Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwasa pamoja na viongozi mbalimbali wakati alipowasili Hifadhi ya Taifa ya Mikumi mkoani Morogroro leo tarehe 16 Agosti 2022. Hapo kesho tarehe 17 Agosti 2022 Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi Magari maalum yatakayotumika katika kuboresha Miundombinu ya Utalii yaliotolewa na Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) Mikumi mkoani Morogoro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...