Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa pongezi kwa  Bondia  Mtanzania Twaha Kiduku  kwa kumchapa kwa alama  za majaji wote watatu (unanimous decision)  Bondia  Abdo Khaled kutoka  Misri, usiku wa Septemba 24, 2022 Mtwara.

Kwa ushindi huo, bondia Kiduku ameweza  kutetea  ubingwa wake wa  UBO Afrika (UBO all Africa Champion)  na Mkanda mpya wa ubingwa wa Mabara (UBO Intercontinental).

Hili ni pambano la 20 kushinda  kwa Kiduku , akitoka  sare 1 na kupoteza  8 akiwa na rekodi ya kucheza  mapambano 29.

Mhe. Mchengerwa amefafanua kwamba dhamira ya Serikali  kwa sasa ni kutumia michezo kuitangaza Tanzania.

Aidha, ametoa wito kwa wanamichezo kuthamini michezo na kufanya kama kazi inayoweza kubadili maisha yao na kuinua uchumi wa nchi kwa ujumla.

Amesema, Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan itaendelea kusaidia wanamichezo wanaofanya vizuri ili wafike mbali.

Kwa upande wake muandaaji wa pambano  hilo Selemani Semunyu  ameishukuru Serikali ya Awamu  ya Sita  chini ya Rais Samia kwa mchango mkubwa wa uwekezaji  inayofanya  kwenye sekta za michezo na sanaa.

Amesema wao kama wadau wataendelea kuonesha  vipaji walivyonavyo vijana na kuomba wadhamini kujitokeza kusaidia maandalizi, kwani kwa kutegemea viingilio pekee ni ngumu kukidhi gharama.

"Na Sasa dhamira yetu ni kufanya pambano kubwa Dar es Salaam au mkoa ambao unaweza kusaidia katika kutafuta udhamini wa pambano hilo" amefafanua Semunyu.

Pambano hilo lilipambwa na mapambano ya utangulizi ambayo yalikuwa na mvuto mkubwa kwa wadau hususan pambano  baina ya Emmilian Polino (JKT) na Osama Arabi (Mtwara) baada ya  bondia chipukizi Osama  kuonesha  kiwango  kikubwa  hadi mwisho wa mchezo licha  ya kushindwa katika pambano hilo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...