Na Mwandishi wetu, Babati
MKOA wa Manyara umepata viongozi wapya wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wa Wilaya sita za Mkoa huo.

Katibu wa UVCCM Mkoa wa Manyara, Ibrahim Kandumila akizungumza mjini Babati amesema uchaguzi huo umekamilika kwa asilimia 100 na kufanyika kwa amani.

Amewataja wenyeviti hao waliochaguliwa na wilaya zao kwenye mabano ni Solomon Mekiory (Babati vijijini), Justin Ammi (Hanang') na Magdalena Urono (Babati mjini).

Amewataja wengine ni Hamza Mngia (Kiteto), Timothy Mollel (Simanjiro) na Elisante Michael (Mbulu).

"Nawapongeza na kuwashukuru wote walioshinda ila watimize majukumu yao ipasavyo na ambao kura hazikitosha wawape ushirikiano wale walioshinda," amesema Kandumila.

Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Babati Vijijini Solomon Melkiory amewashukuru wajumbe wa jumuiya hiyo kwa kumchagua ili awaongoze na ameomba ushirikiano kwao.

Mwandishi wa kituo cha FM Manyara na AYO TV, Charles Mangwe ambaye ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Babati Vijijini kupitia UVCCM amewashukuru wajumbe kwa kumpa kura za ushindi.

Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Babati mjini kupitia UVCCM Husna Mdinku ameomba ushirikiano kwa wajumbe hao na kuahidi kuwaunganisha kupitia nafasi hiyo.

Mjumbe wa mkutano mkuu wa UVCCM Wilaya ya Babati mjini Elias Ernest ambaye ni mwandishi wa kituo cha Wasafi amewashukuru wajumbe kwa kumpatia nafasi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...