Ramadhani Selemani akipatiwa chanjo ya UVIKO-19 na Matilda Seda (muuguzi)katika viwanja vya Ilulu mkoani Lindi katika uzinduzi wa kampeni ya uchanjaji mkoani humo.
======== ======= =======
Ruvuma
Jumatano 10 Agosti 2022. Tangu kuzinduliwa kwa chanjo ya UVIKO-19 na
Rais Samia Hassan mnamo Julai 2021, na baadae kufuatiwa na kampeini nchi
kote kuhusu chanjo, Wizara ya Afya lengo la Kujanja Watanzania kwa
asilimia 70 mpaka mwisho wa mwaka huu kwa kushirikiana na wafadhili
pamoja na wadau wa maendeleo. Wizara ya Afya ilikuja na mbinu tofauti za
kuhamashisha wananchi kujitokeza ili kupata chanjo.
Baadhi ya
mbinu ni kuwatumia wanasiasa, viongozi wa vijiji na viongozi wa dini,
kutumia watoa huduma wa afya ndani ya jamii. Mbinu hizi ziliiwesha Mkoa
wa Ruvuma kuweza kufikia lengo la taifa la Kujanja zaidi ya asilimia 70
ya wananchi kabla hata mwaka kumalizika.
Na ili kuweza kuendelea
kutoa chanjo ya UVIKO-19 na hatimaye kufikia asilimia 100, kampeini ya
kuhamashisha na kutoa elimu juu ya chanjo yenye kauli mbiu Mziki Mnene
Ujanja Kujanja ilizinduliwa mkoani Ruvuma mwishoni mwa wiki huku
akiongozwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya wakiwemo Marioo, Snura,
Ney wa Mitengo, Stamina, Mr Blue, ManFongo, Jay Melody, Baddest 47 na
Tunda Man. Tamasha hili lilifanyika kwenye viwanjwa vya Maji Maji mjini
Songea na iliandaliwa na na Wizara ya Afya kupitia kitengo cha Elimu kwa
Umma, pamoja na FHI 360 kupitia mradi wa EpiC kwa ufadhili wa Shirika
la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID).
Wizara ya Afya
kupitia kitengo cha Elimu kwa Umma imekuwa ikitumia matamasha ya muziki
kutoa elimu na kuhamashisha jamii juu ya umuhimu wa kupata chanjo ya
UVIKO-19. Mpaka kufikia sasa, matamasha hayo yameweza kufanyika kwenye
mikoa ya Lindi, Mtwara ra Ruvuma.
Akizungumza wakati wa tamasha
hilo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Louis Chomboko alisema kuwa mkoa wa
Ruvuma kwa sasa umeweza kuvuka lengo la taifa la kutoa chanjo kwa
asilimia 70. ‘Lengo la taifa ni kutoa chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi
wake kwa asilimia 70 kabla ya mwisho wa 2022. Naomba nichukue fursa hii
kusema kuwa sisi Mkoa wa Ruvuma tayari tushavuka lengo hili. Haya ni
mafanikio makubwa kwa kuwa mkoa wetu unapakana nan chi jirani wetu nah
ii inaonyesha ni kwa jinsi ngani tumejitolea kuwakinga wananchi wetu’.
Chomboko
aliongeza, ‘Nachukua fursa hii kushukuru Wizara ya Afya, viongozi wa
kitaifa, USAID pamoja na wadau wetu FHI 360 kupitia mradi wa EpiC kwa
kuhakikisha kuwa inapatikana muda wote, lakini zaidi ni kwa kutoa elimu
na kuhamashisha jamii yetu juu ya umuhimu wa kupata chanjo ya UVIKO-19.
Naomba kuwahakikishia kuwa tutaendelea kuweka nguvu kwenye kampeini hii
ili kila mwananchi ambaye anastahili kupata chanjo anapata kwa ukaribu
kwenye hospitali zetu za umma, kwenye vituo vya afya pamoja na maeneo
mengine ambayo yameruhusiwa kutoa chanjo kwa kufuata taratibu
zikizowekwa na serikali’.
Kampeini ya chanjo ya UVIKO-19 ambayo
inaratibiwa na Wizara ya Afya kupitia kitengo cha elimu wa umma pamoja
na wadau FHI 360 kwa ufadhili wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya
Kimataifa (USAID) kwa kauli mbiu Bega kwa Bega, Ujanja Kujanja
itaendelea kwenye mikoa ya Njombe na Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa
Ruvuma Laban Thomas alitoa pongezi kwa viongozi wa afya wa mkoa kwa
kuweka nguvu na kufanikisha lengo la taifa la kutoa chanjo. ‘Kwa kuwa
mkoa wa kwanza kufikisha lengo hili la taifa, inaonyesha ni kwa jinsi
ngani mumejitolea kusaidia wananchi wetu. Kwa kutumia njia zenu wenyewe
kufikisha lengo na sasa kwa kutumia tamasha hili la muziki ambalo
limeweza kuvuta umati mkubwa wa wananchi, nina uhakika mtaendelea
kufanya vizuri zaidi’.
EpiC ni mradi wa kimataifa wa miaka
mitano unaotekelezwa na shirika la FHI360 kwa ufadhili wa Mpango wa
Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) pamoja na
Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), uliojikita katika
kufikia na kuendeleza udhibiti wa janga la VVU/UKIMWI katika Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania. Hii ni kupitia kutoa msaada wa kitaalamu na
huduma za moja kwa moja katika kuondoa vikwazo vilivyopo kufikia
95-95-95, na kuhamasisha usimamizi wa kujitegemea wa miradi ya
VVU/UKIMWI kitaifa kwa kuboresha programu za utambuzi wa hali ya
maambukizi ya VVU, kinga, matunzo na tiba.
#UjanjaKuchanja #TanzaniaInachanja
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...