Na John Walter-Manyara.


Mtu mmoja aliefahamika kwa jina la Danile Abraham (40) mkazi wa kijiji cha Kitwai A wilayani Simanjiro mkoani Manyara amefariki dunia baada ya kushambuliwa na Nyati wakati akipeleka ng'ombe kunywa maji jirani na hifadhi ya taifa ya Tarangire.


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Limited Mhongole amethibitisha kutokea kwa tukio hilo wakati akizungumza na vyombo vya habari leo agosti 16 ambapo amesema limetokea agosti 9 mwaka huu kijijini hapo.


Aidha kamanda Mhongole amewataka wananchi wanaoishi karibu na hifadhi za wanyama pori kuchukua tahadhari dhidi ya wanyama wakali ili kuweza kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyama hao.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...