Wa pili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kaskazini TMDA Proches Patrick,akiwa pamoja na wafanyakazi kutoka Mamlaka hiyo wakifurahia kombe mara baada ya ushindi wa pili wa Taasisi za Usimamizi na Udhibiti nanenane 2022


Mmoja wa Mtumishi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba akiendelea kutoa elimu katika Maonyesho ya Nanenane katika viwanja vya Themi Njiro Mkoani Arusha 2022


Dawa ambayo inajulikana kwa jina la 60 minutes- Male Genital Desensinsitizer Spray (The Delay Spray for men)iliyokamatwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba katika mpaka wa Namanga.


Dawa inajulikana kwa jina la Increase MK II (Men’s Penis enlargement) kuongeza maumbile kwa wanaume,iliyokamatwa katika mpaka wa Namanga .





Na.Vero Ignatus,Arusha

Mamlaka ya Vifaa Tiba TMDA Kanda ya kaskazini imetoa wito kwa jamii kuwa makini wakati wanaponunua dawa na kuwataka kuzichunguza vizuri kabla ya kuzitumia na kama watakuwa na mashaka juu ya dawa hizo, watoe taarifa kwa Mamlaka hiyo ili hatua za haraka za kisheria zichukuliwe

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kaskazini TMDA Proches Patrick kwenye Maonyesho ya sikukuu za nanenane viwanja vya Themi Jijini Arusha 8/8/2022,kwamba dawa bandia ni tatizo kwani wapo waingizaji na wasambazaji ambao siyo waaminifu ,wanaojali maslahi yao kuliko Afya za walaji, jambo ambalo husababisha madhara kwa binadamu,na kupunguza uaminifu kwenye mfumo mzima wa utoaji huduma ya Afya.

Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kaskazini TMDA aliainisha baadhi ya dawa zilizokamatwa na Mamlaka hiyo,ambazo hazijasajiliwa ni Pamoja na 60 minutes- Male Genital Desensinsitizer Spray (The Delay Spray for men) inayosababisha kuchelewa kufika kileleni kwa mwanaume,Pamoja na Increase MK II Men’s Penis enlargement) kuongeza maumbile kwa wanaume

‘’Dawa hizi tumezikamata hazijasajiliwa na wala hazina vibali vya usambazaji na uuzaji wa dawa hizo nchini,na wala sisi kama TMDA hatujaitathimini na kusajili dawa hizi kabla ya kuruhusiwa kuingia sokoni maana sisis tunasimamia ubora usalama na ufanisi wa dawa vifaa tiba na vitendanishi .Alisema Proches

Adha alisema kuwa lengo kuu la Mamlaka hiyo kushiriki katika maonyesho ya sikukuu ya nanenane ni kutoa elimu kwa wananchi kwani Aya yao ndiyo mtaji wao hivyo wakiwa na afya bora wataweza kufanya shughuli za uzalishaji mali,na uchumi vizuri.

TMDA imewataka Wananchi kutambua kuwa kutumia bidhaa ambazo hazijasajiliwa ni kuhatarisha Afya zao,maana hawajui mtengenezaji alikuwa anakusudia kutengeneza kitu gani ,hivyo jukumu kubwa ni kuhakisha kwamba vitu ambacho mwananchi wanakitumia ni kile ambacho Mamlaka imethibitisha.

‘’Mamlaka inaendelea kuwakamata wale wote wanaovunja sheria na kuwafikisha mahali panapowastahili, wananchi nunueni bidhaa kwenye maduka yaliyosajiliwa na TMDA na Tasisi za Serikali ,msinunue kwenye vyombo vya usafiri,wala wale wanaopitisha bidhaa mkononi ,nunueni sehemu ambayo mtapewa risiti halali’’Alisisitiza

Aidha maonyesho hayo ya 28 ya Nanenane 2022 yamebeba Kauli Mbiu isemayo Ajenda 10/30 Kilimo ni Biashara Shiriki Kuhesabuiwa kwa Mipango Bora ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...