Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) imewawezesha wakulima wadogo kupata mikopo ya shilingi bilioni 140 kwa ajili ya kuwainua katika shughuli zao.

Afisa Mwandamizi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Andrew Kimbelwa ametoa taarifa hiyo wakati wa maonesho yanayoenda sambamba na maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani inayofanyika katika viwanja vya nanenane Mkoani Tabora.

Kimbelwa amesema, benki hiyo imekuwa mshirika mkubwa wa ushirika hapa nchini na wametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuendeleza ushirika katika maeneo mbalimbali nchini.

"TADB imekua mshirika wa karibu wa shughuli za ushirika na mpaka sasa tumeishatoa zaidi ya shilingi bilioni 140 kwa ajili ya kuendeleza ushirka"Amesema Kimbelwa

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inashiriki maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani ambapo kitaifa yanafanyika Mkoani Tabora


 Afisa Mwandamizi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Andrew Kimbelwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...