joto la juu na kudumu kwa muda mrefu (UHT Milk). Hatua hii inalenga kuwawezesha wazalishaji wa ndani kushindana kikanda na kimataifa, kuongeza ajira na kuboresha maisha ya watu. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 480;

(xvi)   Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifungashio vya maziwa (dairy packaging materials) vinavyotambulika kwa HS Code 3923.30.00, 4819.10.00, 4819.20.00 na 4819.20.90. Hatua hii inalenga kutoa unafuu kwenye sekta ya maziwa nchini na kuwawezesha wazalishaji wa ndani kushindana kwenye masoko ya kikanda na kimataifa. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 1,197;

 

(xvii)Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye hereni za mifugo za kieletroniki (ear tag) zinazotambulika kwa HS Code 3926.90.90, meza za kuwekea hereni za mifugo (Automatic Turning Table/ Ear tag supporting table) zinazotambulika kwa HS Code 8207.30.00, Ear tag Applicators zinazotambulika kwa HS Code 8456.90.00 na Lessor beam Machines zinazotambulika kwa HS Code 9402.90.90.  Lengo la hatua hii ni kuleta ufanisi katika utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo nchini. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 794;

 

(xviii)  Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifaa vya machinjio (stunning box) vinavyotambulika kwa HS Code 8438.50.00 na Skinning & dehiding pulling machines zinazotambulika kwa HS Code 8453.10.00. Hatua hii inalenga kuhamasisha ukuaji wa sekta ya mifugo, kuongeza ubora wa nyama na ngozi na kuhakikisha kuwa viwanda vya ndani vinapata malighafi za kutosha. Msamaha utatolewa baada ya kupata uthibitisho ya Waziri mwenye dhamana ya masuala ya mifugo na uvuvi ili kuhakikisha msamaha husika unatumika kama ilivyokusudiwa na si vinginevyo. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 331.95;

 

(xix)        Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye mbegu za malisho zinazotambulika kwa HS Code 1209.25.00 (pasture grass seeds); HS Code 1209.21.00 (pasture legume seeds), HS Code 1209.29.00 (Pasture multiple tree seeds and pasture cuttings and rhizomes and stolons). Hatua hii inalenga kuhakikisha upatikanaji wa mbegu za malisho za kutosha na kukuza sekta ya mifugo;

 

(xx)  Kufanya marekebisho kwenye Kipengele cha 18 cha Sehemu ya Kwanza ya Jedwali la Msamaha ili kuhusisha vifaa na mashine zinazotumiwa na vyombo vya ulinzi na usalama (military and armed forces). Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ununuzi wa mashine na vifaa husika na kuimarisha mfumo wa ulinzi na usalama nchini. Msamaha utatolewa baada ya kupata uthibitisho wa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya ulinzi na usalama ili kuhakikisha msamaha husika unatumika kwa manufaa ya vyombo vya ulinzi na usalama na si vinginevyo;

 

(xxi)  Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifaa na mitambo ya hali ya hewa vinavyoingizwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA). Hatua hii inalenga kuimarisha mifumo ya utendaji kazi kwa kutumia vifaa vya kisasa kutabiri hali ya hewa kwa ajili ya mipango sahihi na usalama wa Taifa;

 

(xxii)  Kusamehe kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye nyavu za kuvulia (fishing net) zinazotambulika kwa HS Code 3926.09.10; ndoano (fishing hooks) zinazotambulika kwa HS Code 9507.20.00; na kamba za kufungia ndoano (fishing lines) zinazotambulika kwa HS Code 9507.90.00 na 9507.30.00. Lengo la hatua hii ni kukuza wavuvi wadogo na kuchochea ukuaji wa Sekta ya Uvuvi;

 

(xxiii)  Kufanya marekebisho ya Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, SURA 148 ili kuiwezesha Serikali kukusanya Kodi ya Ongezeko la Thamani katika biashara mtandao (digital services) bila kuathiri uwajibikaji chini ya Sheria ya Kodi ya Mapato, SURA 332. Aidha marekebisho haya yanalenga kurahisisha utaratibu wa usajili wa walipakodi wanaotoa huduma za kidijitali bila ya kuwa na makazi hapa nchini (simplified registration). Hatua hii inalenga kwenda sambamba na mwamko wa shughuli za kibiashara duniani zinazofanyika kwa njia ya mtandao. Hatua hii inatarajiwa kuiongezea Serikali mapato ya shilingi milioni 34,240;

(xxiv)  Kufuta msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye simu janja za Mkononi (Smartphones) HS code 8517.12.00, vishikwambi (Tablets) HS Code 8471.30.00 au 8517.12.00 na Modemu HS Code 8517.62.00 au 8517.69.00 kwa kuwa msamaha husika haujawezesha kupatikana kwa bidhaa hizo muhimu kwa bei nafuu kwa walengwa na badala yake unawanufaisha wafanyabiashara. Hatua hii inalenga kuiongezea Serikali mapato kiasi cha Shilingi milioni 33,705; na

 

(xxv)     Kufuta msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye huduma za kukodi ndege (air charter services) kwani huduma hizi hutolewa kibiashara kama huduma za kukodi vyombo vingine vya usafiri ambazo kisheria hulipiwa Kodi ya Ongezeko la Thamani. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shillingi milioni 36,545.

 

Hatua zote za Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa ujumla wake zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 87,523.

(b)  Sheria ya Kodi ya Mapato, SURA 332

103.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya   Kodi ya Mapato, Sura 332 kama ifuatavyo:

 

(i)      Kufanya marekebisho kwenye Jedwali la Kwanza la Sheria ya Kodi ya Mapato ili kuweka kiwango cha asilimia 3.5 kwa walipakodi wenye mauzo yanayozidi shilingi milioni 11,000,000 lakini yasiyozidi shilingi milioni 100,000,000/= kwa mwaka (Presumptive Regime) kwa lengo la kuweka uwazi na kurahisisha makadirio na ulipaji wa kodi. Hatua hii itaongeza ulipaji kodi wa hiari na hivyo kuongeza mapato ya Serikali ambayo yanatarajiwa kuongezeka kwa shilingi milioni 60,413.37. Sambamba na pendekezo hili, inapendekezwa kufanya maboresho kwenye mifumo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania ili kuwezesha malipo kufanyika kwa njia ya simu;

 

(ii)   Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Mapato ili kubainisha kuwa mikopo mbadala iliyoidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania inayotolewa na benki kwa wateja wake ambayo inahusisha ununuzi na uuzaji wa mali anazozihitaji mteja kwa faida inayowekwa juu ya gharama ya mali ni sawa na mikopo mingine ya kawaida. Hatua hii haimwondolei muuzaji wajibu wa kulipa kodi ya ongezeko la mtaji kwa mujibu wa Sheria katika muamala wa mauzo ya mali kwa mteja wa benki aliyenunua mali hiyo kupitia utaratibu wa mkopo mbadala. Lengo la hatua hii ni kuhakikisha kuwa Watanzania wote wanaweza kupata mikopo katika taasisi za fedha ikijumuisha wale ambao hawakubaliani na utaratibu wa riba;

 

(iii) Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 10 cha Sheria ya Kodi ya Mapato ili kumpa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya Fedha mamlaka ya kusamehe kodi ya mapato kwa wawekezaji mahiri maalumu baada ya kuidhinishwa na NISC kwa mujibu wa kifungu cha 20(8) cha Sheria ya Uwekezaji Sura ya 38, pamoja na kupata ridhaa ya Baraza la Mawaziri. Lengo la hatua hii ni kufanikisha maendeleo ya sekta ya uwekezaji nchini na kuondoa mgongano wa kisheria kuhusu utoaji wa vivutio vya ziada vya kikodi kati ya Sheria ya Uwekezaji na Sheria ya Kodi ya Mapato;

(iv)  Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Kodi ya Mapato ili kuondoa msamaha wa kukata Kodi ya Zuio kwenye malipo ya upangishaji nyumba, vyumba na majengo ya biashara. Lengo la hatua hii ni kuwezesha wapangaji kukusanya kodi ya zuio kwenye pango na kuiwasilisha Serikalini. Aidha, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato ataingia makubaliano ya uwakala na OR - TAMISEMI juu ya usimamizi na ukusanyaji wa kodi hii;

 

(v)    Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Mtaji kwenye uhamishaji wa haki na taarifa za madini kwenda kwenye Kampuni za Ubia zinazoundwa baina ya Serikali na wawekezaji na uhamishaji wa hisa (Free Carried Interest) kutoka Kampuni ya Ubia kwenda kwa Serikali. Hatua hii inalenga kusaidia Serikali kutekeleza majukumu yake ya kimkataba na kuhakikisha kuwa uhamishaji na ubadilishaji wa haki na taarifa za madini unafanyika kwa wakati;

 

(vi)  Kusamehe Kodi ya Ongezeko la Mtaji kwenye hisa ambazo Serikali imepata kupitia Msajili wa Hazina. Lengo la hatua hii ni kutatua changamoto zilizopo na kuhakikisha kuwa zoezi la ubadilishaji umiliki wa hisa hizo linafanyika kwa wakati;

 

(vii)      Kusamehe kodi ya zuio kwenye Kuponi za Hati Fungani za Makampuni na Manispaa (Coupon for corporate and municipal bond). Pendekezo hili linalenga kuongeza vyanzo mbadala vya kugharamia miradi ya maendeleo (alternative financing);

 

(viii)    Kupunguza kiwango cha kodi ya zuio kwenye tasnia ya filamu kwa malipo yanayofanyika kwenda kwa watoa huduma wa nje ya nchi kutoka asilimia 15 hadi asilimia 10. Lengo la hatua hii ni kukuza tasnia ya filamu na kuchochea uhamishaji wa ujuzi kwenye tasnia hiyo kwa lengo la kuongeza ajira na kuboresha maisha;

 

(ix) Kutoza Kodi ya Mapato ya asilimia 2 kwenye malipo yanayofanywa kwa watoa huduma za kidijitali wa kigeni. Lengo la hatua hii ni kuongeza wigo wa kodi na kuzingatia kanuni za usawa za kodi. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 4,889.35;

(x)    Kutoza Kodi ya Zuio kwa kiwango cha asilimia 2 kwenye malipo ya wachimbaji wadogo wa madini (Small Scale Miners). Hatua hii inalenga kuweka utaratibu maalum wa utozaji kodi kwa wachimbaji hao na kutatua changamoto zilizopo kwenye ukusanyaji kodi katika sekta hiyo. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 37,290.40;

 

(xi) Kutoza kiwango cha mfuto (flat rate) cha shilingi 3,500,000 ikiwa ni kodi ya mapato inayopaswa kulipwa kwa kila magari ya mizigo na mabasi ya abiria kwa mwaka. Lengo la hatua hii ni kuongeza uwazi katika makadirio ya kodi baina ya Mamlaka ya Mapato Tanzania na walipakodi, kuweka mfumo wa kodi unaotabirika na kuongeza mapato ya Serikali. Hatua hii inatarajiwa kuiongezea Serikali mapato yanayokadiriwa kuwa shilingi milioni 141,052;

 

(xii)      Kuanzisha utaratibu wa kutoza kodi ya awali ya mapato (advance income tax) ya shilingi 20 kwa lita kwa wafanyabiashara rejareja wa mafuta ya petroli nchini itakayokusanywa na waingizaji wa mafuta hayo kwa jumla na kulipwa Serikalini. Lengo la hatua hii ni kurahisisha ulipaji kodi ya mapato kwenye vituo vya mafuta na kupunguza gharama za matumizi hususan karatasi za kutolea risiti za kielektroniki; Hatua hii inatarajiwa kuiongezea Serikali mapato yanayokadiriwa kuwa shilingi milioni 59,820.

 

Hatua hizi za Kodi ya Mapato kwa ujumla wake zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 102,593.

 

(c)   Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147

 

104.  Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa Sheria ya Ushuru wa Bidhaa kifungu cha 124(2), marekebisho ya viwango maalum vya ushuru wa bidhaa (specific duty rates) kwa bidhaa zote zisizo za petroli yanaweza kufanyika kila mwaka ili kuviwianisha na mfumuko wa bei na viashiria vingine vya uchumi jumla. Hata hivyo, kutokana na biashara za bidhaa hizi kuzorota kutokana na athari za kiuchumi zilizosababishwa na kupanda bei kwa bidhaa za mafuta, napendekeza kutokufanya mabadiliko ya viwango maalum vya Ushuru wa Bidhaa kwa bidhaa zote zisizo za petroli. Aidha, hatua hii inazingatia kiwango kikubwa cha mfumuko wa bei nchini na azma ya Serikali ya kujenga uchumi wa viwanda, na hivyo kuhamasisha uwekezaji kwenye sekta ya viwanda, kuvilinda na hatimaye kukuza ajira na mchango wa sekta hiyo kwenye pato la Taifa.

 

105.  Mheshimiwa Spika, napendekeza pia kufanya marekebisho ya Ushuru wa bidhaa kwenye bidhaa zifuatazo:

 

(i)    Kupunguza ada ya leseni kwa wazalishaji na waingizaji wa bidhaa zinazotozwa Ushuru wa Bidhaa kutoka shilingi 500,000/= hadi shilingi 300,000/=. Hatua hii inalenga kuwapa unafuu wazalishaji na waingizaji wa bidhaa hizo pamoja na kusaidia kurejesha ukuaji wa Sekta baada ya athari za UVIKO-19 na athari zinazotokana na msukosuko wa kiuchumi duniani. Hatua hii inatarajiwa kupunguza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 77.4. Utaratibu wa ukusanyaji wa kodi kwenye vitenge unafanywa na Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania chini ya Sheria ya Pamoja ya Ushuru wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya mwaka 2004;

 

(ii)  Kusamehe Ushuru wa Bidhaa kwenye vifungashio vya maua, matunda, na mbogamboga vinavyotambulika kwa HS Codes 3923.29.00 (puneet, plastic cryovac bags, modified atmosphere packaging - MAP bags, plastic sleeves, perforated bags, poly packaging bags), HS Code 3921.12.90 (cling firm), HS Code 3902.90.00 (plastic liners). Lengo la hatua hii ni kuwapunguzia gharama wazalishaji wa matunda, mbogamboga na maua, na kuongeza usafirishaji wa bidhaa hizo nje ya nchi na hivyo kuongeza fedha za kigeni. Hatua hii inatarajia kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 653.12;

  

(iii)        Kutoza ushuru wa bidhaa wa shilingi 700 kwa kilo ya bidhaa za sukari (sugar confectionery) zinazoingizwa kutoka nje ya nchi na shilingi 500 kwa kilo ya bidhaa za sukari zinazozalishwa hapa nchini zinazotambuliwa kwa HS Code 1806.31.00, 1806.32.00, 1806.90.00, (chokoleti), 1905.31 (biskuti) na 1704 (chingamu). Viwango tofauti vinapendekezwa ili kulinda viwanda vya ndani. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 34,453.87; na

 

(iv)Kutoza Ushuru wa Bidhaa kwenye betri za maji (Lead-acid battery) kwa kiwango cha asilimia 5 zinazotambuliwa kwa HS Code 8507.10.00, na 8507.20.00. Hatua hii inalenga kupunguza madhara ya mazingira yanayosababishwa na matumizi ya bidhaa hizo. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 1,864.85;

 

Hatua hizi za Ushuru wa Bidhaa kwenye bidhaa zisizo za petroli kwa ujumla wake zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 50,292.

 

(d)  Sheria ya Usimamizi wa Kodi, SURA 438

 

106.  Mheshimiwa Spika, Napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Usimamizi wa Kodi, SURA 438 ili kumrejeshea Waziri mwenye dhamana ya masuala ya Fedha na Mipango mamlaka ya kusamehe riba na adhabu baada ya kushauriwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania. Lengo la hatua hii ni kuondoa changamoto zilizopo katika kutoa misamaha hii na kurahisisha upunguzaji au uondoaji wa riba na adhabu ya madeni. Aidha, Waziri mwenye dhamana ya Fedha na Mipango atatoa utaratibu wa utoaji wa misamaha hii kwa njia ya kanuni au kwa namna atakavyoona inafaa.

 

(e)   Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, SURA 290

107.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa kama ifuatavyo:

(i)    Napendekeza Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, SURA 290 ili kugawanya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri katika utaratibu ufuatao: asilimia 5 ipelekwe kwenye miundombinu na masoko ya machinga, asilimia 2 kwa ajili ya mikopo kwa vijana, asilimia 2 kwa ajili ya wanawake na asilimia 1 kwa ajili ya watu wenye ulemavu. Lengo la hatua hii ni kuendeleza juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita zinazolenga kuwawekea miundombinu wajasiriamali wadogo ili kuhakikisha wanapata maeneo ya kufanyia biashara kutokana na mikopo wanayopata;

 

(ii)  Aidha, Halmashauri zihakikishe kuwa zinafanya tathmini ya vyanzo vya mapato kabla ya kuingia mikataba ya uwakala wa mapato kutoka kwenye vyanzo husika na kuhakikisha kwamba kiasi kinachokusanywa kinaendana na uwezo wa chanzo hicho. Sambamba na hilo naelekeza kuwa fedha zote zinazokusanywa kwa njia ya Point of Sale (POS) zinazojulikana kama mapato ghafi zihamishiwe benki katika kipindi kisichozidi siku saba kutokea kukusanywa kwa mapato hayo na Halmashauri zihakikishe kuwa fedha zinazokusanywa kwenye Halmashauri za Serikali za Mitaa zinahasibiwa kikamilifu;

(iii)  Kusamehe Ushuru wa Mazao kwenye mbegu (seeds). Hatua hii inalenga kuwapa unafuu wakulima na kuongeza tija kwenye uzalishaji mazao mbalimbali;

 

(iv)Kupunguza Ushuru wa Mazao ya misitu (forest produce cess) kutoka asilimia 5 hadi asilimia 3. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama kwa wafanyabiashara wa mazao ya misitu na kukuza sekta ya misitu;

 

(v)   Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 16(7) cha Sheria ya Fedha za Mamlaka za Serikali za Mitaa Sura 290 ili kubainisha kwamba Makampuni/Taasisi/Biashara/Watu binafsi wanaotakiwa kulipa Ushuru wa Huduma (service levy) kwenye Halmashauri moja wanatakiwa kulipa Ushuru wa Mazao (produce cess) kwenye Halmashauri nyingine ambako wananunua mazao ya kilimo au mazao mengine. Lengo la mapendekezo hayo ni kuhakikisha kwamba kila Halmashauri inanufaika na shughuli za kiuchumi zinazotekelezwa kwenye eneo lake la utawala ili kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa jamii; na

 

(vi)Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 16 ili kumpa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa mamlaka ya kuandaa Kanuni za ugawaji mapato yatokanayo na Ushuru wa Huduma kwenye Makampuni/Taasisi/Bishara/Watu binafsi wanaotekeleza shughuli zao kwenye Halmashauri zaidi ya moja. Kifungu hiki kitamwezesha Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa kutoa Mwongozo wa ugawaji wa mapato hayo kwa Halmashauri husika kulingana na hali halisi.

 

(f)    Sheria ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, Sura 263

 

108.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kwa kupunguza kiwango cha mchango kwa sekta binafsi kutoka asilimia 0.6 inayotozwa sasa hadi asilimia 0.5 ya mapato ghafi ya wafanyakazi. Lengo la hatua hii ni kuleta usawa katika uchangiaji kati ya wafanyakazi wa sekta binafsi na wa umma.

 

(g)   Sheria ya Madini, SURA 123

 

109.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Madini, Sura 123 kama ifuatavyo:

(i)    Kupunguza kiwango cha mrabaha kutoka kwenye makaa ya mawe yanayotumika kama malighafi ya kuzalisha nishati viwandani kutoka asilimia 3 hadi asilimia moja. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za uzalishaji viwandani, kuchochea uwekezaji zaidi na kukuza ajira;

 

(ii)  Kupunguza kiwango cha kutoza mrabaha (royalty) kutoka asilimia 6 hadi asilimia 4 kwa dhahabu inayouzwa kwenye vituo vya kusafishia madini (refinery centres). Lengo la hatua hii ni kuhakikisha kuwa vituo vilivyoanzishwa nchini vinapata malighafi ya kutosha kwa ajili ya kusafisha na hatimaye kuongeza ajira na mapato ya Serikali;

 

(h)  Sheria ya Korosho, Namba 18

 

110.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Korosho ili mapato yatokanayo na tozo ya kusafirisha korosho ghafi nje ya nchi yagawanywe kama ifuatavyo: asilimia 50 ipelekwe Wizara ya Kilimo kwa ajili ya ruzuku ya pembejeo na Mfuko wa Kilimo (ADF); na asilimia 50 ipelekwe mfuko mkuu wa Serikali. Lengo la hatua hii ni kuchochea maendeleo ya Sekta ya kilimo na kusaidia upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya ruzuku na tafiti.

 

(i)    Sheria ya Usafirishaji Bidhaa Nje ya Nchi, SURA 196

 

111.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Usafirishaji Bidhaa Nje kwa kuanza kutoza tozo ya asilimia 30 au dola za kimarekani 150 kwenye shaba chakavu (copper waste) zinazotambulika kwa HS Code 7204 na vyuma chakavu (scrap metals) zinazotambulika kwa HS Code 7404. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vya ndani na kuhakikisha upatikanaji wa malighafi kwenye viwanda husika. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 2,446.

 

(j)     Sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa, SURA 437

 

112.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa kwa kupunguza tozo ya muamala kutoka kiwango kisichozidi shilingi 7,000 hadi kiwango kisichozidi shilingi 4,000 katika kila muamala wa kutuma au kutoa pesa. Punguzo hili ni sawa na asilimia 43 ya kiwango cha sasa. Sambamba na hilo, napendekeza kuongeza wigo wa tozo hiyo ili kuhusisha miamala yote ya kielektroniki. Lengo la hatua hii ni kupunguza makali ya maisha kwa mtanzania hasa katika kipindi hiki cha changamoto kubwa ya kiuchumi na kuweka usawa katika utozaji wa tozo hiyo.

 

(k)  Sheria ya Bima, SURA 394

 

113.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Bima kwa kuongeza wigo wa bima ya lazima (mandatory insurance) kwa kujumuisha masoko ya umma, majengo ya biashara, bidhaa zote zinazoagizwa kutoka nje, vyombo vya baharini na vivuko. Hatua hii inalenga kuimarisha ushirikishwaji wa kifedha (financial inclusion) na kuongeza matumizi ya bima.

 

(l)     Sheria ya Magari ya Kigeni, SURA 84

 

114.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Magari ya Kigeni, SURA 84 ili kupunguza tozo ya magari yanayozidi ekseli 3 kutoka dola za kimarekani 16/100 km hadi dola za kimarekani 10/100 km. Lengo la hatua hii ni kuwianisha utozaji wa viwango vya tozo hizo katika ukanda wa EAC, SADC na COMESA.

(m)     Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania, SURA 197

 

115.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania kwa kuweka kiwango cha ukomo wa Serikali kukopa kuwa kiasi kisichozidi asilimia 18 ya mapato ya ndani yaliyoidhinishwa katika mwaka husika badala ya kiwango cha sasa cha moja ya nane ya mapato ya ndani yaliyokusanywa katika mwaka uliotangulia. Lengo la hatua hii ni kuwianisha kiwango husika na nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na kuiwezesha Serikali kutekeleza Bajeti yake.

 

(n)  Sheria ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya mwaka 2004

 

116.  Mheshimiwa Spika, kikao cha Mawaziri wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika tarehe 13 Mei, 2022 Mombasa Kenya, kilipendekeza kufanya marekebisho ya Viwango vya Pamoja vya Ushuru wa Forodha (EAC-Common External Tariff) kwa mwaka wa Fedha 2022/23. Mapendekezo hayo yanalenga kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuimarisha Sekta za uzalishaji kwa ajili ya kuboresha maisha.

117.  Mheshimiwa Spika, mapendekezo ya Mawaziri wa Fedha ya kufanya marekebisho kwenye Viwango vya Pamoja vya Ushuru wa Forodha yanahusisha hatua mpya na zinazoendelea ambazo zimekuwa zikitekelezwa katika Mwaka wa Fedha 2021/22. Hatua hizo ni kama zifuatazo:

(i)         Mapendekezo ya hatua mpya za Viwango vya Ushuru wa Forodha ni kama ifuatavyo: -

(a)   Kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 35 au dola za Marekani 1.5 kwa kila mita moja ya mraba (square meter) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwa mwaka mmoja kwenye bidhaa za marumaru zinazotambulika kwa HS Codes 6907.21.00; 6907.22.00; na 6907.23.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vya ndani vinavyozalisha marumaru, pamoja na kudhibiti udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo kutoka nje;

 

(b)   Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 10 au dola za Marekani 125 kwa kila tani moja (Metric ton) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwenye mabati yanayotambulika kwa HS Codes 7212.20.00; na 7226.99.00 kwa mwaka mmoja badala ya ushuru wa asilimia 10 pekee. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vya ndani kutokana na udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo zinapoingizwa kutoka nje (under-invoicing and under valuation), na kulinda ajira pamoja na mapato ya Serikali;

 

(c)    Kurejesha utozaji wa Ushuru wa Forodha wa kiwango cha asilimia 0 kutoka kiwango kilichokuwa kinatumika cha asilimia 25 kwenye mafuta ghafi ya kula (Crude Palm Oil) yanayotambulika kwa HS code 1511.10.00. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wachakataji wa mafuta ghafi hapa nchini ili wananchi waweze kupata mafuta ya kula kwa bei nafuu;

 

(d)   Kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 10 kwa mwaka mmoja kutoka kiwango cha awali cha asilimia 0 kwenye mafuta ghafi ya soya, karanga, nazi na haradali zinazotambulika kwa HS codes 1507.10.00; 1508.10.00; 1513.11.00; 1514.91.00; na 1515.11.00. Lengo la hatua hii ni kuoanisha viwango vya mafuta haya ghafi vifanane na viwango vya mafuta ghafi ya alizeti, pamba na mafuta ghafi mengineyo ambayo viwango vyake ni asilimia 10. Aidha, hatua hii pia inalenga kulinda na kuhamasisha uzalishaji wa mbegu za mafuta ya kula nchini, kuongeza ajira pamoja na kulinda fedha za kigeni zinazotumika kuagiza mafuta hayo nje ya nchi;

 

(e)    Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 500 kwa kila tani moja ya ujazo (Metric ton)  kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa badala ya asilimia 35 kwa mwaka mmoja kwenye mafuta ya kula yaliyochakatwa kwa kiwango cha kati na cha mwisho (semi-refined and refined) yanayotambulika kwa HS codes 1507.90.00;  1508.90.00; 1509; 1510.10.00; 1510.90.00;  1511.90.10; 1511.90.30; 1511.90.90; 1512.19.00; 1512.29.00; 1513.19.00; 1513.29.00; 1514.19.00; 1514.99.00; 1515.19.00; 1515.29.00; 1515.50.00; na 1515.90.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda na kuhamasisha uchakataji wa mbegu na mafuta ghafi yaliyoingizwa nchini ili kuongeza thamani ya bidhaa (value addition) na kukuza ajira;

 

(f)     Kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 35 kwa mwaka mmoja kwenye taulo za watoto (Baby Diapers) zinazotumbulika kwa HS code 9619.00.90. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vinavyozalisha bidhaa hii nchini, kuongeza ajira pamoja na mapato ya Serikali;

 

(g)    Kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 10 hadi asilimia 25 kwa mwaka mmoja kwenye nyuzi za pamba (cotton yarn) zinazotambulika kwa Headings 52.05, 52.06 na 52.07 isipokuwa nyuzi za pamba zinazotambulika kwa HS Code 5205.23.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vinavyozalisha bidhaa hiyo na kuongeza thamani ya zao la pamba (value addition) nchini;

 

(h)   Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 35 kwenye milango na madirisha ya alluminium na chuma yanayoagizwa kutoka nje yanayotambulika kwa HS Codes 7610.10.00 na 7308.30.00. Lengo la hatua hii ni kulinda wajasiriamali wa ndani wanaotengeneza bidhaa hizo, kuongeza ajira pamoja na mapato ya Serikali;

 

(i)     Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwa utaratibu wa Duty Remission kutoka asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kutengeneza viongeza ladha kwenye vyakula na vinywaji (food flavors) zinazotambulika kwa HS Code 1901.90.10; 3302.10.00; na 3505.10.00. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa watengenezaji wa bidhaa hizo nchini;

 

(j)     Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwa utaratibu wa Duty Remission kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye karatasi zinazotambulika kwa HS Codes 4804.19.90; 4804.39.00; 4804.42.00; 4804.51.00; 4804.52.00; 4805.11.00; 4805.19.00; 4805.24.00; 4805.25.00; 4805.93.00; 4810.13.00; 4810.19.00; 4810.31.00; na 4810.32.00 zinazotumika kama malighafi ya kutengeneza vifungashio aina ya maboksi (corrugated boxes). Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wazalishaji wa vifungashio hivyo hapa nchini ili wananchi waweze kuvipata kwa urahisi na kwa bei nafuu;

 

(k)   Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwa utaratibu wa Duty Remission kutoka asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kutengeneza vioo vizito (toughened glass) zinazotambulika kwa HS Codes 7005.10.00; 7005.21.00; 7005.29.00; na 7005.30.00. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa watengenezaji wa vioo hivyo nchini;

 

(l)     Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwa utaratibu wa Duty Remission kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kutengeneza nyaya za umeme (electrical cables) zinazotambulika kwa HS Codes 7312.10.00; 7217.20.00; 7408.19.00; 7409.11.00; 7605.21.00; 2710.19.56; 3815.90.00; 5402.19.00; 5903.90.00; 7217.20.00; 7907.00.00; 7312.10.00; na 2712.10.00. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa watengenezaji wa nyaya hizo pamoja na kuvutia uwekezaji nchini;

 

(m)Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwa utaratibu wa Duty Remission kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kutengeneza sabuni (toilet soap) zinazotambulika kwa HS Code 3401.20.10. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wazalishaji wa sabuni nchini, kuongeza ajira na mapato ya Serikali;

 

(n)   Kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 25 badala ya kiwango cha asilimia 100 au dola za Marekani 460 kwa kila tani moja ya ujazo kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwa mwaka mmoja kwenye sukari ya matumizi ya kawaida (consumption sugar) inayoagizwa kutoka nje ya nchi kwa vibali maalum kwa lengo la kuziba pengo (gap) la uzalishaji hapa nchini;

 

(o)   Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwa utaratibu wa Duty Remission kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwenye hema za chuma (Prefabricated building) zinazotambulika kwa HS Code 9406.20.90 zitakazoagizwa na wafugaji, kwa mwaka mmoja. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwenye sekta ya mifugo, kuvutia uwekezaji, kuongeza ajira, pamoja na mapato ya Serikali kutokana na uwekezaji;

 

(p)   Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 35 kwenye nywele bandia zinazotambulika kwa Heading 6704. Hatua hii inalenga kulinda wazalishaji wa ndani wa bidhaa hizo, kuongeza ajira pamoja na kuongeza mapato ya Serikali;

 

(q)   Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 kwenye mafuta mengineyo ya petroli yanayotambulika kwa HS Code 2710.19.10. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu na kulinda watumiaji wa bidhaa hii;

 

(r)    Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 35 kwenye sigara za kielektroniki zinazotambulika kwa HS Code 8543.40.00. Lengo la hatua hii ni kulinda mnyororo wa thamani wa zao la tumbaku nchini, kulinda viwanda vya ndani, pamoja na kuongeza ajira;

 

(s)    Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kufanya marekebisho kwenye tafsiri (descriptions) ya HS Codes 7310.29.20 na 7612.90.10 ambapo awali zilikuwa zinatafsiri makasha ya kuhifadhia vinywaji pekee ambayo ushuru wa forodha ni asilimia 0 na sasa kujumuisha makasha ya kuhifadhia chakula ili yaweze kutozwa ushuru wa forodha kwa kiwango cha asilimia 0 badala ya asilimia 25. Lengo la marekebisho hayo ni kutoa unafuu kwenye vifungashio vya vyakula ili kulinda walaji.

 

(ii)       Mapendekezo ya kuendelea na utekelezaji wa Viwango vya Ushuru wa Forodha vya mwaka 2021/22 ni kama ifuatavyo; -

(a)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi zinazotumika katika uzalishaji wa vifaa maalum vinavyotumika katika kupambana na ugonjwa wa homa kali ya mapafu (UVIKO-19) vikiwemo barakoa (Masks), kipukusi (sanitizer), mashine za kusaidia kupumua (ventilators), na mavazi maalum ya kujikinga yanayotumiwa na madaktari na wahudumu wa afya (PPE). Msamaha huu utatolewa kwa utaratibu wa duty remission”. Hatua hii inalenga kutoa unafuu kwa wazalishaji wa vifaa hivyo hapa nchini ili kuongeza kasi katika kupambana na ugonjwa huo;

 

(b)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye mashine za kielektroniki zinazotumika kukusanya mapato ya Serikali (Cash registers, Electronic Fiscal Device (EFD) Machines and Point of Sale (POS) machines) zinazotambulika kwa HS Code 8470.50.00 na 8470.90.00. Lengo la hatua hii ni kuhamasisha matumizi ya vifaa hivi katika kuhasibu mapato ya Serikali;

 

(c)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vinavyotumiwa na wazalishaji wa maziwa kwa joto la juu yanayodumu kwa muda mrefu (UHT Milk) vinavyotambulika kwa HS code 4819.50.00. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wazalishaji wa maziwa hapa nchini. Utaratibu wa Duty Remission utatumika kutoa unafuu huo;

 

(d)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka kiwango cha asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifuniko vya chupa za mvinyo (corks and stoppers) vinavyotambulika kwa HS Code 4503.10.00 kwa kuzingatia kuwa havizalishwi hapa nchini. Hatua hii inalenga kuwapunguzia gharama wazalishaji wa mvinyo ili kuhamasisha na kuendeleza kilimo cha zao la zabibu nchini pamoja na ajira. Utaratibu wa Duty Remission utatumika kutoa unafuu huo;

 

(e)           Kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 0 hadi asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwenye unga wa kakao unaoingizwa kutoka nje unaotambulika kwa HS Code 1805.00.00. Lengo ni kuchochea na kuhamasisha kilimo cha zao la kakao nchini pamoja na kuongeza mapato ya Serikali;

 

(f)             Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya kuhifadhia kahawa vinavyotumiwa na viwanda vya kusaga kahawa nchini. Vifungashio vitakavyohusika ni vile vinavyotambulika kwa HS codes 7310.21.00; 6305.10.00; 3923.50.10; 3923.50.90 na 3920.30.90. Hatua hii inalenga kuongeza thamani kwenye zao la kahawa na kuvipa unafuu wa gharama viwanda vinavyosaga kahawa hapa nchini. Utaratibu wa “Duty Remission utatumika katika kuagiza vifungashio hivyo;

(g)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya kuhifadhia korosho. Vifungashio vitakavyohusika ni vile vinavyotambulika katika HS code 3923.21.00. Hatua hii inalenga kuongeza thamani kwenye zao la korosho na kuvipa unafuu wa gharama viwanda vinavyochakata korosho hapa nchini. Aidha utaratibu wa “Duty Remission” utatumika katika kuagiza vifungashio hivyo;

 

(h)          Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya kuhifadhia pamba (cotton lint). Vifungashio vitakavyohusika ni vile vinavyotambulika kama HS codes 3920.30.90; 6305.39.00 na 7217.90.00. Hatua hii inalenga kuvutia uwekezaji ili kuongeza thamani ya zao la pamba nchini;

 

(i)             Kupunguza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 0 kwa mwaka mmoja kutoka kiwango cha awali cha asilimia 25 kwenye malighafi za kutengeneza taulo za watoto (Baby Diapers) zinazotumbulika kwa HS code 3506.91.00 Hot Melt Adhesive; PE film HS Code 3920.10.90, Empty bag for Baby Diapers HS Code 6305.33.00, Plastic cask HS Code 3926.90.90; na kiwango cha awali cha asilimia 10 kwenye Super Absorbent Polymer HS Code 3906.90.00, Wet strength paper HS Code 4803.00.00, Non-woven HS Code 5603.11.00, Polyethylene laminated Nonwovens HS Code 5903.90.00, Spandex HS Code 5402.44.00 na Dust free paper HS Code 4803.00.00. Aidha, msamaha huu utatolewa kwa utaratibu wa Duty Remission”. Hatua hii inalenga kutoa unafuu wa gharama za uzalishaji na kuongeza ajira;

 

(j)             Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifaa vinavyotumika katika kukata, kungarisha na kuongeza thamani ya madini ya vito vinavyotambulika kwa HS Codes 6804.10.00; 7018.90.00; 7020.00.99; 3606.90.00; 6813.20.00; 8202.20.00; 8202.99.00; 8203.20.00; 8205.10.00; 8423.89.90; 8513.10.90; na 9002.19.00. Hatua hii inalenga kuchochea uongezaji wa thamani kwenye madini, kukuza ajira pamoja na kuongeza mapato ya Serikali. Utaratibu wa Duty Remission” utatumika katika kuagiza vifaa hivyo;

 

(k)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya mbegu vinavyotambulika kwa HS codes 3923.29.00; 6305.10.00; 4819.40.00; 7310.29.90; 6305.33.00; 6305.20.00; 6304.91.90 na 7607.19.90. Utaratibu utakaotumika kutoa unafuu huo ni wa “Duty Remission”. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wazalishaji wa mbegu hapa nchini; 

 

(l)             Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 10 au dola za Marekani 125 kwa kila tani moja ya ujazo (Metric ton) kwenye bidhaa za chuma kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa badala ya ushuru wa asilimia 10 kwa mwaka mmoja. Bidhaa hizo ni Flat -rolled products of iron or non-alloy steel and other alloy steel.  Bidhaa hizi zinatambulika kwa HS Codes 7209.16.00; 7209.17.00; 7209.18.00; 7209.26.00; 7209.27.00; 7209.28.00; 7209.90.00; 7211.23.00; 7211.90.00; 7225.50.0 na 7226.92.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vya hapa nchini, kukuza ajira pamoja na kudhibiti udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo kutoka nje;

 

(m)        Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 250 kwa kila tani moja ya ujazo (metric ton) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa badala ya ushuru wa asilimia 25 au dola za Marekani 200 kwa kila tani moja ya ujazo (metric ton) kwa mwaka mmoja kwenye bidhaa za mabati zinazotambulika kwa HS codes 7210.30.00; 7210.49.00; 7210.61.00; 7210.69.00; 7210.70.00 na 7210.90.00. Lengo la hatua hii ni kuwalinda wazalishaji wa bidhaa hizo hapa nchini kutokana na ushindani wa nje;

 

(n)          Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 10 au dola za Marekani 250 kwa kila tani moja ya ujazo (Metric ton) kwa mwaka mmoja kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwenye bidhaa za mabati zinazotambulika katika HS Code 7212.60.00 badala ya ushuru wa asilimia 10 pekee. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vya ndani kutokana na udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo zinapoingizwa kutoka nje (under-invoicing and under valuation), pamoja na kulinda ajira na mapato ya Serikali;

       

(o)           Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 250 kwa kila tani moja ya ujazo (Metric ton) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa badala ya ushuru wa asilimia 25 au dola za Marekani 200 kwa kila tani moja ya ujazo (Metric ton) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwa mwaka mmoja kwenye bidhaa za mabati zinazotambulika kwa HS Code 7212.30.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vya ndani kutokana na udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo zinapoingizwa kutoka nje (under-invoicing and under valuation), pamoja na kulinda ajira na mapato ya Serikali;

 

(p)           Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 250 badala ya kiwango cha asilimia 25 au dola za Marekani 200 kwa kila tani moja ya ujazo (metric ton) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwenye bidhaa za chuma (Reinforment bars and hallow profile) kwa mwaka mmoja. Hatua hii inahusu bidhaa zinazotambulika kwa HS Codes 7213.10.00; 7213.20.00; 7213.99.00; 7306.30.00; 7306.50.00; 7306.61.00; 7306.69.00; na 7306.90.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vinavyozalisha nondo hapa nchini kutokana na udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo zinapoingizwa kutoka nje (under-invoicing and under declaration), pamoja na kulinda ajira na mapato ya Serikali;

 

(q)           Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 250 badala ya kiwango cha asilimia 10 kwenye bidhaa za chuma (Flat-rolled products of other alloy steel, of a width of 600 mm or more) zinazotambulika kwa HS Codes 7225.91.00; 7225.92.00; na 7225.99.00 kwa mwaka mmoja. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vinavyozalisha nondo hapa nchini kutokana na udanganyifu wa thamani halisi ya bidhaa hizo zinapoingizwa kutoka nje (under-invoicing and under declaration), pamoja na kulinda ajira na mapato ya Serikali,

 

(r)            Kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 0 hadi asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwenye bidhaa za fito za plastiki zijulikanazo kama PVC Profiles zinazotambulika kwa HS Codes 3916.10.00; 3916.20.00; na 3916.90.00 ambazo hutumika kutengenezea fremu za milango, madirisha n.k. Lengo la hatua hii ni kuongeza mapato ya Serikali;

 

(s)           Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 badala ya asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwenye karatasi zinazozalishwa na viwanda vya hapa nchini ambazo zinatambulika kwa HS code 4804.29.00. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vinavyozalisha karatasi hizo hapa nchini;

 

(t)            Kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 10 badala ya asilimia 35 kwa mwaka mmoja kwenye ngano inayotambulika kwa HS Codes 1001.99.10 na 1001.99.90 kwa utaratibu wa “Duty Remission” ambapo wanaonufaika na unafuu huu ni wenye viwanda vya kusaga ngano. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama kwa viwanda vinavyozalisha unga wa ngano ili kurahisisha upatikanaji wa bidhaa za ngano kwa bei nafuu;

 

(u)          Kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 0 kutoka kiwango cha awali cha asilimia 25 kwa mwaka mmoja kwa utaratibu wa Duty Remission kwenye bidhaa ijulikanayo kama “Printed Alluminium Barrier Laminates” (ABL) HS Code 3920.10.90 ambayo hutumika kama malighafi ya kutengeneza vifungashio vya dawa ya meno kwenye viwanda vya ndani. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu wa gharama kwa viwanda vinavyozalisha dawa ya meno nchini;

 

(v)           Kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 0 kutoka kiwango cha awali cha asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwa utaratibu wa “Duty Remission” kwenye malighafi ya kutengeneza sabuni ijulikanayo kama RBD Palm Stearin HS Code 1511.90.40 kwa viwanda vinavyotengeneza sabuni nchini. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa viwanda vya kuzalisha sabuni nchini;

 

(w)         Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 1.35 kwa kila kilo moja ya viberiti (safety match boxes) vinavyotambuliwa kwenye HS code 3605.00.00 kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa badala ya asilimia 25 pekee kwa mwaka mmoja. Lengo la hatua hii ni kulinda viwanda vinavyozalisha viberiti nchini dhidi ya bidhaa zenye ruzuku kutoka nje na hivyo kuwa na ushindani sawa katika soko;

 

(x)           Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 25 au dola za Marekani 350 kwa kila tani moja ya ujazo (Metric ton) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwa mwaka mmoja kwenye bidhaa za chuma za misumari zinazotambulika kwa HS code 7317.00.00 (nails, tacks, drawing pins, corrugated nails, and staples other than those of heading 83.05) badala ya asilimia 25 pekee. Hatua hii inalenga kulinda viwanda vinavyozalisha bidhaa hizo nchini.

 

(y)           Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 60 badala ya asilimia 35 kwa mwaka mmoja kwenye maji ya kunywa (mineral water) yanayotambulika kwa HS code 2201.10.00. Hatua hii inalenga kulinda viwanda vinayvozalisha maji ya kunywa nchini;

 

(z)            Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 10 badala ya asilimia 0 kwenye Gypsum Powder inayotambulika kwa HS code 2520.20.00 kwa mwaka mmoja. Lengo la hatua hii ni kulinda wazalishaji wa Gypsum Powder nchini;

 

(aa)      Kutoza Ushuru wa Forodha wa asilimia 35 kwa mwaka mmoja kwenye mitumba inayoingia kutoka nje badala ya asilimia 35 au dola za Marekani 0.40 kwa kilo moja kutegemea kiwango kipi kikubwa kwa lengo la kutoa unafuu kwa watumiaji nchini;

 

(bb)      Kutoa unafuu wa Ushuru wa Forodha kwenye malighafi, vipuri na mashine vinavyotumika katika kutengeneza viatu vya ngozi na nguo. Lengo la hatua hii ni kuhamasisha ukuaji wa sekta ya nguo na viatu vya ngozi nchini;

 

(cc)       Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwenye mabasi ya abiria yanayotambulika kwa HS Codes 8702.10.99 na 8702.20.99 yanayoingizwa nchini kwa ajili ya mradi wa mabasi yaendayo haraka. Hatua hii inalenga kupunguza gharama za uingizaji wa mabasi hayo ili kurahisisha huduma ya usafiri kwa wananchi;

 

(dd)      Kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 10 hadi asilimia 25 kwa mwaka mmoja kwenye matairi mapya ya pikipiki (new pneumatic tyres of rubber) yanayotambulika kwa HS Code 4011.40.00. Lengo la hatua hii ni kuhamasisha uzalishaji wa matairi hayo nchini kwa kuwa kuna malighafi za kutosha;

 

(ee)       Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye nyaya (wire of other alloy steel) zinazotambulika kwa HS Codes 7229.20.00 na 7229.90.00. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama kwa wazalishaji wanaotumia bidhaa hiyo kama malighafi;

 

(ff)          Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye milk cans zinazotambulika kwa HS Codes 7310.10.00 na 7310.29.90. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu wa vifungashio vya kuhifadhia maziwa ili kuwalinda walaji nchini;

 

(gg)       Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye LABSA (Organic surface-active agents - Anionic) inayotambulika kwa HS Code 3402.11.00 kwa utaratibu wa Duty Remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wazalishaji wa sabuni za unga na maji nchini;

 

(hh)     Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kuchakata ngozi zinazotambulika kwa HS Codes 3208.20.00 na 3210.00.10 kwa utaratibu wa duty remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wachakataji wa ngozi nchini;

 

(ii)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kutengeneza mbolea zinazotambulika kwa HS Codes 2710.99.00, 2528.00.00 na 3505.20.00 kwa utaratibu wa Duty Remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wazalishaji wa mbolea nchini;

 

(jj)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya tumbaku iliyochakatwa vinavyotambulika kwa HS Code 5310.10.00 kwa utaratibu wa Duty Remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wachakataji wa tumbaku nchini;

 

(kk)      Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya chai iliyochakatwa vinavyotambulika kwa HS Codes 4819.20.90, 5407.44.00 na 3923.29.00 kwa utaratibu wa Duty Remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa wachakataji wa chai (tea blenders) nchini;

 

(ll)           Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 kwa mwaka mmoja kwa waunganishaji wa pikipiki za matairi matatu bila kujumuisha fremu ili ziweze kutengenezwa na kuunganishwa hapa nchini (CKD for three-wheel motorcycles excluding chassis and its components) zinazotambulika kwa HS Code 8704.21.90 kwa utaratibu wa Duty Remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa waunganishaji wa pikipiki hizo nchini ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo;

(mm) Kupunguza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 au asilimia 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye malighafi za kutengeneza mabomba ya plastiki (glass reinforced plastic pipes) zinazotambulika kwa HS Codes 3920.61.10, 7019.39.00, 7019.31.00, 6006.90.00, 7019.12.00, 3920.10.10, 4016.93.00, na 3907.91.00 kwa utaratibu wa duty remission. Lengo la hatua hii ni kutoa unafuu kwa watengenezaji wa mabomba hayo nchini ili kupunguza gharama za uzalishaji na kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya maji; na

 

(nn)     Kutoza Ushuru wa Forodha kwa kiwango cha asilimia 10 kutoka kiwango cha asilimia 100 au dola za Marekani 460 kwa kila tani moja ya ujazo (metric tone) kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa kwa mwaka mmoja kwenye sukari ya matumizi ya viwandani (sugar for industrial use) inayoagizwa kutoka nje ya nchi. Lengo la hatua hii ni kuwezesha na kutoa unafuu kwenye viwanda vinavyotumia bidhaa hii kama malighafi.

 

(iii)    Mawaziri wa Fedha wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki walikubaliana kiwango cha juu cha ushuru wa forodha cha zaidi ya asilimia 25 kuwa ni asilimia 35. Hivyo, Muundo mpya wa ushuru wa forodha wa EAC utakuwa katika mpangilio wa viwango vinne (Four Tariff Bands) yaani asilimia 0, asilimia 10, asilimia 25 na asilimia 35 na utekelezaji wake utaanza tarehe 1 Julai 2022. Bidhaa zitakazo tozwa ushuru wa asilimia 35 ni pamoja na nyama, samaki, bidhaa za mbogamboga na matunda, mafuta ya kula, Chai, magunia ya kitani, kahawa, siagi ya karanga, soseji (sausages), nyanya zilizosindikwa (tomato sauces), saruji, chumvi, sabuni, rangi za majengo, vinywaji, vipodozi na urembo, bidhaa za samani, bidhaa za ngozi, bidhaa za chuma, marumaru, pamoja na bidhaa za sukari kama vile chingamu (chewing gum), biskuti, peremende, na chokoleti (chocolates).  

Hatua hizi kwa ujumla wake zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 66,791.

 

(o)  Utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Kufanya Biashara (Blueprint) kwa kurekebisha Ada na Tozo mbalimbali.

 

118.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufuta au kupunguza ada na tozo mbalimbali zinazotozwa na Wizara, Idara na Taasisi zinazojitegemea ili kuondoa kero na urasimu kwa wafanyabiashara na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji hasa katika kipindi hiki cha changamoto kubwa ya kiuchumi kufuatia kuenea kwa janga la UVIKO-19 na baadaye kuzuka kwa vita ya Urusi na Ukraine. Hatua hizi ni sehemu ya mwendelezo wa utekelezaji wa Mpango wa kuboresha Mfumo wa udhibiti wa Biashara (Blueprint for Regulatory Reforms to Improve the Business Environment). Marekebisho hayo yatajumuisha:

 

(i)     Wizara ya Mifugo na Uvuvi

 

(a)  Sekta ya Mifugo

Napendekeza kufanya marekebisho ya tozo mbalimbali kwenye sekta ya mifugo kama ilivyoanishwa katika Kiambatisho Namba 5; na

(b)  Sekta ya Uvuvi

Napendekeza kufanya marekebisho ya tozo mbalimbali kwenye sekta ya uvuvi kama ilivyoainishwa kwenye Kiambatisho Namba 6.

 

(ii)  Wizara ya Kilimo

(a)  Kufuta tozo ya shilingi 200 (impoundment fee) inayotozwa kwa kila mita ya mraba ya eneo la uso wa maji yaliyohifadhiwa kwenye mabwawa ya umwagiliaji. Hatua hii inalenga kupunguza gharama kwa wakulima wanaofanya kilimo cha umwagiliaji; na

(b)  Kuongeza ada ya kibali cha kusafirisha mbolea nje ya nchi kutoka dola za kimarekani 0.2 kwa tani hadi dola za kimarekani 0.5 kwa tani.  Lengo la hatua hii ni kuchochea uzalishaji wa mbolea nchini na kuongeza ajira. Hatua hii pia inaendana na dhima ya Serikali ya kuchochea maendeleo ya viwanda hapa nchini.

(iii)  Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Kuanzisha utaratibu wa kutoza ada ya shilingi 1,000 hadi 3,000 kwenye ada ya matumizi ya kingamuzi kulingana na kiwango cha matumizi.

 

(iv)   Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Napendekeza kuanzisha tozo ya asilimia 1.5 kwenye vifaa vinavyotumika kuzalisha, kusambaza, kudurufu na kutunza kazi za Sanaa, uandishi na ubunifu mwingine kama vile muziki, filamu, vitabu, picha na aina nyingine za kazi za ubunifu.  Vifaa hivi ni Radio/ TV set enabling recording; Analogue audio recorders; Analogue video recorders; CD/DVD Copier; Digital Jukebox na MP 3 Player.  Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 9,600.

 

(v)   Shirika la Viwango Tanzania

Kupunguza tozo ya kuthibitisha ubora wa shehena (Batch Certification Fee) za sukari zinazoingizwa nchini kutoka shilingi 6 kwa kilo hadi shilingi 2.5 kwa kilo. Lengo la hatua hii kupunguza gharama kwa waingizaji wa sukari nchini ili kutoa unafuu kwa wananchi.

(vi)   Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA)

Kufuta tozo ya kipimio cha mzio (peak expiratory flow test fee) inayotozwa shillingi 10,000 na tozo ya kipimo cha kilele (allergy test fee) inayotozwa shilingi 25,000. Pendekezo hili linatarajia kuchochea mazingira wezeshi ya biashara nchini hususan katika maeneo ya viwandani.

 

(vii)Tume ya nguvu za mionzi Tanzania

(a)  Kupunguza ada ya Utambuzi wa Mionzi kutoka asilimia 0.2 ya Malipwani kwenda asilimi 0.1 ya Malipwani kwenye mizigo yote ya vyakula inayosafirishwa nje ya nchi ikiwa pamoja na mbolea, tumbaku na bidhaa za tumbaku na chakula cha msaada kinachoingizwa nchini. Lengo la hatua hii ni kupunguza tozo kero na gharama za biashara na hivyo kuchochea mauzo ya bidhaa nje ya nchi sambamba na kupunguza utoroshaji wa mazao hayo kwenda nchi jirani kwa ajili ya kuuzwa nje ya nchi ; na

(b)  Kufanya Maboresho ya ada na tozo mbalimbali zinazotozwa na Tume ya Nguvu za Mionzi kama zilivyoainishwa kwenye kiambatisho Namba 7 ;

(viii)       Jeshi la Zimamoto na Uokoaji

Napendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Jeshi ya Zimamoto na Uokoaji Sura 427 kwa kupunguza ada na tozo mbalimbali kama zilivyoainishwa kwenye kiambatisho Namba 8. Lengo la hatua hii ni kupunguza tozo kero na gharama za biashara.

 

(ix)   Bodi ya Michezo ya Kubahatisha

Napendekeza kufanya marekebisho kwenye Jedwali la viwango vya tozo na ada la Kanuni za Michezo ya Kubahatisha chini ya Sheria ya Michezo ya Kubahatisha Sura Na. 41 kama ilivyoainishwa kwenye kiambatisho Na 9.

 

(x)   Idara ya Uhamiaji

Mwaka wa fedha 2021/22 Serikali ilipitisha uamuzi wa kuondoa ada ya kibali cha kuingia nchini (VISA/PASS FEE) kwa wanafunzi wa elimu ya juu kutoka nchi ya Msumbiji kwa ajili ya Mpango wa kubadilishana wanafunzi wa Elimu ya Juu baina ya Tanzania na Msumbiji (TAMOSE). Pamoja na uamuzi huo, napendekeza kuondoa tozo ya vibali vya ukaazi kwa wanafunzi wa elimu ya juu kutoka nchi ya Msumbiji. Lengo la hatua hii ni kutekeleza matakwa ya makubaliano kati ya nchi hiyo na Tanzania kuondoleana tozo hizo ambapo Msumbiji imeshaanza kutekeleza makubaliano hayo.

 

119.  Mheshimiwa Spika, napendekeza pia kufanya maboresho ya Sheria mbalimbali ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa kupunguza mwingiliano wa Sheria. Mapendekezo hayo ni kama ifuatavyo:

 

(i)            Kufuta kifungu cha 6(10) (b) (ii) na (iii) cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ili kuwa na viwango vya kitaifa (National Standards) kwa kuzingatia kifungu cha 4(3) cha Sheria ya Viwango Na. 2. Lengo la hatua hii ni kufanya jukumu la viwango vya kitaifa kubaki kwa Shirika la Viwango Tanzania pekee. Iwapo Mamlaka ya Mawasiliano itakuwa na mahitaji ya viwango, itashirikiana na Shirika la Viwango Tanzania;

 

(ii)          Kufuta kifungu cha 7 (1) (b) (ii) na (iii) cha Sheria ya Udhibiti wa Nishati na Maji, SURA 414 ili kubakisha jukumu la viwango vya kitaifa kubaki kwa Shirika la Viwango Tanzania pekee. Endapo kuna mahitaji ya viwango EWURA watawasiliana na Shirika la Viwango Tanzania;

 

(iii)       Kufuta Kifungu cha 5(1) (c) (i) na (ii) cha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu Na. 3 ili kazi ya viwango ifanywe na Shirika la Viwango Tanzania. Mahitaji ya viwango ya LATRA yatawasilishwa Shirika la Viwango Tanzania;

 

(iv)        Kufuta Kifungu cha 5(2) (c) cha Sheria ya Pamba Na. 2 ya mwaka 2001 ili kubakiza jukumu la viwango kwa Shirika la Viwango Tanzania. Mahitaji ya viwango vya Bodi ya Pamba Tanzania yatawasilishwa Shirika la Viwango Tanzania;

 

(v)          Kufuta Kifungu cha 12(1) (b) na (c) cha Sheria ya Wakala wa Meli Tanzania Na. 14 ya mwaka 2017 ili jukumu la viwango vya kitaifa libaki kwenye Sheria ya Viwango Na. 2 ya mwaka 2009. Mahitaji ya viwango ya TASAC yatawasilishwa Shirika la Viwango Tanzania;

 

(vi)        Kufuta Kifungu cha 5 (1) (l) cha Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Na. 1 ya mwaka 2003 ili jukumu la viwango vya kitaifa libaki kwenye Sheria ya Viwango Na. 2 ya mwaka 2009. Mahitaji ya viwango ya TMDA yatawasilishwa Shirika la Viwango Tanzania;

 

(vii)      Kufuta Kifungu cha 41 (1) cha Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Na. 1 ya mwaka 2003 ili kazi ya udhibiti wa machinjio ifanywe na Wizara ya Mifugo na Uvuvi pekee;

 

(viii)   Kufuta Kifungu cha 3(2) (g) cha Sheria ya Magonjwa na Wanyama Na. 17 ya mwaka 2003 ili chanjo zisajiliwe na TMDA pekee;

 

(ix)        Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 10 cha Sheria ya Tasnia ya Maziwa ili Bodi ya Maziwa iweze kufanya ukaguzi kwa kushirikiana na Shirika la Viwango Tanzania;

 

(x)          Kufanya marekebisho kwenye maginal note ya Kifungu cha 46 cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishirikishi ili kuondoa mgongano wa kimaslahi katika kutekeleza majukumu ya Chama Cha Hakimiliki Tanzania. Aidha, napendekeza kuondoa neno society na kuweka neno Copyright Office kwenye Kifungu cha 46, 47, 48 na jedwali lake;

 

(xi)        Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 51 cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishirikishi ili kuongeza sehemu mpya ya saba (PART VII) inayoweka hitaji la Collective Management Organisations kutoa taarifa ya hesabu zao zilizokaguliwa kwa Copyright Office kila mwaka na hivyo kuwa na uwajibikaji na kuimarisha usimamizi wa masuala yanayohusu Hakimiliki na Hakishirikishi;

 

(xii)     Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 5(2) cha Sheria ya Tasnia ya Pamba SURA 201 ili jukumu la kusimamia viwango vya pamba lifanywe na Shirika la Viwango Tanzania pekee;

 

(xiii)   Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 23 cha Sheria ya Utalii SURA, 65 ili kumpa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii mamlaka ya kutoa vibali baada ya kuridhiwa na Bodi;

 

(xiv)   Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 28 cha Sheria ya Mbolea SURA, 378 ili jukumu la kuandaa kanuni za viwango litekelezwe na Shirika la Viwango Tanzania pekee;

 

(xv)      Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 17 cha Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, SURA 297 ili kuweka sharti la OSHA kutoa leseni ndani ya siku 7 baada ya mwombaji kukidhi vigezo;

 

(xvi)   Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 35 cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Urban Authority) SURA, 287 ili kuweka sharti la Mamlaka za Miji kuanzisha vituo vya pamoja kwa ajili ya uratibu, uhamasishaji na uboreshaji wa mazingira ya ufanyaji biashara;

 

(xvii) Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 113 cha Sheria ya Serikali za Mitaa (District Authorities) SURA 288 ili kuweka kuweka sharti la Mamlaka za Vijiji kuanzisha vituo vya pamoja kwa ajili ya uratibu, uhamasishaji na uboreshaji wa mazingira ya ufanyaji biashara;

 

(xviii)  Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 6, 7, na 8 cha Sheria ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa SURA, 290 ili kupunguza kiwango cha tozo ya kitanda siku (hotel levy) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 5; na

 

(xix)   Kufanya marekebisho kwenye Kifungu cha 3 cha Sheria ya Ngozi na Bidhaa za Ngozi SURA, 120 ili kuondoa mkanganyiko uliopo kati ya ngozi za wanyama wa majumbani na za wanyama pori.

 

(p)   Marekebisho madogo madogo katika baadhi ya Sheria za Kodi na   Sheria nyingine mbalimbali.

 

120.  Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho mengine madogo madogo yasiyo ya kisera katika sheria mbalimbali za kodi pamoja na sheria nyingine ili ziwe sanjari na azma ya kurahisisha utekelezaji wake. Marekebisho hayo yataainishwa katika Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2022 na Matangazo ya Serikali (Government Notices).

 

121.  Mheshimiwa Spika, sambamba na hatua zilizobainishwa hapo juu, napendekeza kutoa tamko la biashara ya bima nchini kufanywa kwa ushindani kwa kufuata misingi ya soko huria kama ilivyo kwa biashara nyingine na kuyaelekeza mashirika ya bima yanayomilikiwa na Serikali ambayo ni Shirika la Bima la Taifa (NIC) na Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) kufanya  biashara kiushundani kwa kutoa huduma bora tofauti na maelekezo yaliyopo sasa yanayoipatia NIC pekee fursa ya kupata biashara kutoka kwenye Taasisi za Umma.  

 

(q)  Tarehe ya Kuanza Kutekeleza Hatua Mpya za Kodi.

 

122.  Mheshimiwa Spika, hatua hizi za kikodi zinazopendekezwa zitaanza kutekelezwa tarehe 1 Julai, 2022, isipokuwa pale itakapoelezwa vinginevyo.

VI.                          SURA YA BAJETI KWA MWAKA 2022/23

123.  Mheshimiwa Spika, Sura ya Bajeti kwa mwaka 2022/23 inaonesha kuwa jumla ya shilingi trilioni 41.48 zinatarajiwa kukusanywa na kutumika. Jumla ya mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa shilingi trilioni 28.02, sawa na asilimia 67.5 ya bajeti yote. Kati ya mapato hayo, mapato yatakayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania yanakadiriwa kuwa shilingi trilioni 23.65 na mapato yasiyo ya kodi (Wizara, Idara, Taasisi na Mamlaka za Serikali za Mitaa) yanakadiriwa kuwa shilingi trilioni 4.37.

 

124.  Mheshimiwa Spika, misaada na mikopo nafuu kutoka kwa Washirika wa Maendeleo inatarajiwa kuwa shilingi trilioni 4.65, sawa na asilimia 11.2 ya bajeti yote. Aidha, Serikali inatarajia kukopa shilingi trilioni 5.78 kutoka soko la ndani ambapo shilingi trilioni 3.30 ni kwa ajili ya kulipia hatifungani na dhamana za Serikali zinazoiva na kiasi cha shilingi trilioni 2.48 ni kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo. Vilevile, Serikali inatarajia kukopa shilingi trilioni 3.03 kutoka soko la nje kwa masharti ya kibiashara kwa lengo la kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

125.  Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali inapanga kutumia jumla ya shilingi trilioni 41.48 kwa matumizi ya kawaida na maendeleo. Kati ya kiasi hicho, shilingi trilioni 26.48 zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikiwa ni asilimia 63.8 ya bajeti yote, ikijumuisha shilingi trilioni 11.31 kwa ajili ya ulipaji wa deni la Serikali na gharama nyingine za Mfuko Mkuu na shilingi trilioni 9.83 kwa ajili ya mishahara ikiwemo nyongeza ya mshahara, upandishaji wa madaraja kwa watumishi na ajira mpya. Aidha, shilingi trilioni 5.34 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo (OC) ikijumuisha shilingi bilioni 200.0 kwa ajili ya kulipa madeni yaliyohakikiwa ya watumishi na wazabuni.

 

126.  Mheshimiwa Spika, matumizi ya maendeleo yanatarajiwa kuwa shilingi trilioni 15.0, sawa na asilimia 36.2 ya bajeti yote. Kati ya kiasi hicho, shilingi trilioni 12.31 ni fedha za ndani, sawa na asilimia 82.0 ya bajeti ya maendeleo na shilingi trilioni 2.70 ni fedha za nje. Fedha za maendeleo za ndani zinajumuisha: shilingi trilioni 1.11 kwa ajili ya kugharamia mradi wa ujenzi wa reli kwa kiwango cha Standard Gauge; shilingi trilioni 1.44 kwa ajili ya kugharamia mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere; shilingi trilioni 1.18 kwa ajili ya Mfuko wa Barabara; shilingi bilioni 944.1 kwa ajili ya mifuko ya Reli, Maji na REA; shilingi bilioni 570.0 kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu; shilingi bilioni 230.0 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya madeni yaliyohakikiwa ya wakandarasi; na shilingi bilioni 346.5 kwa ajili ya kugharamia elimumsingi bila ada.

 

127.  Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia mfumo wa bajeti kama nilivyoeleza hapo awali, sura ya bajeti kwa mwaka 2022/23 ni kama inavyooneshwa katika Jedwali Na.1.

 

 


Jedwali Na 1: Mfumo wa Bajeti Kwa Mwaka 2022/23

Chanzo:Wizara ya Fedha na Mipango


VII.                         HITIMISHO

 

128.  Mheshimiwa Spika, maendeleo endelevu ya Taifa lolote duniani hujengwa kwa ushiriki wa wananchi wote chini ya uongozi madhubuti na shupavu. Bajeti hii ni muendelezo wa kuiishi dhana hiyo kwani imeandaliwa kwa kushirikisha makundi yote katika jamii yetu ya Tanzania. Makundi hayo ni wawakilishi wa wananchi ambao ni Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sekta binafsi, Washirika wa Maendeleo, watalaamu mbalimbali kutoka taasisi za umma na binafsi pamoja na wananchi wa kawaida. Maoni yaliyowasilishwa na makundi hayo yamesaidia kuboresha maandalizi ya bajeti hii katika kupanga vipaumbele na sera zinazolenga kutatua changamoto mbalimbali katika nchi yetu. Kwa msingi huo, ni dhahiri kabisa hii ni “Bajeti ya Wananchi, ni “Bajeti Yetu Wote” kwa ajili ya maendeleo yetu.

 

129.  Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kusema hapo awali, bajeti ya mwaka 2022/23 inalenga kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuimarisha sekta za uzalishaji kwa ajili ya kuboresha maisha, hivyo nguvu kubwa itaelekezwa katika maeneo hayo chini ya kaulimbiu ya Kazi Iendelee”.

130.  Mheshimiwa Spika, pamoja na vipaumbele nilivyoviainisha awali, wote tunafahamu kuwa tafsiri ya dhana ya ukuaji wa uchumi ni lazima ifungamane na maendeleo ya mtu mmoja mmoja na familia za Watanzania wote na tunajua kuwa, Mama hawezi kumuacha mwanae apate tabu, Mama ana huruma, Mama anajali na Mama ana upendo kwa wanae”. Hivyo, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya “MAMA YETU” Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imehakikisha kuwa, bajeti hii inaenda kugusa na kuboresha maisha ya watanzania wa hali zote kwa kuboresha sekta za uzalishaji. Hii itasaidia kuongeza ajira na vipato, kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo mfumuko wa bei uliotokana na mabadiliko ya kiuchumi duniani na athari za mabadiliko ya tabianchi.

 

131.  Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kujenga misingi ya Taifa letu kujitegemea kiuchumi. Matunda ya mikakati hiyo yatafikiwa na kutunufaisha wote ikiwa kila mtanzania kwa nafasi yake atashiriki kwenye shughuli za uzalishaji mali zinazofuata sheria za nchi na kuchangamkia fursa za kiuchumi ili kujiongezea kipato na kuongeza mapato ya ndani ya Serikali. Hivyo, nawahimiza wananchi wote, taasisi za umma na binafsi kudai risiti sahihi wanapofanya ununuzi wa bidhaa na huduma ili kuhakikisha kuwa Serikali inakusanya kodi stahiki kutoka kwenye shughuli zinazofanyika. Vilevile, nawahimiza wafanyabiashara na kampuni zote kuwajibika kwa hiari katika ulipaji wa kodi kwa Serikali kutokana na shughuli wanazozifanya.

 

132.  Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa namna anavyomsaidia Rais kutekeleza majukumu ya kuiletea maendeleo nchi yetu. Aidha, napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa uongozi wake shupavu na nia yake thabiti ya kuleta maendeleo Zanzibar. Napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kusimamia na kuratibu kazi za kila siku za Serikali na utendaji wa Serikali Bungeni kwa umahiri mkubwa pamoja na kumsaidia vyema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuliletea Taifa letu maendeleo. Vile vile, ninampongeza Mheshimiwa Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi kwa kutayarisha kwa wakati Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2022 na Muswada wa Sheria ya Matumizi ya Mwaka 2022.

 

133.  Mheshimiwa Spika, naomba nikupongeze wewe binafsi kwa kuwa mwanamke wa pili kushika uongozi wa Mhimili huu wa Bunge. Kipekee, nampongeza Naibu Spika ambaye ameungana nawe kuchaguliwa kwa kishindo katika nafasi za kuliongoza Bunge letu Tukufu. Tunategemea kuwa umakini, weledi, busara na hekima kubwa mliyodhihirisha katika nafasi mlizokuwa nazo zitaendelea kukua zaidi mnapotekeleza wajibu wenu katika nafasi hizi kubwa zaidi. Vilevile, nawapongeza Wenyeviti wa Bunge kwa kusimamia kwa ustadi wa hali ya juu kazi waliyopewa ya kuongoza vikao vya Bunge letu, kwa hakika mmekuwa msaada mkubwa sana katika uendeshaji wa Bunge kwa ujumla. Vilevile, naomba kutoa pongezi zangu za dhati kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Daniel Baran Sillo - Mbunge wa Babati Vijijini pamoja na Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua - Mbunge wa Kilindi kwa maoni na ushauri wao mzuri katika kuboresha utendaji wa Wizara pamoja na maandalizi ya Mpango na Bajeti kwa mwaka 2022/23.

 

134.  Mheshimiwa Spika napenda kumpongeza Mheshimiwa Profesa Ibrahimu Hamisi Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania kwa kazi nzuri ya kuongoza mhimili wa Mahakama. Kazi yenu ni nzuri sana na ni ya muhimu sana kwenye usitawi wa jamii, upendo na amani ya nchi. Neno la Mungu linasema, HAKI HUINUA TAIFA, BALI DHAMBI NI AIBU YA WATU WOTE (MITHALI 14;34). Endeleeni kusimamia sheria na kutenda haki mtekelezapo majukumu yenu. Niwapongeze vyombo vya Ulinzi na Usalama vikiongozwa na JWTZ kwa kazi nzuri mnazozifanya, mmeiheshimisha Nchi yetu na kuifanya kuwa nchi ya tofauti duniani kote. Mheshimiwa Rais ambaye ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kila wakati anatuelekeza Wizara ya Fedha na Mipango tutekeleze bajeti zenu sawasawa na mahitaji yenu ili mtekeleze majukumu yenu kwa manufa ya watanzania wote, nasi tutaendelea kufanya hivyo.

 

135.  Mheshimiwa Spika, nawashukuru waheshimiwa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu Kiongozi, Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na wataalam wa Wizara zote na Taasisi za Serikali kwa michango waliyotoa ili kukamilisha Bajeti hii. Kwa unyenyekevu mkubwa, nawashukuru viongozi na waumini wa dini zote kwa kuendelea kuliombea Taifa letu. Aidha, naomba nitumie nafasi hii kuwaomba viongozi na waumini wa dini zote kuendelea kumuombea Rais wetu pamoja na viongozi wote wa Serikali ya Awamu ya Sita, Mungu aendelee kuwajalia afya njema, hekima, unyenyekevu na dhamira njema katika kusimamia rasilimali za nchi yetu katika utekelezaji wa majukumu yao.

 

136.  Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Mheshimiwa Khamad Hassan Chande, Mbunge wa Jimbo la Kojani, ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, kwa ushirikiano na msaada anaonipatia katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Fedha na Mipango. Aidha, napenda kumshukuru Bw. Emmanuel Mpawe Tutuba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali kwa usimamizi wa kazi za kila siku za Wizara na uratibu mzuri wa maandalizi ya Bajeti hii, akisaidiwa na Naibu Makatibu Wakuu. Ninawashukuru pia wakuu wa taasisi nyingine zilizo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango; Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara; pamoja na watumishi wote wa Wizara na taasisi zake kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kukamilisha Bajeti hii.

 

137.  Mheshimwa Spika, nipende kuwashukuru Washirika wa Maendeleo kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya sita katika kuwaletea maendeleo wananchi wake. Washirika wanaotarajiwa kuchangia bajeti ya Serikali  ya mwaka 2022/23 ni pamoja na: Serikali za Canada, China, Denmark, Finland, India, Ireland, Italia, Japan, Korea ya Kusini, Marekani, Norway, Poland, Sweden, Ubelgiji, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani na Uswisi. Aidha, Mashirika na Taasisi za Kimataifa zinazotarajiwa kuchangia bajeti hii ni Benki ya Maendeleo ya Afrika, Benki ya Dunia, Shirika la Fedha la Kimataifa, Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Kiuchumi Katika Afrika, Mfuko wa Abu Dhabi, Mfuko wa Kuwait, Mfuko wa Kimataifa wa Kusaidia Mapambano Dhidi ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria, Umoja wa Ulaya, Benki ya Uwekezaji ya Ulaya, Umoja wa Mataifa na mashirika yote yaliyopo chini yake, Mfuko wa OPEC kwa Maendeleo ya Kimataifa, pamoja na Shirikisho la GAVI. Vilevile, ninapenda kuyatambua Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya ndani na nje ya nchi kwa michango yao kwenye sekta za kijamii kwa ajili ya ustawi wa watu wetu. Ninapenda kuwathibitishia kuwa, Serikali inathamini michango yenu na itaendelea kufungua fursa za ushirikiano.

 

138.  Mheshimiwa Spika, ninapoelekea kuhitimisha, nitumie fursa hii kuipongeza sana timu ya Yanga kwa mwenendo wao mzuri sana mwaka huu na nitumie fursa hii kumwomba radhi Bosi wangu Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kitendo alichowafanyia mwanangu FEI TOTO kule Mwanza. Mniwie radhi, nilipompeleka FEI TOTO Yanga sikujua atakuja kuwafanyia kitumbaya hivi, mpaka nasikia anatafutwa maliasili eti kaua mnyama bila kibali. Nakupongeza Mheshimiwa Anthony Mavunde wewe ndio ulikuwa Mwenyekiti wa kuisaidia Yanga ikiwa na mapito. Nampongeza GSM kwa kurejesha furaha ya wananchi hasahasa kwa udajili wa Fiston Mayele. Mayele amekuwa maarufu kuliko Makatibu wenezi wa baadhi ya vyama vya Siasa. Nawapongeza sana na marafiki zangu klabu ya Simba kwa kuwakilisha vyema kwenye mashindano ya Kimataifa, wananijua mara zote kimataifa tuko pamoja, siwezi kukana Bendera ya Taifa langu kwa ajili ya utani wa jadi.

139.  Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kuendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uwezo wa kuwasilisha hotuba hii. Kwa moyo wa dhati napenda kuishukuru familia yangu, mke wangu NEEMA NCHEMBA na watoto wangu, leo yupo Joshua MWIGULU na Mdogo wangu Peripetua Madelu, kwa kuendelea kunitia moyo na kuniombea wakati wote ninapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yangu. Vilevile, nitumie fursa hii kuwashukuru kwa dhati wananchi wa Jimbo la Iramba Magharibi kwa kuendelea kunipa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yangu ya ubunge. Kadhalika, nawashukuru Waheshimiwa Wabunge na Watanzania Wote kwa kunisikiliza.

 

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA. KAZI IENDELEE!

 

 

140.  Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.




 



 


 

 


 


 

Kiambatisho Na. 5

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

THIRTEENTH SCHEDULE

(Made under Regulation 22)

 

IMPORT AND EXPORT FEE FOR ANIMAL AND ANIMAL PRODUCTS

Serial

No.

Animal / Animal products

Unit of charge

Import fees

(Tshs)

Export fees

(Tshs)

 

 

 

Current

Proposed

Current

Proposed

1

Cattle

Each

10,000

0

25,000

25,000

2

Sheep/goat

Each

7,000.00

0

5,000.00

5,000.00

3

Pigs

Each

7,000.00

0

10,000.00

10,000.00

4

Mule/Donkeys

Each

5,000.00

0

30,000.00

30,000.00

  10

Poultry

 

 

 

 

 

 

(A)Parent Stock

 

(i)  Parent stock DOC

Each

30.00

0

20.00

20.00

 

(i)  Hatching eggs

Each

20.00

0

10.00

10.00

 

(C) Table eggs

Per tray (30 eggs)

5,000.00

5,000.00

100.00

10.00

 

 

(D) Poultry: adult chicken/guinea fowls

Each

500.00

500.00

200.00

20.00

19

Meat

 

(i)     Beef

Kilogram (Kg) for imports, Consignment for exports

4,000.00

 

3,000.00

40,000.00

40,000.00

 

(ii)   Mutton/ chevon

Kilogram (Kg) for imports, Consignment for exports

4,000.00

 

3,000.00

40,000.00

40,000.00

 

(iii) Pork /bacon/lard

Kilogram (Kg) for imports,

Consignment for exports

4,000.00

3,000.00

20.00

20.00

 

(iv) Chicken meat

Kilogram (Kg) for imports,

Consignment for exports

4,000.00

 

3,000.00

40,00.000

40,000.00

 

(v)   Game Meat

Kilogram (Kg)

4,000.00

4,000.00

500.00

500.00

21

Milk

 

 

 

 

 

 

(i)  Pasteurized whole milk

Litre

2,000.00

1000.00

100.00

50.00

 

(ii)        Skimmed

Litre

2,000.00

1000.00

100.00

50.00

 

(iii)      Yoghurt

Litre

2,000.00

1000.00

50.00

50.00

 

(iv)      Powdered

Kilogram (Kg)

2,000.00

1000.00

100.00

50.00

28

Incubator

Permit

50,000.00

0.00

10,000.00

0.00

30

Livestock Identification items including ear tags and ear tags aplicatiors

Permit

50,000.00

0.00

50,000.00

0.00

 

b). by deleting item 41, 42, 43, 44 and 45 of the thirteenth schedules. Recommended

c). by re-arranging item 46 to be 41Recommended

 

 

1.  The principal Regulations are amended by deleting item 1 for registration in the Fifteenth Schedule and improve item 3 by adding a word ‘grazing fee”.

 

 

FIFTEENTH SCHEDULE

(Made under regulation 21)

FEE FOR QUARANTINE, ANIMAL HOLDING GROUNDS AND CHECK POINTS

S/N

SERVICE

ANIMAL

FEES (Tshs)

 

 

 

Current

Proposed

1

Registration

Cattle

500.00

0.00

 

 

Sheep/Goat

500.00

0.00

 

 

Horse/Donkey

500.00

0.00

 

 

Camel

500.00

0.00

3

Accommodation and grazing fees per day

Cattle

1,000.00

1,000.00

 

 

Sheep/Goat

500.00

500.00

 

 

Horse/Donkey

1,000.00

1,000.00

 

 

Camel

1,000.00

1,000.00

 

 

Dog/Cat

500.00

500.00

 

 

2.  The principal Regulations are amended by deleting the Sixteenth Schedules on movement permit fees for animals and animal products on-transit to other countries.

 

SIXTEENTH SCHEDULE

(Made under regulation 22A)

MOVEMENT PERMIT FEES FOR ANIMALS AND ANIMAL PRODUCTS ON-TANSIT TO OTHER COUNTRIES

S/N

ITEM NUMBER

UNIT

FEES (TSHS)

1.

Cattle

Each

2,500.00

2.

Sheep/goats

each

1,500.00

3.

Pigs

each

1,500.00

4.

Horse/mule/donkey

Each

2,500.00

5.

Dogs/Cats

Each

1,000.00

6.

camel

Each

2,500.00

7.

Poultry adult/Guinea fowls

Each

200.00

8.

Commercial Day-Old chick

100 chicks

1,000.00

9.

More than 100 trays of table eggs

30eggs tray

500.00

10.

More than ten trays of parent stock hatching eggs of hatching eggs

each

1,000.00

11.

Turkey

each

1,000.00

12.

Parrot /falcon /ostrich

each

15,000.00

13.

Wild birds

each

500.00

14.

rabbits

each

500.00

15.

Amphibians/reptiles/insects

permit

20,000.00

16.

Laboratory Animals

permit

30,000.00

17.

Wild Animals

Each

1,000.00

18.

Trophies

permit

30,000.00

19.

Meat/meat products of more than 50 kilogram

kilogram

50.00

20.

Sausage/minced meat/other meat products

kilogram

50.00

21.

Bile

Permit

50.000.00

22.

Bull-whip/testicle/tendons

Permit

200,000.00

23.

Milk

Litre

500.00

24.

Yogurt

Litre

2,000.00

25.

Powdered milk

Kilogram

4,000.00

26.

Cheese/ghee

Kilogram

2,000.00

27.

Hides

Per piece

500.00

28.

Skin

Per piece

100.00

29.

Cattle/Goat/Sheep horn tips/Hooves/Hairs

Tone

10,000.00

30.

Feathers/ Wool/Hairs

Permit

20,000.00

31.

Animal feeds

Tone

10,000.00

32.

Organic Manure

Tone

5,000.00

33.

Embryos

Each

5,00.00

34.

Semen

Straw

50.00

35.

Specimen

Permit

20,000.00

36.

Laboratory reagents/equipment

Permit

300,000.00

37.

Livestock identification items (ear tags, etc)

Permit

200,00.00

3.   

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

THE MEAT INDUSTRY ACT

(Cap. 421)

________

REGULATIONS

________

(Made under section 34)

 

THE MEAT INDUSTRY (LOCATION, DESIGN, CONSTRUCTION AND OPERATION OF LIVESTOCK MARKETS) (AMENDMENT) REGULATIONS 2022

Citation and commencement

 

 

GN No. 38 of 2011

(i)                    

(ii)      These Regulations may be cited as the Meat Industry (Location, Design, Construction and Operation of Livestock Markets) (Amendment) Regulations 2022 and shall be read as one with the Meat Industry (Location, Design, Construction and Operation of Livestock Markets) (Amendment) Regulations 2011 hereinafter referred to as the Principal Regulations and shall come into operation on 1st July, 2022

(iii)   The second schedule is amended by deleting the schedule and substituting for it with the following:

 

SECOND SCHEDULE

 

(Made under Regulation 13)

 

FEES PAYABLE FOR TRADE OF LIVESTOCK

 

        SALE OF ANIMALS (MARKET USER FEES)

(a)      Primary Markets:

Type of Fee

Central Government TZS (Proposed)

Local Government TZS

Total Fee Payable TZS

(i)   Fee payable for each head of cattle, camel, horse and donkey

1,000

4,000

5,000

(ii) Fee payable for each head of goat, sheep and pig.

500

1,000

1,500

 

(b)     Upgraded primary market to secondary and border markets (new arrangement):

Type of Fee

Central Government

Local Government

Total Fee Payable

(i)     Fee payable for each head of cattle, camel, horse and donkey

1,000

4,000

5,000

(ii)   Fee payable for each head of goat, sheep and pig

500

1,000

1,500

 

(c)      Secondary markets (Reference Table of ongoing Fee):

Type of Fee

Central Government

Local Government

Total Fee Payable

i.) Fee payable for each head of cattle, camel, horse and donkey

4,000

1,000

5,000

ii.) Fee payable for each head of goat, sheep and pig-

1,000

500

1,500

 

(d)     Boarder Markets (Reference table of ongoing Fee):

Type of Fee

Central Government

Local Government

Total Fee Payable

(i)     Fee payable for each head of cattle, camel, horse and donkey

4,000

1,000

5,000

(ii)   Fee payable for each head of goat, sheep and pig.

1,000

500

1,500

 


Kiambatisho Na. 6

PROPOSED AMMENDMENTS OF THE FISHERIES REGULATIONS OF 2020 GN 491A ON EXPORT LICENCING FEE, EXPORT AND IMPORT ROYALTY OF FISH AND FISHERY PRODUCTS (table G - export license fee and H-export royalty)

S/N

Type of licensing fee/export and import royalty

Tanzanian citizens

Export Licensing fees (USD)

Non-Citizen

 Export license fees

(USD)

 

 

Current

Proposed

Current

Proposed

1

 

 

Export license fees for dried dagaa of Lake Tanganyika

250 USD for small scale processor

 

250 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

2,500 USD

2500 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

 

500 USD for large scale processor

500 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

 

 

2

Export license fees for Haplochromis and dagaa of Lake Victoria

250 USD for small scale processor

250 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

2,000 USD

2000 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

500 USD for large scale processor

500 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

 

 

3

Export license fees for dagaa of Lake Nyasa

250 USD for small scale processor

250 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

2,000 USD

2000 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

 

 

500 USD for large scale processor

500 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

 

 

4

Export license fees for dagaa of Marine Waters

250 USD for small scale processor

250 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

2000 USD

2000 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

500 USD for large scale processor

500 USD combined the three fishery products dried/fresh/frozen dagaa

 

 

5

Export Licence Fee for dried fish/ fishery products from salty lakes (Eyasi, Manyara and Natron), and Lake Rukwa, Nyumba ya Mungu, Mtera and Bahi Swamp

500 USD for small scale processor

300 USD for small scale processor

Prohibited

Prohibited

700 USD for large scale processor

400 USD for large scale processor

 

 

6

Export licence of With or without Head and Gutted Whole Nile Perch” (H&G)

1000 USD for small scale processor

700 USD for small scale processor

2,500 USD

2,500 USD

1200 USD for large scale processor

1000 USD for large scale processor

 

 

7

Sea shells (all types except prohibited Species)

300 USD for small scale processor

150 USD

 Prohibited

700 USD

350 USD for large scale processor

300 USD

8

Frozen Prawns

500 USD for frozen prawns head on for small scale

500 USD combined the two fishery products (head on and headless)

 

2,500 USD head on

2,500 USD combined the two fishery products (head on and headless)

500 USD for frozen prawns headless for small scale processor

2,500 USD headless

1000 USD for frozen prawns’ head for large scale processor

1000 USD combined the two fishery products (head on and headless)

 

 

 

1000 USD for frozen prawns headless for large scale processor

 

 

9

Export License for live crabs and lobster

Live lobster 500 USD

500 USD combined lobster and crabs

prohibited

prohibited

Live crabs 500 USD

1000 USD Large scale processor for lobster

1000 USD combined lobster and crabs

1000 USD large scale processor for crab

10

 

Export License for frozen crab and lobster

500 USD for frozen lobster for small scale processor

500 USD combined for frozen lobster and crabs

2500 USD for frozen lobster

2500 USD combined for frozen lobster and crabs

500 USD for frozen crabs for small scale processor

2500 USD for frozen crabs

1000 USD large scale processor for lobster

1000 USD combined for frozen lobster and crabs

 

1000 USD large scale processor for crabs

 

 

 

11

Export license for frozen Octopus/Squids/cuttlefish

500 USD for small scale processor frozen Octopus

500 USD Frozen Octopus and Squids/Cutlle fish

 

2500 USD for frozen Octopus

2500 USD for frozen Octopus and Squids/Cutlle fish

 

500 USD for small scale processor Squid/Cuttle fish

2500 USD for Squid/Cuttle fish

1000 USD for large scale processor for octopus

1000 USD Frozen Octopus and Squids/Cutlle fish

 

 

1000 USD for large scale processor for Squid/Cuttle fish

12

Import License fee for crustacean/cephalopods/Mollusc

2500 USD

 

250 USD

 

5000 USD

3000 USD

 

13

Cardina spp (Fresh water shrimps)

300 USD for small scale processors

200 USD for small processors

Prohibited

 

500 for large processors

500 for large processors

Prohibited

 

14

Cardina spp marine water shrimps)

300 for small scale processors

200 USD for small processors in marine waters

Prohibited

 

500 for large processors

500 for large processors in marine waters

Prohibited

 

15

Import fee for crustacean/cephalopods

2.5 USD per kg

0.5 USD per kg

2.5 USD per kg

 

0.5 USD per kg

 

16

Export royalty fees for dagaa of Lake Tanganyika

0.5 USD per kg for dried dagaa

0.3 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa

0.5 USD per kg  for dried dagaa

0.3 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa

17

Export royalty fees for Haplochromis (furu) and dagaa of lake Victoria

0.16 USD per kg for dried dagaa

0.1 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa/furu

0.16 USD per kg for dried dagaa

0.1 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa/furu

18

Export royalty fees for frozen/dried dagaa of lake Nyasa

0.16 USD per kg for dried dagaa

0.1 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa

0.16 USD per kg for dried dagaa

0.1 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa

19

Export royalty fees for frozen/dried dagaa of marine waters

0.16 USD per kg for dried dagaa

0.1 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa

0.16 USD per kg for dried dagaa

0.1 USD per kg for dried/fresh/frozen dagaa

20

Export royalty fee for dried fish/ fishery products from salty lakes (Eyasi, Manyara and Natron), and Lake Rukwa, Nyumba ya Mungu, Mtera and Bahi Swamp

0.2 USD per kg

0.08 USD per kg

Prohibited

Prohibited

21

Export royalty fees With or without Head and Gutted Whole Nile Perch” (H&G)

0.21 USD per kg for without Head and Gutted Nile Perch” (H&G)

0.18 USD per kg for headed and gutted Nile perch (H&G)

0.21 USD per kg for without Head and Gutted Nile Perch” (H&G)

0.18 USD per kg for headed and gutted Nile perch (H&G)

0.25 USD per kg Whole Gutted Nile Perch”

deleted

 

      

          -

 

 

       -

22

Export Royalty for Fish Steak/ Fillets

0.2 USD per kg

0.1 USD per kg

 

 

23

Export Royalty for Fish Maws

4% of market value for dried fish maws per kg

3.3 USD per kg

4% of market value for dried fish maws per kg

3.3 USD per kg

4% of market value for fresh and frozen fish maws per kg

2.70 USD per kg

4% of market value for fresh and frozen fish maws per Kg

2.70 USD per kg

 

 

 

 

 

Definition:

‘’Citizen Company’’ means a company which is owned by a person or all owners/shareholders/drectors of a company or partners of registered business are Tanzanians;

 

‘’Non-Citizen company’’ means a company which is owned by a person or one of the owner(s)/shareholder(s)/director(s) is/are not Tanzanians;

 

Large Scale processor’’ means a processor with Certificate of Incorporation issued by BRELLA and the owner(s) is registered as Directors, and has an approved fish processing establishment;

’Small Scale processor’’ means a processor with Certificate of Incorporation issued by BRELLA and the owner(s) is recognized as a proprietor, and has an approved fish establishment or entered into legal agreement with an approved fish establishment for processing or storage of fish and fishery products’’

 

 

 

 

 

Proposed Fee for Movement Permit.

S/N

 

Category

Range (Kgs)

Charges/Fees

(Tshs)

1

Permit for movement of fish and fishery products (dagaa, furu, dried/frozen/chilled fish)

i) Dried fish and fishery products

 

0 – 500 kg

Free

 

501 kg and above

10 TZS   per kg

Any excess undeclared

100 TZS per kg

ii) Frozen/Chilled/

Fresh fish and fishery product

0 – 1000 kgs

Free

 

1001kg and above

10 TZS per kg

 

Any excess undeclared

200 TZS per kg

 

 

 

 


Kiambatisho Na. 7

 

TANZANIA ATOMIC ENERGY COMMISSION - TAEC

MATRIX OF THE ATOMIC ENERGY (FEES AND CHARGES) REGULATIONS

 

S/N

Regulation No

Current practice

Proposed change/ recommendation

Benefit /reasons for the proposed change

01

Fourth Schedule –Fees for radioactivity analysis of food chain and related commodities (Regulations 7)

A. For Imports of Food Chain Materials, Tobacco and Tobacco Products

i.  Tanzania shilling 35,000/= for import consignment whose Freight on Board value does not exceed equivalent of Tanzanian shillings ten million

 

0.4 percent of the Freight on Board value for all consignment with Freight on Board value above Tanzanian shillings 10 million up to equivalent of Tanzanian shillings one billion.

i.  Import consignment not exceeding FoB of TSHS 1,000,000 will be analyzed free of charge (100% reduction);

 

ii.  0.4 percent of the Freight on Board value for all import consignment above Tanzanian shillings 1,000,000/= up to one billion and a limit of Tanzania shillings four million for consignment whole Freight on Board value is above to an equivalent of Tanzanian shillings one billion

There are reasons for charging using FoB values:

 

i.    The FOB model is cheaper. The cost for sampling and analysis of the consignment using FOB value give relief to business community than any other means.

The cost of analysing one sample is Tsh. 428,000 as such business community would be very expensive. Note that one consignment might need several samples depending on the volume or quantity of food chain materials. For example, simulation shows that the quantity-based model for a consignment of FoB value of Tshs. 41,894,000 which weigh 260MT is Tshs 83,000 while the quantity model would attract a charge of Tshs. 910,000 which is equivalent to an increase of 1096%

 

ii.    Quantity based charging does not facilitate trade for the customers with bulk consignment. This means the larger the consignment the more the samples would be needed. Using FoB value is cheaper because same amount is charged irrespective of the number of samples taken in a specific consignment. But using quantity method each sample will be charged and make this method very expensive for the clients. For example, in a year TAEC analyses 28,000 samples and if each sample is to be charged 428,000/= will results to 11.96B which is almost twice the current practice when using FoB. Therefore, with quantity method customer loose the benefit of lower charges offered by TAEC and would need to pay more than when the FoB is used.

 

iii.    The FOB model is efficiency because there is no need to confirm declared quantity as such is time and money saving.

 

iv.    FOB model increase transparency on sampling process since there is no possibility for negotiation between the sampler and the customer.

 

Other benefits of proposed amendments:

i.      These charges were used since 2011 and therefore do not reflect the current practices.

 

ii.      To facilitate trade and create better environment to small business traders where the trader who is currently paying 35,000/- for the importation of a consignment with FOB value less than 1,000,000 will not pay anything; the trader whose consignment value is 1,000,001/= will pay 4,000/= instead of 35,000/=; the trader whose consignment value is 5,000,000/= will pay 20,000 /= instead of 35,000/= and still the limit holds for higher values.

 

iii.      To continue protecting the public and environment from harmful effect of radiation through performing regulatory activities (sampling, sample analysis, inspection, authorization) of imported foodstuffs.

ii.   Tanzania shillings four million for consignment whole Freight on Board value is above to an equivalent of Tanzanian shillings one billion.

B. For exports of Food Chain Materials including fertilizers, tobacco and tobacco products, and imported relief food

i.  Tanzania shilling 35,000 for Export consignment whose Freight on Board value does not exceed equivalent of Tanzanian shillings twenty million.

i.  Export consignment not exceeding 2000 US dollar will be analyzed free of charge (100% reduction);

 

ii.  0.1 percent of the Freight on Board value for all consignment with Freight on Board value above two thousand US dollar up to an equivalent of Tanzanian shillings one billion (Reduced by 50%) and a limit of Tanzania shillings two million for consignment whole Freight on Board value is above to an equivalent of Tanzanian shillings one billion.

 

iii.  0.1 percent of the Freight on Board value for the value added finished products (Reduced by 50%) and a limit of Tanzania shillings two million for consignment whole Freight on Board value is above to an equivalent of Tanzanian shillings one billion

There are reasons for charging using FoB values:

 

    i.        The FOB model is cheaper. The cost for sampling and analysis of the consignment using FOB value give relief to business community than any other means. The cost of analysing one sample is Tsh. 428,000 as such business community would be very expensive. Note that one consignment might need several samples depending on the volume or quantity of food chain materials. For example, simulation shows that the quantity based model for a consignment of FoB value of Tshs. 41,894,000 which weigh 260MT is Tshs 83,000 while the quantity model would attract a charge of Tshs. 455,000 which is equivalent to an increase of 548%.

 

   ii.        Quantity based charging does not facilitate trade for the customers with bulk consignment. This means the larger the consignment the more the samples would be needed. Using FoB value is cheaper because same amount is charged irrespective of the number of samples taken in a specific consignment. But using quantity method each sample will be charged and make this method very expensive. For example, in a year TAEC analyses not less than 28,000 samples and if each sample is to be charged 428,000/= will results to 11.96B which is almost twice the current practice when using FoB. Therefore, with quantity method customer loose the benefit of lower charges offered by TAEC and would need to pay more than when the FoB is used.

 

 iii.        The FOB model is efficiency because there is no need to confirm declared quantity as such is time and money saving.

 

 iv.        FOB model increase transparency on sampling process since there is no possibility for negotiation between the sampler and the customer

 

   v.        The charge of 0.1% has been obtained aiming at encouraging exports of value-added finished products

 

 vi.        Protecting the foreign market of our products and therefore stimulate our economy.

 

vii.        To enable TAEC to control illicit trafficking and nuclear security issues such as sabotage and malicious acts.

 

viii.        To enable TAEC to control contamination from naturally occurring radioactive materials in the environment such as Uranium and Thorium.

 

Other benefits for the proposed change include:

 ix.        These charges were used since 2011 and therefore do not reflect the current practices.

 

   x.        To facilitate export trade and create better environment to small business traders, whereby the trader who is exporting a consignment with FOB value less than 5,000,000/= (USD 2000) was supposed to pay 35,000/= but the samples will be analyzed free of charge/= (not pay anything) and the trader whose consignment value is 20,000,000/= was supposed to pay 40,000/= but it is proposed to pay only 32,000/= and still the limit holds for higher values.

 

 xi.        To continue fulfilling the international requirements and standards (FAO/WHO/IAEA/WTO) for the exporting country to ensure safety of food chain material as such avoid international trade cases.

 

xii.        Protecting the public and environment from harmful effect of radiation through performing regulatory activities (sampling, sample analysis, inspection, authorization) of exported foodstuffs

iv.   0.2 percent of the Freight on Board value for all consignments with Freight on Board above Tanzanian shillings 20 million up to equivalent of Tanzanian shillings one billion 

v.  Tanzania Shilling two million for consignment whole Freight on Board value is above to an equivalent of Tanzania Shillings one billion

C. For all manufacturers, processors and milling of Food chain materials, Tobacco and Tobacco products and possess and use underground and reservoir waters

 

A)  Radioactivity analysis fees per annum as follows:

 

i.    Free for Micro Enterprises and Small Enterprises (SMEs)

ii.  Tanzania shillings two hundred and fifty thousand for Medium Enterprises (MSEs).

iii.Tanzania shillings three hundred thousand (300,000/=) for Large Enterprises (LE)

NOTE:

According to the Small and Medium Enterprise Development Policy (2003), Tanzania defines categories of enterprises as follows:

1.Micro Enterprises as up to 4 employees or up to 5 Million investments in Machinery

 

2.Small enterprises are mostly formalized undertakings engaging between 5 and 49 employees or with capital investment from TZS 5 million to TZS 200 million.

 

3.Medium enterprises employ between 50 and 99 people or use capital investment from Tshs.200 million to TSHS 800 million.

 

4.Large enterprises employ at least 100 people or have machinery investment above TSHS 800 million.

 

B)  For radioactivity analysis license to possess and use underground and reservoir waters, water reservoir Tanzania shillings 50,000/= per unit in every three years.

i.The proposed lower fees will enhance traders to comply and create a cost sharing mode. Taking into account that the cost for sampling and analysis one sample is estimated to be TZS 428,000. For every manufacturer and processor will require more than one sample per year depending on the scale of manufacturing and processing of food stuffs, Tobacco and Tobacco products.

ii.          To contribute to empowering TAEC in controlling the danger of radiations as per Section 30 and 31 of the Atomic Energy Act.

iii.        To continue protecting the public and environment from harmful effect of radiation through performing regulatory activities (sampling, sample analysis, inspection, authorization)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Contamination from natural occurring radioactive materials is likely to affect the citizens using underground and reservoir waters, thus protection of citizens is of great importance.

 

02

First Schedule for Licensing/Registration of Various Practices

(Regulations 4)

 

 

1. Medical and non-medical applications (Radiation Generating Devices and Radiation Sources), research clearance and scrap metals

Authorization to use and or possess Medical Diagnostic Equipment:

i.  X-ray machine and dermatology- Up to 2 units 150,000/= with an increase of 25% for each additional unit

i.  For authorization to use and possess, operate, hire, Import, export or transfer of medical diagnostic equipment shall be charged Tshs. 200,000/= per unit

 

ii.  For authorization to use and possess, operate, hire, Import, export CT scanner, therapeutic (teletherapy and brachytherapy), angio-suite, MRI, Nuclear Medicine, PET CT and biological irradiation facilities shall be charged Tshs 300,000/= per unit

 

iii.  For authorization to use and possess, operate, hire, Import, export transfer non-medical radiation emitting equipment, device, communication base stations, premises for storage of radiation sources, and research clearance shall be charged Tshs 300,000/= per unit/ research

 

 

i   To meet the cost servicing an X-ray machine which is 1,700,000 per unit and CT scan which is 3,000,000 per unit per annum. The same applies to other practices.

 

ii These charges were used since 2011 and therefore do not reflect the current costs.

 

iii           To reduce number of categories of charges in order to simplify handling.

 

iv           To reduce the cost of cancer diagnostic and treatment to enable patients to access services and thus to stimulate early diagnosis and minimize or prevent the growing of cancer cases.

 

v    To enable TAEC to continue protecting workers, patients, public and environment through conducting regulatory activities (inspection, reviews, authorization, enforcement) to medium risk radiological practices.

 

vi  To facilitate the regulatory processes of research clearance, permit on peaceful application of nuclear technology as per section 53. of Atomic Energy Act. No 7 2003

 

 

ii.         Authorization to use and or possess therapeutic (teletherapy and brachytherapy) and biological irradiation facilities 200,000/= per unit

iii.       Authorization to use and or possess X-ray equipment used for level detection and sorting of minerals 150,000/= per unit

iv.        Possess and use CT scanner 150,000/= per unit

v.Authorization to use and or possess X-ray and or radioactive materials for Non Destructive Testing 200,000/=

vi.        Authorization to use and or possess fixed/portable nuclear gauges for level measurement, density measurement, thickness control, moisture measurement and control and in-stream analysis of slurries 200,000/=

vii.      Authorization to import and or export therapeutic (teletherapy and brachytherapy) and biological irradiation facilities 300,000/= per unit

viii.    Authorization to import and or export Medical diagnostic Equipment: a) X-ray machine and dermatology 120,000/= and CT Scanner 200,000/= per unit

ix.        Authorization to import and or export fixed or portable nuclear gauges for level detection, density measurement, thickness, control moisture measurement and control in stream analysis of slurries 200,000/= per unit

x.Authorization to import and or export Level Detection and Sorting of Minerals Authorization to import and or export 150,000/= per unit

xi.       Authorization to import and or export X-ray Fluorescence, X-ray Diffraction and Neutron Activation Analysis 100,000/= per unit

xii.     Authorization to use and or possess linear accelerators and or devices with radioactive sources for cargo and container inspection Tshs 600,000 per unit

i.  Tanzania shillings 500,000/= per unit/consignment for authorization to use and possess, Import, Export, hire, transfer or class4 laser product, non-medical Linear Accelerator, cyclotron, Fixed X-ray or Radioactive Devices for Non Destructive Testing, Cargo or Container Inspection scanner, or and other devices of considerable significant high risk, soil samples containing radioactive materials, NORMs; and screening of consignment of scrap metal.

i.  These charges were used since 2011 and therefore do not reflect the current practices.

 

ii.           To reduce categories of charges and to merged them for smooth managing complicated procedures

 

iii.         To enable TAEC to conduct regulatory activities (inspection, reviews, enforcement) to complex and high risk radiological practices in order to ensure safety of workers, the general public and the environment.

 

iv.         To enable TAEC to conduct inspection of scrap metals in order to search for radioactive sources and prevent radioactive sources from entering steel pool and protect heath of workers, general public and the environment

xiii.    Authorization to import and or export Linear Accelerator or Radioactive Devices for Non Destructive Testing and Cargo, container inspection 500,000/= per unit

xiv.    Authorization to import and or export Linear accelerators and or Devices with Radioactive Sources for cargo and or container inspection 600,000/= per unit

xv.      Authorization to use and or possess industrial irradiation & Nuclear Reactors –to be determined- by TAEC in consultation with the Minister

 

ii.  Tanzania shillings 5,000,000/= per unit for authorization to use and or possess, hire, transfer, export, import industrial irradiation source/facility, nuclear research reactor, radioactive minerals and Tanzania Shillings 10,000,000/= for siting, construction, operation or decommissioning of Nuclear Power Plant.

 

i.Usually nuclear installation have several stages which need license and government commitment.

 

ii.         The proposed charges will increase efficiency by removing complications and managing and subjectivity in decision making as such increase efficiency in managing radiation safety.

 

iii.         To enable TAEC to conduct regulatory activities (inspections, reviews, guidance, enforcement)to more complex and high risk radiological practices in order to ensure protection and safety of occupationally exposed workers, public and the environment

xvi.    Authorization to import and or export Industrial Irradiation Sources 5,000,000/= per unit

 

 

 

 

iii.  Additional Tanzania Shilling 1,000,000/= per unit for  authorization to import all Ionizing and Non-Ionizing Radiation emitting for equipment or devices of age above 8 years since manufactured (NEW)

i   To discourage aged materials/devices and protect the environment from dumping. For example, importing a device with radioisotope Americium-241 used in water industries, breweries, beverages, road construction etc have half half-life of 432.2 years and will need 4322 years for safe disposal to the environment. For the device with caecium-137 with hall-life of 30 years will need 300 years for safe disposal to the environment

 

ii   To enable TAEC to conduct regulatory processes (registration, inspections, reviews, guidance, authorization) to the imported/exported radiation sources

2. Registration of qualified personnel, Technical Service Providers and License to Transport Radioactive Sources

i.      Tanzania Shillings 50,000/= for the registration of qualified personnel to administer ionizing radiation to person( charged for 5yrs)

i.    Free of charge for qualified personnel to administer ionizing radiations to persons

 

ii.    For every 5 years Tanzania Shillings 50,000/= for  registration of qualified personnel to operate, install, repair and maintenance radiation devices or apparatus or plant

i.  Monitoring of qualified personnel is very important to ensure that personnel administering ionizing radiation to personnel are qualified.

 

ii.  In the current practice the charges is paid by the hospitals therefore removing it will reduce medical expenses to the public

 

iii.  To continue protecting workers, patients public, and environment from harmful effect of radiation through performing the regulatory activities

ii.       Tanzania shillings 1,000,000/= per consignment for Authorization to transport Category 1 to 3 radioactive material within and on transit through Tanzania

iii.    Tanzania shillings 1,000,000/= for Authorization to transport Category 1 to 5 radioactive material, Mineral containing radioactive materials and NORMs within and /or on transit through Tanzania, and provision of technical services such as, Personnel dosimetry services, workplace monitoring services, standards calibration services, environmental monitoring services, radio analytical measurements, repair and maintenance of nuclear equipment, Supplier of radiation devices, Transporters of radioactive materials, Storage of radiation devices, storage of Radioactive Waste, Radiation Protection Training Services providers, Quality Assurance and Quality Control Services providers. (Excluding reimbursable).

i.  To continue protecting workers, public, and the environment from harmful effects of radiations through conducting regulatory activities (inspections, reviews, enforcements, etc) in authorization to transport radioactive materials, radioactive minerals, NORMs and technical services

 

ii.           To enable TAEC to monitor technical services and enhance safety in technical service involving nuclear applications and during transport radioactive sources

 

03.

Second schedule Pre-Authorization Inspection Fees

(Regulation 5)

 

 

Non-routine inspection Fee for facility or activity for Medical and Non-Medical Applications (Radiation Generating Devices and Radiation Sources).

 

i.  Assessment and Inspection of Radiology X-ray unit, up to 2 units: 100,000/= with an increase of 25% for each additional unit

i.  Tanzania Shillings 100,000/= per unit for assessment and Inspection of Radiology X-ray unit

 

ii.  Tanzania Shillings 200,000/= per unit for assessment and inspection of Radiation emitting equipment, device and base stations, and radioactive material storage facility and other low and moderate risk practices excluding reimbursable

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

i.  The current charges have been in use since 2011 and therefore do not reflect the current practices.

 

ii.  Simplified management and handling of fees by merged categories and removed complications of calculations

 

iii.  To enable TAEC to conduct inspection to medium risk radiological practices in order to protect heath of patients, occupationally exposed workers, and public from harmful effects of radiation

ii.   Assessment and or Inspection of CT Scanner, Radiotherapy devices and Nuclear medicine facilities: up to 2 units: 200,000/= with an increase of 25% for each additional unit

iii.  Assessment and or Inspection of Duo diagnostic (both conventional and Fluoroscopy) Fluoroscopic and Mammography units, baggage screening up to 2 units: 150,000/= with an increase of 25% for each additional unit

iv.   Assessment and or inspection of Gamma units for non-destructive testing, fixed/portable nuclear gauges and biological irradiator up to 2 units: 300,000/= with an increase of 25% for each additional unit

 

v.  Assessment and or inspection of teaching and or education radiation sources up to 2 units: 50,000/= with an increase of 25% for each additional unit.

vi.   Assessment and or inspection of Nuclear Analytical techniques, X ray Fluorescent Analysis and X-ray Diffraction up to 2 units: 100,000/= with an increase of 25% for each additional unit.

vii.Assessment and or inspection of linear accelerators and or devices with radioactive source for cargo and or  container inspection  up to 2 units: 500,000/= with an increase of 25% for each additional unit

iii.  Tanzania shillings 500,000/= per unit for assessment and inspection of base station, Class 4 laser products, Linear Accelerator, Fixed X-ray or Radioactive Devices for Non Destructive Testing, Cargo or Container Inspection scanner, cyclotron  or and CT scan, MRI, scrap metal warehouse and other devices of considerable significant high risk, excluding reimbursable.

To enable TAEC to continue protecting the public, workers and the environment by conducting inspection to medium risk radiological practices in order to protect heath of patients, occupationally exposed workers, and public from harmful effects of radiation

viii.Assessment of the plan for any nuclear power Plant and or Nuclear Reactor 5,000,000/=

iv.  For each assessment/inspection during sitting, construction, commission, operation and decommission of mines containing naturally occurring radioactive minerals or conventional mines, Assessment of radon gas concentrations in underground mines, Irradiator facility shall be charged Tanzania Shillings 5,000,000/=

 

v.  For each assessment and inspection during sitting, construction, commission, operation and decommission of Nuclear Power, Nuclear Research Reactor, Radioactive minerals mine, processing, disposal and tailings facility shall be charged Tanzania shillings 10,000,000/= excluding reimbursable

To continue protecting the public, workers and environment by

 

i.    Enabling TAEC to maintain the quality of inspection including equipment and inspectors whose cost of training is approximately 500,000 Euros in European union and need quarterly inspections with different expertise with not less than 5 inspectors per category of inspection.

 

ii.    Enabling TAEC to conduct regulatory inspection to complex/high risk radiological practices in order to protect heath of workers, public and the environment from harmful effects of radiation

 

iii.    It is important to monitor radon gas in underground mines to reduce the biological effect of radon to miners

04.

Third schedule- Fees and Charges For Activities Relating to Prospecting/Exploration, Mining and Processing of Radioactive Minerals

(Regulations 6)

ix. Verification in respect of Decommissioning of radioactive ore mine and its processing facilities 100,000,000/= per mine or processing facility

Twenty million Tanzanian shillings (20,000,000/) per annum per facility or processing facility for verification in respect of Decommissioning Process of radioactive minerals mine and its processing facilities.

i. To simplify payments to the mining operators

ii.          To align with the government budget time frame

iii.        To continue protecting workers, public and the environment from harmful effects of radiations through regulatory activities (reviews, guidance, authorization, enforcement) of decommissioning radioactive ores mine or ore processing facilities

05.

 

Fifth Schedule Fees and charges for other related activities or services

(Regulation 8)

i.  Review of radiation shielding (External beam radiation)- (200,000/= per facility for Diagnostic, (240,000/= for Therapy), 200,000/= for Industrial)

Tanzania Shillings 200,000/= per unit to Provide Structural Design and layout of diagnostic X-ray facilities, Review of radiation shielding radiological facilities, Perform quality control tests of diagnostic radiation equipment, Testing of integrity of package of radioactive sources for transport and maintenance of survey meters

i.  To continue enabling TAEC to provide technical and radiation protection services to protect heath of workers, public and the environment from harmful effects of radiation.

 

 

ii.  Quality control tests of diagnostic X-ray equipment-Conventional radiography( Up to 2 units 100,000/= with an increase of 25% for each additional unit, - Radiographic mammography and fluoroscopy (Up to 2 units 150,000/= with an increase of 25% for each additional unit and CT scanner(Up to 2 units 200,000/= with an increase of 25% for each additional unit

iii.  Testing of integrity of package of radioactive sources for transport( 150,000/= per device and 15,000/= for any additional device

iv.   Tanzanian Shillings 100,000/= per unit to Provide Structural Design and layout of diagnostic X-ray facilities

i.  Tsh 50,000/- or USD 50 for measurement of sample by (HPGe) or NaI(Tl) per sample

 

(i) Tanzania Shillings 100,000/- and 25% discount for students for measurement of one sample by either gamma spectrometry, EDXRF or TXRF.

i.    To enable sample preparation, reagents and consumables sampling, reference standards sample measurements.

ii.    To promote and encourage students and scientists to engage in science and technology applications

ii.   TSH 34,000/- or 50 USD for measurement of sample by XRF per sample.

iii.  Tsh 100,000/ Personal dosimetry services for up to two TLDs and Tshs. 34,000/= for each additional TLD

Tanzania Shillings 100,000/ Personal dosimetry services per TLD

To enable sample preparation, reagents and consumables sampling, reference standards sample measurements.

 

iv.   Tsh 170,000/- per lost TLD.

For lost TLD will be charged per market price of the TLD

To have ability to replacement the lost TLD and continue with services for monitoring workers

 

v.  Tsh 100,000/- (resident) or USD 50 (non- resident) for calibration of individual and environmental monitoring detector up to ten (10) detectors and Tsh. 34,000/- (resident) or USD 20 ( non- resident) for each additional detector

Tanzania Shillings. 150,000/- or USD 150 (non- resident) for calibration of radiation Survey meter, Electronic personnel dosimeter, individual and environmental monitoring detector

i.      To ensure the reliability of instruments, that it can be trusted

 

ii.      To determine the accuracy of instruments.

 

iii.      To ensure the readings/results are consisted with other measurements

 

 

vi.   Tsh. 350,000/-(resident) or USD 200(non- resident) for calibration of radiation Survey meter and Tsh. 350,000/-(resident) or USD 200 (non-resident) for each additional meter

vii.  Tsh. 150,000/- (resident) or USD 100 (non - resident) for calibration of Electronic personnel dosimeter and Tsh.100,000/=(resident) or USd 100 (non- resident) for each additional dosimeter

 

 

viii.  Tsh. 1,900,000/- for calibration, repair and maintenance of Moisture and density gauges

Tanzania Shillings. 1,900,000/- for calibration, repair and maintenance of Moisture and density gauges excluding reimbursable.

This still caters the cost of calibration of which clients will continue benefiting the same price

ix.   Tsh. 500,000/= for consultation services on the proper use of X-ray machines

Tanzania Shillings. 500,000/= for consultation services on the proper use of X-ray machines

This still caters the cost of consultation services of which clients will continue benefiting the same price

 

x.   5% of FOB value of the machine or flat rate of 3,500,000/= for installation of each X-ray machine for machine which its FOB value is not known.

Tanzania Shillings 2,500,000/= for installation, repair and maintenance of x-ray machine excluding reimbursable

This still caters the cost of installation services of which clients will continue benefiting the same price

 

 

xi.   5% of FOB value of the machine or flat rate of 3,500,000/= for repair and maintenance of each X-ray machine for machine which its FOB value is not known.

 

 

xii.  Fees for radioactive waste management

Tanzania Shillings 3,000,000/= shall be charged for Storage of disused sealed radioactive sources and Tanzania Shillings.1,000,000/= for conditioning of disused sealed radioactive sources (excluding reimbursable)

To facilitate transportation of sources with special transportation condition and enhance storage and decommission after the end of ten half-lives. For example disposal and conditioning of  a device with caecium-137 radioisotope have hall-life of 30 years and will need to remain under TAEC custody for 300 years

 


Kiambatisho Na. 8

 

THE FIRE AND RESCUE FORCE ACT,
(CAP. 427)
__
REGULATIONS
___
(Made under section 32(g))
______

THE FIRE AND RESCUE FORCE (SAFETY INSPECTION AND CERTIFICATES) (AMENDMENT) REGULATIONS, 2022

 

S/N

PROPOSAL

CURRENT

PROPOSED

JUSTIFICATION

ITEM

LEVY

ITEM

LEVY

1

3.TRADE FAIR

3.TRADE FAIR

 

3.TRADE FAIR

 

Previous meter square is not realistic because 2000m2 is small compared to reality.

To enlarge the areas of category from   to 10,000m2 and Above 10,000m2.

Less than or equal to 2000m2

L12 (700000 -1000000)

Less than or equal to 10000m2

L12 (700,000 -1000000)

 

Above 2,000m2

L15 (1,500,000 -3,000,000)

Above 10,000m2

L15(1,500,000 -3000000)

2

10. EDUCATION BOARDING SCHOOL

10. EDUCATIONAL BOARDING SCHOOL

 

10. EDUCATIONAL BOARDING SCHOOL

 

To reduce levy burden and increase compliance.

Increase the number of boarders

Less than or equal to 100 boarders

L7 (50,000 -200,000

Less than or equal to 200 boarders

L7 (50,000 -150,000

 

101-500 boarders

L8 (200,000 – 500,000)

201-500 boarders

L8 (200,000 – 500,000)

 

Above 500 boarders

L9 (300,000 -600,000

501-1000 boarders

L9 (300,000 -600000

 

 

 

Above 1001 boarders

L10 (550,0000 - 700,000)

3

We propose to reduce the fire inspection fee from 100,000 to 8,000,000 of the previous to 10,000/= to 3, 000,000/=

11. TRAINING INSTITUTIONS

 

TRAINING INSTITUTIONS

 

 

Less than or equal to 500 students

L5(10,000 - 40,000)

Less than or equal to 500 students

L5(10,000 -40,000)

501-1,000 students

L6(40,000 -100,000)

501-1,000 students

L6(40,000 -100,000)

1,001-2,000 students

L7 (50,000-200,000)

1,001-2,000 students

L7(50,000 -200,000)

2,001-3,000 students

L9 L (300,000 -600,000

2,001-3,000 students

L8A (400,000)

More than 10,000 students

L19(8,000,000/=)

3,001-4,000 students

8B (300,000)

 

 

4,001–5,000 students

L8(200,000 – 500,000)

 

 

5,001–6,000 students

L9(300,000-900,000)

 

 

6,001–7,000 students

L10(550,000-700,000)

 

 

7,001–8,000 students

L11(500,000-800,000)

 

 

8,001–9,000 students

L12(700,000-1,000,000)

 

 

9,001 - 10,000 students

L13(600,000-1,500,000)

 

 

More than 10,000 students

L15(1,500,000 – 3,000,000)

4

We propose to categorize the type of Bar.

12.BAR

 

12. BAR

 

 

L6(40,000 -100,000)

Bar without cooking facilities

L6(40,000 -100,000)

 

Bar with cooking facilities

L7 (50,000-200,000)

5

We propose to add new fire category and its levy

NONE

 

13. SERVICE BAYS

L5(10,000 - 40,000)

To increase compliance and new source of income.

6

In the in the classification guide were added a new item “lodge and bandas” as the new source and it will be charged from tsh 200,000/= to 4,000,000/= depending on the rooms and huts and location.

16.HOTEL IN PROTECTED AREA

 

HOTEL/LODGE/BANDAS IN PROTECTED AREA

 

 

7

In the in the classification guide were added a new item “vibrated blocks making facilities” as the new source and it shall be charged from 40,000/= to Tsh 3000,000/= dependin on m2 and locations. And also to change the area(m2)

19.INDUSTRIAL SERVICES

 

18. INDUSTRIAL SERVICES

 

 

Less than or equal to 50m2

L6(40,000 -100,000

Less than or equal to 100m2

L6(40,000 -100,000

Gross floor area 51-500m2

L7(50,000 - 200,000

Gross floor area 101-500m2

L7(50,000 - 200,000

Gross floor area 501-1000m2

L8(200,000 - 500000

Gross floor area 501-1000m2

L8(200,000 – 500000

Gross floor area 1001-2000m2

L9 (300,000 -600000

Gross floor area 1001-2000m2

L9 (300,000 -600000

Gross floor area 2001-3000m2

L10(550,000 - 700000

Gross floor area 2001-3000m2

L10(550,000 – 700000

Gross floor area 3001-5000m2

L12(700,000 - 1000000

Gross floor area 3001-4000m2

L12(700,000 – 1000000

Gross floor area 5001-7000m2

L13(600,000 - 1,500,000

Gross floor area 4001-5000m2

L13(600,000 - 1,500,000

Gross floor area 7001-8500m2

L14(800,000 - 2,000,000

Gross floor area 5001-6000m2

L14(800,000 - 2,000,000

More than 8501m2

L15 (1,500,000 -3,000,000)

More than 6000m2

L15 (1,500,000 -3,000,000

8

In the in the classification guide were added a new item “demolition or alteration” as the new source and it shall be charged as the same as construction site. i.e tsh L7 (50,000-200,000)

21. CONSTRUCTION SITE

 

21 CONSTRUCTION SITE

 

To increase compliance and revenue.

(Commercial, and Industrial only)

(Commercial, Research and Industrial only)

9

We propose to change m2 of some items under this category

20. BEVERAGE INDUSTRIES

 

19. BEVERAGE INDUSTRIES

 

To reduce tax burden and increase compliance

(a) For non-alcoholic industries

 

(a)    For non-alcoholic industries

 

Less than or equal to 500m2

L5(10,000 - 40,000)

Less than or equal to 500m2

L5(10,000 - 40,000

Gross floor area 501-1125m2

L6(40,000 -100,000)

Gross floor area 501-1000m2

L6(40,000 - 100,000

Gross floor area 1126-2000m2

L7(50,000 - 200,000

Gross floor area 1001-2000m2

L7A (50,000 -150,000

Gross floor area 2001-3500m2

L8(200,000 - 500000

Gross floor area 2001-3000m2

L8(200,000 - 500,000)

Gross floor area 3501-4500m2

L9 (300,000 -600000

Gross floor area 3001-4000m2

L9 (300,000 -600,000

  Gross floor area 4501-5500m2

L12(700,000 - 1000000)

Gross floor area 4001-5000m2

L12 (700,000 -1,000000)

   Gross floor area 5501-7000m2

L13(600,000 - 1,500,000

Gross floor area 5001-7000m2

L13(600,000 - 1,500,000

 Gross floor area 7001-8000m2

L14(800,000 - 2,000,000

Gross floor area 7001-8000m2

L14(800,000 - 2,000,000

More than 8501m2

L15 (1,500,000 -3,000,000)

More than 8000m2

L15 (1,500,000 -3000000)

(b) For alcoholic industries less than or equal to 500 m2

L7(50,000 - 200,000)

(b)   For alcoholic industries less than or equal to 500 m2

L7A (50,000 -150,000

Gross floor area 501-1125m2

L8(200,000 - 500000)

Gross floor area 501-1000m2

L8(200,000 - 500,000)

Gross floor area 1126-2000m2

L9 (300,000 -600000)

            Gross floor area 1001-2000m2

L9 (300,000 -600000

Gross floor area 2001 – 3500m2

L10(550,000 - 700000)

Gross floor area 2001 – 3000m2

L10 (5500000 - 700,000)

Gross floor area 3501-4500m2

L12(700,000 - 1,000,000)

Gross floor area 3001-4000m2

L11(500,000 - 800,000)

Gross floor area 4501-5500m2

L13(600,000 - 1,500,000)

Gross floor area 4001-5000m2

L12 (700,000 -1000000)

Gross floor area 5501-7000m2

L14(800,000 - 2,000,000)

Gross floor area 5001-6000m2

L13(600,000 - 1,500,000

Gross floor area 7001-8500m2

L15 (1,500,000 -3,000,000)

Gross floor area 6001-7000m2

L14(800,000 - 2,000,000

More than 8501m2

L16(2,500,000 - 4,000,000)

More than 7000m2

L15 (1,500,000 -3000000)

10

We propose to add new item “fishing port and cruise home port and their corresponding levy. And the word “lake port” to replace with the word “inland port”

25. PORT

 

24.PORT

 

 

Lake port

L12(700,000 – 1,000000)

 Inland port

L12(700,000 – 1,000,000)

Sea port

L14(800,000 - 2,000,000

Sea port

L14(800,000 - 2,000,000)

 

Fishing Port

L8(200,000 - 500,000)

 

 

Cruise home  port

L8(200,000 - 500,000)

11

We propose to add new item fire Levy and proposed under this category that will be charged from tsh L6(40,000 - 100,000) to L17(2,000,000 - 5,000,000)

33. POWER STATION

 

33.POWER STATION

 

 

Hydro

L18(3,000,000 - 6,000,000)

Mini Hydro less than 10 megawatt

L7 (50,000 -200,000

Gas

L17(2,000,000 - 5,000,000)

Hydro more than 10 megawatt

L18(3,000,000 - 6,000,000

Wind/Thermal

L17(2,000,000 - 5,000,000)

Gas

L18(3,000,000 - 6,000,001

Sub - Station

L6(40,000 -100,000

Wind

L17(2,000,000 - 5,000,000

 

 

Sub- Station

L12 (700,000 -1,000,000)

12

We propose to delete this item that charged tsh 30,000/=

34. TRANSFORMER

 

 

 

To reduce  burden

13

We propose to Reduce the fire levy under this category from tsh L3 (5,000 - 20,000 to L2 (10,000/=) for surveyed area and from L2 (10,000/=) to L1A (5,000/=) for un surveyed area.

34.RESIDENTIAL/RESIDENCE HOUSE

 

34.RESIDENTIAL/RESIDENCE HOUSE

 

To reduce  levy burden and increase compliance

Surveyed area

L3(5,000 - 20,000

Surveyed area

L2(10,000)

Un surveyed area

L2(10,000)

Un surveyed area

L1A(5,000)

14

 

36.RESIDENTIAL/BUILDING UNIT GROUP TITLE COMMUNITY

(perunit/

apartment)

L7(50,000 - 200,000)

GROUP TITLE COMMUNITY (per unit/

apartment )

L6(40,000 -100,000)

To reduce  levy burden and increase compliance

15

 

RESIDENTIAL FLAT

 

RESIDENTIAL FLAT

 

To reduce levy burden and increase compliance

Less than or equal to 4 levels

L8(200,000 - 500,000)

Less than or equal to 4 levels

L8A(400,000)

5-8 levels

L9 (300,000 -600000)

5-8 levels

L8B(300,000)

9-12 levels

L10(550,000 – 700000)

9-12 levels

L8(200,000 - 500,000)

13-16 levels

L12(700,000 – 1000000)

13-16 levels

L10 (550,0000 - 700,000)

17-20 levels

L15 (1,500,000 -3,000,000)

17-20 levels

L12 (700,000 -1,00,0000)

21-24 levels

L16(2,500,000 - 4,000,000)

21-24 levels

L13(600,000 - 1,500,000)

25-28 levels

L17(2,000,000 - 5,000,000)

25-28 levels

L14(800,000 - 2,000,000

More than 28 levels

L20(6,000,000 - 9,000,000)

More than 28 levels

L15 (1,500,000 -3,000,000)

16

we propose to add new fire category

NONE

NONE

43. MIXED USE BUILDINGS

 

 

Less than or equal to 4 levels

L8(200,000 - 500,000)

5-8 levels

L10(550,000 - 700000

9-12 levels

L12(700,000 - 1000000

13-16 levels

L13(600,000 - 1,500,000)

17-20 levels

L14(800,000 - 2,000,000

21-24 levels

L15 (1,500,000 -3000000)

25-28 levels

L16(2,500,000 - 4,000,000)

More than 28 levels

L17(2,000,000 - 5,000,000)

17

We propose to add new item which whole sale and ‘Mini super market’ which will be charged tsh L4(30,000/=) for each item,

45.SHOP

 

45. SHOP

 

 

Retail

L3(5,000 - 20,000

Wholesale

L4(30,000)

Mini supermarket 

L4(30,000)

18

We propose to add new item "Sales of Portable Fire Equipments" and their corresponding fire levy that will be charged at TShs. 100,000/=

54. FIRE EQUIPMENT DEALER

 

54. FIRE EQUIPMENT DEALER

 

To increase revenue and compliance to propriators who only sells Portable Fire Extinguishers without involving servicing and maintenance

 

 

Sales of Portable Fire Equipments

L6 (100,000)

19

In the classification guide were added a new item “ferry and airport” as the new source .

63. TERMINAL

 

 

 

 

20

we propose to add new fire category "WORKSHOPS" and their corresponding fire levy that will be charged from 10, 000/= THS to Tsh 40,000/= depending on their location.

NONE

NONE

64. WORKSHOP

L5(10,000 - 40,000)

To increase compliance and source of revenue

21

We propose to remove this category from this schedule and establish a new schedule special for this case for reducing the fire levy.

58. APROVAL OF  FIRE ENGENEERING

 

 

This will reduce the fire levy from the minimum level of tsh 200,000/= to the minimum of tsh 15,000/=

To increase compliance.

22

We propose to  Add new Fire category and their Fire Levy that will be charged tsh 10,000  to 40,000/= as "Dry cleaners" were charged as Offices

NONE

NONE

68.DRY CLEANER

 

To provide clarity for Dry Cleaner category as it was charged under Office category

23

We propose to delete this category and their corresponding levy

13 FARMING/ GRAZING

 

 

 

To reduce levy burden in agriculture sector.

Less than or equal to 10 hectares

L6(40,000 - 100,000)

11-40 hectares

L8(200,000 - 500,000

41-100 hectares

L10 (5500000 - 700,000

More than 100 hectares.

L12 (700,000 -1000000)

 

We propose to delete this category and their corresponding levy

17. SISAL COFEE AND TEA PLANTATIONS

 

 

 

To reduce levy burden in agriculture sector.

Less than or equal to 500m2

L6(40,000 - 100,000)

501-1000m2

L7(50,000 - 200,000

1001-6000m2

L8(200,000 - 500,000

Above 6000m2

L12 (700,000 -1000000)

More than 40 hectares

L11(500,000 - 800,000

 


Kiambatisho Na. 9

First Schedule

____________

(Made under Regulation 4 and 14)

Licence fees and Levy

No

Type of License

Application Fee

Licence Fee

Levy

1.

CASINO - DAR

TZS 1,000,000 (annually)

USD 40,000 (annually)

-

2.

CASINO - REGION

TZS 1,000,000 (annually)

USD 20,000 (annually)

-

3.

SLOT MACHINES OR ROUTE OPERATIONS (SHOP)

TZS 100,000 (annually)

TZS 500,000 (annually)

TZS 10,000 (monthly per machine)

4.

SLOT MACHINES OR ROUTE OPERATIONS (CLUBS/PLACES SELLING LIQUOR)

TZS 10,000 (annually)

TZS 50,000 (annually)

TZS 10,000 (monthly per machine)

5.

NATIONAL LOTTERY

TZS 1,000,000

USD 50,000 (annually)

2% on Gross Gaming Revenue (GGR) paid monthly

6.

COMMERCIAL LOTTERY (UNDER SEC. 41 (3) OF THE ACT)

TZS 1,000,000

USD 40,000 (annually)

-

7.

PRIVATE LOTTERY

TZS 5,000 (per lottery)

TZS 50,000 (per lottery)

-

8.

PUBLIC LOTTERY

TZS 5,000 (per lottery)

TZS 50,000 (per lottery)

-

9.

FETE

-

TZS 10,000 (per week)

-

10.

BINGO (IN A HALL OR CASINO

TZS 100,000 (annually)

TZS 500,000 (annually)

5% on  Gross Gaming Revenue (GGR) paid monthly

 11.

TOMBOLA (CLUBS OR REGISTERED SOCIETIES)

TZS 5,000 (per application)

TZS 10,000 (per month)

-

12.

PROMOTIONAL LOTTERY (PROMOTIONAL BUDGET BELOW TZS 5,000,000)

TZS 10,000 (per lottery)

TZS 100,000

(per month)

-

13.

PROMOTIONAL LOTTERY (PROMOTIONAL BUDGET OF TZS 5,000,000 OR ABOVE)

TZS 10,000 (per lottery)

6% (of total promotional budget)

-

14.

TRANSFER OF PERMIT

TZS 30,000 (per location)

-

-

15.

POSTPONEMENT OF DRAW

TZS 50,000

-

-

16.

KEY EMPLOYEE

TZS 10,000 (annually)

TZS 50,000 (annually)

-

17.

SUPPORT EMPLOYEE

-

TZS 10,000 (annually)

-

18.

DUPLICATE LICENCE

TZS 10,000

-

-

19.

AMUSEMENT WITH OR WITHOUT PRIZE

TZS 5,000

TZS 10,000 (per location)

-

20.

INSPECTION OF LICENCE HOLDERS REGISTER

TZS 20,000 (per inspection)

-

-

21.

POOL BETTING SCHEME

TZS 50,000 (annually)

TZS 50,000 (annually)

10% of bet amount

22.

FORTY MACHINES SITE LICENCE (DAR ES SALAAM)

TZS 100,000 (annually)

TZS 4,000,000 (annually)

-

23.

FORTY MACHINES SITE (OTHER REGIONS)

TZS 100,000 (annually)

TZS 2,000,000 (annually)

-

24.

SPORTS BETTING (SHOP)

TZS 500,000 (annually)

TZS 1,000,000 (annually)

-

25.

PRIZE COMPETITION

TZS 10,000 (per lottery)

10% of the Promotional Budget

-

26.

MANUFACTURER CERTIFICATE

TZS 500,000 (annually)

TZS 1,000,000 (annually)

-

27.

SELLERS/DISTRIBUTORS/SUPPLIERS

TZS 500,000

(annually)

TZS 1,000,000 (annually)

-

28.

SERVICE PROVIDER

TZS 500,000 (annually)

TZS 1,000,000

(annually)

-

29.

RETAILERS ON PREMISES

-

TZS 100,000 (Casino)

TZS 20,000 (Forty Machines Site)

TZS 10,000 (Slot Shops & Bars)

TZS 10,000 (Bingo)

-

30.

ACCREDITATION

-

TZS 10,000

-

31.

PRINCIPAL LICENCE (SPORTS BETTING)

TZS 500,000 (annually)

USD 30,000 (annually)

-

32.

PRINCIPAL LICENCE (SLOT OR ROUTE OPERATIONS)

TZS 500,000 (annually)

USD 10,000

(annually)

-

33.

INTERNET CASINO

TZS 1,000,000 (annually)

USD 40,000

(annually)

-

34.

OPERATIONS UNDER SEC.51(2)

TZS 1,000,000 (annually)

USD 10,000

(annually)

 

5% on Gross Gaming Revenue (GGR) paid monthly

35.

VIRTUAL GAMES

(IN SPORTS BETTING PREMISES)

TZS 50,000

(per location annually)

TZS 100,000 (per location annually)

5% on Gross Gaming Revenue (GGR) paid monthly

36.

ONLINE VIRTUAL GAMES

TZS 500,000 (annually)

USD 10,000 (annually)

5% on   Gross Gaming Revenue (GGR) paid monthly

37.

VIRTUAL GAMES (STAND-ALONE) PREMISE

TZS 50,000.00

(per location annually)

TZS 100,000 (per location annually)

 

5% on Gross Gaming Revenue (GGR) paid monthly

38.

CERTIFICATE OF SUITABILITY

-

TZS 1,000,000

-

39.

GAMING CONSULTANCY

TZS 10,000

TZS 1,000,000

(every two years)

-

40.

PLAY STATIONS

TZS 10,000 (per location annually)

TZS 50,000

(per location annually)

-

41.

INTERNET SPORTS BETTING

TZS 1,000,000 (annually)

USD 30,000 (annually)

-

42.

NUMBER GAMES

TZS 1,000,000 (annually)

USD 40,000 (annually)

-

 

 

Amendment of Second Schedule 20.  The principal Regulations are amended by deleting the Second Schedule and replacing it with the following new schedule:

 

Second Schedule

____________

(Made under regulation 68 (1))

Registration of devices

No.

Devices

Casino

Slot Machines Operations

Sports Betting

Forty Machines Site

Other Devices

1.

SLOT MACHINE

TZS    50,000

TZS   30,000

        -

TZS 40,000

-

2.

LIVE TABLES

 TZS 100,000

-

        -

 

-

3.

ELECTRONIC TABLES-SEATS

TZS    50,000

-

        -

TZS 50,000

-

4.

SPORTS BETTING TERMINALS

         -

          -

TZS   30,000

         -

-

5.

POOL TABLES

         -

          -

         -

         -

TZS 10,000

6.

PLAY STATIONS

         -

          -

         -

         -

TZS 10,000

 

Additional of new Schedule

21.

The principal Regulations are amended by adding immediately after the Second Schedule the new Schedule as follows:

 

Third Schedule

____________

Made under Section 85 (2) (g)

Administrative Sanctions to Licensee

No.

RELEVANT CLAUSE OF THE GAMING ACT, 2003 OR REGULATIONS

ACTS, OMISSIONS OR OFFENCE COMMITTED

 

SANCTIONS: PENALTY

Gaming Act, Cap 41.

1.

Section 15(2)

Failure to renew licence within prescribed time

Penalty of 5% of the required licence fee and an Interest of 25% of the penalty for every month delay

2.

Section 82A (c)

Placing Machines on un–Authorized Premise

TZS. 1,000,000 (per location)

3.

Section 86B

Failure for a licensee to comply with requirements of Section 86B

TZS. 1,000,000 for every day of delay.

 

GAMING REGULATIONS, 2003

4.

Regulation13

Failure of a licensee to display a gaming licence in a gaming premise

TZS. 100,000 (per location)

5.

Regulation 18(4)

Failure to inform the Board on suspension and recommencement of business

TZS. 500,000

6.

Regulation 18(5)

Failure to file a report to the Board for approval of transfer of any share prescribed under Regulation 18(5)

TZS. 7,000,000

7.

Regulation 25 & 26

Failure of a licensee to develop and implement organisation structure prescribed under Regulation 25 and 26

TZS. 300,000

8.

Regulation 27

Failure of a licensee to prepare and implement the requirements of job compendium prescribed under Regulation 27

TZS. 300,000

9.

Regulation 29&32

Employ key and support staff without gaming license

TZS. 100,000 (per person)

10.

Regulation 34& 60

Failure of Key or Support employee to make available and display of employees gaming license for inspection set under Regulation 34 and 60.

TZS. 20,000 (per person)

11.

Regulation 38

Failure to comply with the minimum requirement of theoretical and demonstrable return to public prescribed under Regulation 38

TZS. 1,000,000

12.

Regulation 39 & 40

Breach of Regulation 39 or 40 in relation to the use and approval of chips, tokens

TZS. 500,000

13.

Regulation 44 to 48

Failure of licensee to comply with the requirements relating to installation, operation and maintenance of surveillance system, records as prescribed under Regulation 44 to 48

TZS. 10,000,000

14.

Regulation 64

Failure to display winning combinations together with corresponding prizes on every slot machine in violation of Regulation 64

TZS. 100,000

15.

Regulation 65

Failure to comply with the minimum requirement of theoretical and demonstrable return to public prescribed under Regulation 65

TZS. 500,000

16.

Regulation 68

Failure to Register Gaming Device

TZS. 40,000 (per device)

17.

Regulation 74& 78

Breach of requirement in relation to conventions of gaming machine set under Regulation 74 and Regulation 78

TZS 5,000,000

18.

Regulation 82

Failure to submit annual audited financial

statements with any of the requirements prescribed under Regulation 82

TZS. 1,000,000

19.

Regulation 84 (4)

Failure to submit gaming levy within prescribed time

Penalty of 10% of the required gaming levy and an Interest of 25% of the penalty for every month delay.

INTERNET GAMING REGULATIONS 2021

20.

Regulation 9 (1)

Failure to have sever in Mainland Tanzania

TZS.7,000,000

21.

Regulation 9 (2)

Failure to obtain approval of having a replica sever

TZS.7,000,000

22.

Regulation 19(3)

Failure to inform the Board on the incident which the licensee is unable to resolve under Regulation 19(4) (a)

TZS. 300,000

23.

Regulation 21

Failure to notify the Board of any unclaimed non-monetary prize

TZS. 300,000

24.

Regulation 23

Failure of a licensee to inform the Board circumstances of incident that prizes was withheld

TZS. 300,000

25.

Regulation 25

Failure of a licensee to display prizes on every game offered for play under Regulation 25

TZS. 1,000,000

26.

Regulation 56

Failure of a licensee to keep records as per requirements of Internet Gaming Regulations, 2021

TZS. 5,000,000

 

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...