Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi na Askari wahitimu wa Mafunzo ya Awali Kozi Na. 1,2022 ya Jeshi la Uhamiaji pamoja na Wananchi katika Hafla ya Ufungaji wa Mafunzo hayo iliyofanyika katika Chuo cha Uhamiaji Boma Kichakamiba Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga tarehe 15 Agosti, 2022.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi Cheti kwa Mshindi wa Jumla kwenye Mafunzo ya Awali Kozi Na. 1,2022 ya Jeshi la Uhamiaji Konstebo Geofrey Felician Zakaria, wakati wa Ufungaji wa Mafunzo hayo yaliyoshirikisha jumla ya Wahitimu 818 katika Chuo cha Boma Kichakamiba Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga tarehe 15 Agosti, 2022.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Uhamiaji kuondoa urasimu wa utoaji vibali vya kuingia nchini (Visa) kwa wageni.

Rais Samia ametoa agizo hilo leo wakati wa hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali ya Askari wa Jeshi la Uhamiaji Kozi na. 1/2022, katika Chuo cha Uhamiaji cha Boma Kichakamiba.


Aidha, Rais Samia amesema Idara hiyo haina sababu ya kuchelewesha wageni kupata vibali vya kuingia nchini kwa kuwa wanatumia mifumo ya kisasa ya kielektroniki katika utoaji wa vibali hivyo.


Vile vile, Rais Samia amemuagiza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala kuwarudisha mafunzoni Maafisa na Askari waliopo kazini kupata mafunzo tena chuoni hapo.


Pia, Rais Samia ametaka kuwepo kwa mafunzo baina ya vikosi vya Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini ili kupata uzoefu wa pamoja.


Rais Samia amelitaka Jeshi la Uhamiaji kubuni njia mbalimbali zitakazosaidia kuimarisha utendaji ili kukabiliana na mabadiliko ya kiteknolojia na mbinu mpya za uhalifu zinazojitokeza.


Haya ni mafunzo ya kwanza kwa Uhamiaji tangu kuanza kujitegemea kwa Jeshi hilo ambapo Askari wa uhamiaji 818 wamehitimu na mafunzo hayo kupewa jina la Operesheni Ujenzi.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...