Na Mwandishi wetu, Rombo
MKURUGENZI
Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA)
Mhandisi Clement Kivegalo, amemuagiza Mkandarasi Kampuni ya Best One
Ltd, inayotekeleza miradi miwili ya wilaya ya Rombo itakayogharimu jumla
ya Sh. 5.3 bilioni kuikamilisha kwa wakati ili shida ya maji Rombo
imalizike.
Akizungumza
baada ya kukagua utekelezaji wa miradi hiyo, Mhandisi Kivegalo amesema
Miradi hiyo, ambayo inatekelezwa kwa pamoja baina RUWASA na Mamlaka ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Rombo ni lazima ikamilike kwa wakati ili
wananchi wa Rombo wapate huduma muhimu ya maji.
"Nimekuja
Rombo na wataalam wangu kuona utekelezaji wa miradi ya maji ndani ya
Wilaya ya Rombo kufuatia wito uliotolewa na Mbunge wa Rombo baada ya
kuona utekelezaji unasuasua. Aidha, nimetembelea pia Mradi wa Njiro II
unaotekelezwa kwa fedha za UVIKO-19 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. Nimefarijika kuona kuwa
Mradi wa UVIKO-19 umekamilika kwa kiasi kikubwa na tayari baadhi ya
vijiji vimeanza kupata maji, hivyo tunataka kasi iongezeke" amesema.
Amesema
kuna changamoto kidogo katika utekelezaji wa miradi miwili mojawapo
ikiwa ni ucheleweshaji wa msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani hivyo,
amekutana na wataalam wake na Mkandarasi kujadiliana nao.
"Moja
kati ya miradi hii, ambao ulilalamikiwa kuchelewa ulikuwa chini ya
Mamlaka ya Maji Rombo na sasa RUWASA tutashirikiana nao kuona
unakamilika, kama ambavyo wameomba," amesema
Hata
hivyo, Mkurugenzi huyo wa RUWASA amesema changamoto katika miradi hiyo
zitapatiwa ufumbuzi na amemtaka Mkandarasi kuharakisha utekelezaji wa
miradi ili wananchi wa Rombo wapate maji.
Kaimu
Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Rombo, Martin Kinabo ameaema kwa sasa
miradi ambayo inatekelezwa katika wilaya hiyo ni miwili mradi wa Njoro
II, ambao utagusa vijiji 15 utasaidia wananchi 24,454 ambao utagharimu
Sh. 3.4 bilioni.
Amesema
mradi mwingine ni mradi wa Ona ambao utahusisha vijiji 29 na utagharimu
Sh. 2.9 bilioni na miradi yote inaendelea vizuri.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Best one Ltd, Juma Mvamba ameahidi kukamilisha miradi
hiyo kwa wakati endapo atawezeshwa malipo ya awali na mahitaji mengine
kama msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani.
"Tunaendelea
kutekeleza mradi mmoja, mwingine tayari umekamilika na wananchi
wanapata maji na RUWASA wameahidi kutusaidia kukamilisha mradi kwa
wakati" amesema.
Hivi
karibuni Mbunge wa jimbo la Rombo, Profesa Adolf Mkenda akiwa katika
ziara kwenye jimbo lake, alilalamika kuchelewa kukamilika mradi mmoja na
kutaka RUWASA makao makuu kuingilia kati ili wananchi wa Rombo wapate
maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...