Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Sendiga akiwa na viongozi wa CCM Mkoa wa Rukwa Leo alipowasili rasmi mjini Sumbawanga ambapo amesema yupo tayari kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kuleta maendeleo kwa wananchi.

(Habari na Picha na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa)

…………………………

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mheshimiwa Queen Sendiga leo (09.08.2022) amewasili katika Kituo chake cha kazi Mkoa wa Rukwa kufuatia kuteuliwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan hivi karibuni.

Mapema akiwa mjini Sumbawanga amesaini kitabu cha wageni katika Ofisi Kuu ya CCM Mkoa wa Rukwa ambapo amewaeleza kuwa amekuja kufanya kazi kwa ustawi wa Wana Rukwa na Taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Rainer Lukala amemkaribisha kiongozi huyo na kumuahidi kuwa CCM itashirikiana naye kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Donald Nssoko kesho Agosti 10 Mkuu huyo wa Mkoa wa Rukwa atakabidhiwa rasmi ofisi toka kwa mtangulizi wake Mheshimiwa Joseph Mkirikiti tukio litakalofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Sumbawanga.

Mheshimiwa Sendiga anahamia Mkoa wa Rukwa kutokea Mkoa wa Iringa kufuatia uteuzi uliofanywa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...